RIWAYA; BARUA KUTOKA JELA
MTUNZI; IBRAHIM GAMA
SEHEMU YA ISHIRINI NA SITA
SIMU/WHATSAPP 0718603654 / 0688039464
Timamu Afande Coplo Dihenga alimwambia
Inspekta Jamila, huku akiwa katika ukakamavu,
kuonesha heshima kwa mkubwa wake.
Inspekta Jamila, alipanga timu yake, dakika ishirini
na tano baadae, gari mbili za kiraia, aina ya
TOYOTA NOAH zikiwa na askari nane, wenye silaha
za kivita smg, walikuwa wamezipakata katika
miguu yao, huku Inspekta Jamila, na Sagenti
Kubuta, wakiwa katika gari ndogo Toyota Soluna,
ikikamilisha idadi ya gari tatu, zinazoelekea eneo la
Kongowe,katika wilaya ya Temeke.
*******
Jeradi Mwaipopo akiwa na mtu aliemwita nduguye,
anaeitwa Mwakyembe Anthony, baada ya kutoka
katika hospitali ya taifa ya Muhimbili, wakitumia
usafiri wa Mwakyembe, pikipiki aina Boxer kutoka
India.Ikiendeshwa na Mwakyembe, walivaa
elementi wakawa wanaonekana kama abiria
amepanda Bodaboda!
Safari yao, ilielekea Maeneo ya wilaya ya
Temeke,katika eneo liitwalo Kongowe, kama
unaelekea Mkuranga, nyumbani kwake
Mwakyembe.
Walipofika waliingiza pikipiki ndani, wakafunga geti
na kukumbatiana upya, kama watu waliokuwa
hawajaonana muda mrefu nyuma.
Asante sana ndugu yangu, kumbe bado
unakumbuka maagizo yangu kuwa, nikikwita na
kukwambia njoo unifae, namaanisha nini?!
Jeradi Mwaipopo alimwambia mtu aliependa
kumwita ndugu yake, kwa sababu wote walikuwa
wanatoka katika mkoa mmoja wa Mbeya.
Naam nakumbuka sana, kwani natambuwa kama
umeshakamatwa, kwani nilikuwa nafatilia kwa
karibu sana. Ndiyo maana uliponiambia nije
nikufae, upo muhimbili,kisha ukanitaka nije na
chakula kwa ajili ya wale askari, nikatambuwa
natakiwa nifanye nini! Nilipita duka la dawa pale
muhimbili, nikanunua zile Njunja(LAGACTIL)
nikimwambia muuzaji, ndugu yangu anasumbuwa
mwenye ugonjwa wa akili akiwa hospitali, na
manesi wa pale muhimbili, wamenielekeza nije
kununua dawa zao za usingizi hapa! Naomba
nisaidie dada yangu. Basi Yule muuzaji wa duka la
dawa Muhimu. Alinipa dozi kabisa, nami nikampa
elfu ishirini, nikimwambia chenji aendelee nayo!
Nikaenda pale karibu na Geti lakuingilia, upande
wa kushoto, nikanunua maziwa paketi mbili,
nikanunua na chipsi mayai, na kuku, nikasaga zile
dawa za wehu za usingizi, nikazinyunyizia katika
kile chakula, nikamtafuta Yule askari katika namba
yake, akanielekeza ndiyo nikaja kukufaa! Nilidhani
wangenambia nionje kile chakula, basi ningeonja
kisha ningekunywa yale maziwa pakiti moja
kuondosha ile sumu ya zile dawa, nabado balaa
lingekuwa upande wao!
Mwakyembe alihitimisha taarifa yake, kwa JM
huku akiwa na wingi wa furaha. Asante sana
ndugu yangu kwa kunifaa, kwani nilikuwa sina mtu
mwengine zaidi yako, ambae ni shababi na
anaeweza kucheza mchezo ulioufanya leo! Sasa
kuanzia sasa, jeshi la polisi litakuwa linakutafuta
wewe pamoja na mimi, hivyo umakini unahitajika
sana! Nakupongeza kwa kuchukua simu za wale
askari, kwani wangebaki nazo, ile simu uliyoipigia
namba yako ingebaki, na wangekusumbua, ila kwa
kuwa umeichukuwa, umefanya jambo la maana
sana!
JM alimwambia Mwakyembe huku akimtizama
kama alikuwa na neno la ziada, alipomuona
hakuwa na neno, aliendelea. Itabidi mie niondoke
sasa hivi nielekee nyumbani kwangu Vingunguti,
kwani kule ndiyo kuna hazina, na nikiwa kule
hujihisi nipo pahala salama zaidi. Jm alisema
maneno yale na kutulia huku akijinyoosha viungo
vyake!
*******
Nipe taarifa tafadhali, amebadilisha eneo?
Inspekta Jamila alikuwa akiwasiliana na Koplo
Dihenga kutoka makao makuu.
Hapana Afande, inaonekana bado yupo hapohapo,
kwani Imei inasomeka bado katika mnara huohuo,
akiwa katika usawa uleule wa nyumba ya kumi na
mbili,upande wa kusini, kutoka katika mnara.
Alijibu Koplo Dihenga, huku akiwa anaangalia
katika kompyuta iliyokuwa mbele ya macho yake!
Sawa Koplo umesomeka, nipo Mbagala Kizuiani
nasonga eneo la tukio, tafadhali hakikisha hupotezi
lada! Alihitimisha Inspekta Jamila, kisha akakata
simu. Akawa anaangalia mbele huku akiwa kimya
na mawazo tele!
Sagenti Kubuta, alikuwa anaendesha gari
akiongoza msafara ule, huku akiombea wahusika
wanaowafata, wawakute ili wamalizane nao!
Wakiwa njiani eneo la Mbagala rangi tatu, simu ya
Inspekta Jamila iliita, nae kwa papara akaitwaa
simu yake, nakuitazama namba inayopiga, na hata
alipoiona akaipokea simu ile chapu kwa haraka!
Unasomeka nipe taarifa! Ilikuwa ni simu ya Koplo
Dihenga kwa Inspekta Jamila. Afande simu ya
Konstebo Iddy Gebo, imewashwa katika mnara
huohuo, ila imetolewa line iliyosajiliwa simu hiyo,
na sasa imewekwa line nyingine! Hapa inasoma
imei yake katika mnara, umenisoma mpaka hapo?
Alimaliza taarifa yake Koplo Dihenga kwa swali. Na
Inspekta Jamila kwa wahaka mkubwa alimjibu.
Nimekusoma Koplo, hiyo inaonesha mtu
mwengine yupo na Mwakyembe, anaweza kuwa ni
JM, au Mwakyembe ameamua aitumie pia simu
yapili! Endelea kunijuza tafadhali,nakaribia eneo la
tukio nipo Tanita mpakani mwa Mbagala na
Kongowe! Alijibu Inspekta Jamila na Koplo
Dihenga akakata simu.Dakika kumi baadae,
wakawa eneo la Kongowe,wakiikaribia nyumba
husika, Inspekta Jamila akampigia Koplo Dihenga,
na kumwambia Nipo eneo la tukio, je kupo vilevile,
au kuna badiliko?! Koplo Dihenga aliangalia
komptuta yake akamwambia. Afande simu ya
Constebo Iddy Gebo, imezimwa kama dakika tano
hivi, ila simu ya Mwakyembe bado taa ya mnara
inasomeka yupo hapohapo! Alisema Koplo Dihenga
na Inspekta Jamila,akamwambia Labda itakuwa
imezimika chaji, ngoja tufanye ambushi tutajuwa
hapo hapo ndani, je hapa tumeshahesabu nyumba
ya kumi na mbili, kutoka katika mnara wa simu,
unaoonekana mbele yetu, kwa upande wa kusini,
upo sahihi na data?
Hapo sahihi kabisa mkuu, hakuna shaka na data,
endelea na kazi mkuu!
Koplo Dihenga, alimjibu mkubwa wake akiwa
anajiamini na majibu yake!
Inspekta Jamila, alikata simu, nakupanga timu
yake kuzunguka nyumba ile, kisha yeye akaenda
mlangoni nakulijaribu geti la nyumba ile, akaliona
limefungwa nganganga! Akamtizama Sajenti
Kubuta, kama aliekuwa anataka msaada, Sajenti
Kubuta, akamwambia kiongozi wake. Plani B plus
mkuu!
Na hata alipokwisha kusema maneno yale,
Inspekta Jamila akamjibu Plani B, Sajenti!
Kufumba na kufumbua askari wale waliparamia
ukuta wa nyumba ile, huku baadhi ya raia
wakishangaa kwa kitendo kile, lakini kwa kuwa
wao walikuwa kazini, wala hawakutaka kuwajali,
waliendelea na hamsini zao. Askari wanne
walikuwa juu ya ukuta, na wanne walibaki
chini.Wale askari waliokuwa chini, kila mmoja
alikuwa na silaha, aina ya SMG,akiwa ameikamata
barabara, akiwa doria katika pembe ya nyumba ile,
akihakikisha kwamba hakuna mtu, asiyekuwa wao
ataeruka kupitia ukuta wa pembe aliyokuwepo!
Inspekta Jamila, Sajenti Kubuta, na askari wawili,
wataalam wa mapambano ya mikono, wote kwa
pamoja waliparamia ukuta wa nyumba ile uliokuwa
na ruva nyingi, kwa ajili ya kuruhusu hewa
kuingiza kwa wingi ndani ya nyumba ile. Kwa
ustadi mkubwa waliparamia na kufika juu kabisa
ya ukuta ule usiopungua futi nane urefu wake,
wakachuchumaa huku mikono yao, ikiwa imezama
viunoni mwao, ilipokuja ibuka ilikuwa imekamata
silaha ndogo ya Bastola mikononi mwao! Vitendo
vyote hivyo vilikuwa vikifanyika kwa pamoja tena
bila kelele! Wote wakiwa pale juu ya ukuta na
bastola mikononi mwao, waliruka pamoja hadi
chini ndani ya uwa wa nyumba ile, wakibimbilika
walipofika chini na kulalia tumbo huku silaha zao,
zikielekezwa mbele tayari kwa matumizi! Walilala
pale chini kwa sekunde kadhaa, walipoona kimya
hakuna rabsha yoyote iliyotokea, walitambaa kwa
matumbo,na viwiko vya mikono, wakiufata mlango
mkubwa wa kuingilia ndani, huku wakichelea
kuonekana kama wangelisimama kupitia dirisha
lililokuwa pana mbele yao! Na hata walipoufikia
mlango, waliukuta mlango ule umefungwa kwa
funguo, nyumba ikiwa kimya kabisa!
Sasa wakainuka huku wakijigawa wawili kila
pande, waliegemea ukuta, huku silaha zao sasa
zikikamatwa kwa mikono miwili, zikiwa
zimeelekezwa juu!
Inspekta Jamila, alitoa ishara kwa wenzake, na
kitendo bila kuchelewa, Sajenti Kubuta alirudi
nyuma, kisha akapiga hatua kubwa na kupitia bega
lake, aliukumba ule mlango kwa kishindo kimoja
kikubwa, na ule mlango bila khiyana, ukafungukia
kwa ndani kwa kasi na kujipigiza ukutani!
Askari wale wote wakalala chini kifudifudi kwa kasi
ya ajabu,na kutulia pale chini huku sasa wakiwa
wanaitazama korido ikiwa tupu haina mtu! Pia
wakijikinga kama adui akiwa na silaha,basi kama
angefyatua risasi, risasi ile ingepita juu, na wao
wangekuwa salama. Askari wale waliinuka kwa
ghafla wawili wakiwa upande wa kulia, na wengine
wawili wakiwa upande wa kushoto. Wakatembea
na ukuta huku wakiwa makini, safari hii wakiwa
katika mwendo wa kunyata, askari mmoja wakila
upande wa mbele alikuwa ameielekeza silaha yake
mbele, na aliekuwa nyuma yake, aliielekeza silaha
yake nyuma! Kifupi ilikuwa kila mmoja alikuwa
akimlinda mwenzake, huku wakisonga mbele!
Walipofika usawa wa iliyoonekana kama mwanzo
wa sebule, walisimama huku wakiegemea ukuta, na
Inspekta Jamila kupitia mkono mmoja, alikuwa
anatowa ishara, ilihali mkono mwingine, alikuwa
amekamata silaha yake sawasawa. Askari wale
kila mmoja alitikisa kichwa kuwashiria kuwa
ameelewa maelekezo aliyokuwa anayatowa
kiongozi wao.Inspekta Jamila na vijana wake,
walivamia wakiwa katika mstari mmoja bastola
zikilenga mbele, tayari kwa kutumika, naam
wakafika katika sebule lakini wasiyaamini macho
yao! Wote walipigwa na mzubao wa mwaka, huku
wakiongeza umakini mara dufu, walipiga goti,
wakawa wanageuka kila upande tayari kwa
mashambulizi, lakini bado ulikuwa kama kucheza
na kivuli chake mtu, huwa hakina madhara yoyote!
Inspekta Jamila huku akiwa ametaharuki kwa hali
anayoishuhudia, alitowa ishara ya kusachi
vyumbani, katika nyumba ile iliyokuwa mpya
kabisa, ikiwa haina samani nyingi ndani yake, pia
kulikuwa bado milango ya vyumbani, ilikuwa
haijawekwa katika nyumba ile! Hivyo haikuwa
shida kufika vyumbani, lakini hadi kinafikiwa
chumba cha nne na cha mwisho katika nyumba ile,
hakukuwa na majibu yaliyopatikana, yaliyotofautian
a na ya vyumba vingine, vilikuwa hakuna
mwanaadamu aliekuwa katika vyumba vile, sasa
wakiwa wameshusha silaha zao chini, wote
walijongea pale sebuleni, wakiwa bado hawaamini
kitu wanachokiona kwa macho yao!
Mwakyembe Anthony, alikuwa amelala chali macho
yamemtoka pima yakiwa hayaoni yanachotazama!
Mwili wake ukiwa na matundu ya risasi usawa wa
moyo wake, damu nyingi zilikuwa zimetapakaa
sebuleni pale,na zilianza kuganda kuonesha kiasi
ya kama dakika kumi na tano hivi, ndiyo roho
imeacha mwili wa Mwakyembe Anthony, Lakini
Jeradi Mwaipopo, akiwa hajulikani alipo wala
hakuwamo katika nyumba ile! simu ya marehemu
Mwakyembe, aina ya Blackbery, ilikuwa ipo juu ya
stuli ikiwa ipo on! Inspekta Jamila alitikisa kichwa
kwa masikitiko, safari hii akimkosa Jeradi
Mwaipopo,au JM kwa dakika chache sana!
*******
Jeradi Mwaipopo, alikuwa anajinyoosha viungo
vyake,Mwakyembe alitowa simu yake pamoja na
simu za wale askari,akawa anazithaminisha, ndipo
JM alipoiona ile simu ya Blackbery ya Mwakyembe,
na mara moja moyo wake ukapiga paah!
Akakumbuka simu hii ndiyo aliyowasiliana na yule
askari, akipigiwa na yeye kupiga, JM anatambuwa
tangu akiwa askari, madhara ya simu za Blackbery
kwani zinaweza kukuonesha kila ulipo, na yeye
mwenyewe alishawahi kuwakamata wahalifu
waliokuwa wameziiba simu za aina hiyo, kwani
hata kama ungebadilisha laini, lakini bado
ingeweza kusomwa mahala ulipo, akahisi matatizo
mbele yake,yakimjia kwa haraka!
Akamwambia Mwakyembe, una kitu gani cha
kutulinda humu ndani, ikitokezea mahasimu wetu,
wakitujia hapa?! Mwakyembe huku akitabasamu,
alimwambia JM. Ondoa shaka juu ya hilo,hapa
nina Bastola inayobeba risasi kumi na nane, tena
ikiwa imejaa risasi, lakini kama haitoshi jana tu
ndiyo nimepata kiwambo chake cha kuzuia sauti!
Mwakyembe alisema maneno hayo, huku
akikigeuza kiti cha kukaa mtu mmoja, aina ya sofa,
juu chini na kuibua bastola peke yake ikiwa
imevishwa magazini yake, na kiwambo cha kuzuia
sauti kikiwa pembeni yake. Akamkabidhi JM kwa
maana ya kumuonesha! JM aliipokea ile silaha
huku akitabasamu, akakivesha kiwambo cha kuzuia
sauti, akapandisha risasi chemba, akiwa kama
anaeijaribu ile silaha kama inafanya kazi
sawasawa, huku akiwa ameielekeza juu silaha ile,
na risasi ikapanda juu, ikisubiri amri ya kutumwa
iende wapi, naam JM akiwa anatizamana uso kwa
uso na Mwakyembe, aliishusha ile silaha kwa kasi
ikamlenga Mwakyembe, usawa wa moyo, na JM
huku akifumba macho, aliziruhusu risasi mbili,
kutoka katika silaha ile, naam nazo zikajibu kama
zilivyotumwa, zikafumua moyo wa Mwakyembe,
kila moja ikipiga katika moyo na kufumua nyama
kubwa kwa nyuma!Kwa kuwa Mwakyembe alikuwa
karibu kama futi tatu kutoka alipokuwa JM, risasi
zile zilimrusha nyuma kama mita nzima na
kumtupa chali chini kama mzigo alitupa mikono
kidogo akatulia tulii kama maji mtungini, akawa
amebadilishwa jina na kuwa marehemu
Mwakyembe! JM aliibusu ile silaha aliekuwa
anaihitaji kuliko kitu chochote kile kwa wakati ule,
kisha akafunga usalama wa silaha ile automatic,
huku risasi nyingine, ikiwa tayari ipo chemba,
ikisubiri safari! Jm aliziendea zile simu zilizokuwa
zimewekwa katika stuli na marehemu Mwakyembe,
akaichukua simu moja iliyouwa inahadhi na
heshima kidogo, mali halali ya Konstebo Iddy Gebo,
akatowa line iliyokuwemo mle ndani, akatoa line
nyingine ya simu, kutoka katika sehemu ya kuvalia
mkanda kwa nje, aliibinjua suruali yake, na sehemu
iliyokuwa imekatwa, akasogeza kwa vidole vyake,
akatowa line ya kampuni ya simu ya Airtel, na
kuipachika katika simu ile akaiwasha, na simu
ikakubali kuwaka! Baada ya kujiridhisha kuwa
ameshapata simu, silaha kwa ajili ya kujilinda,
akaichukua na ile simu ya yule askari mwingine,
nokia ya toch, akaziweka mfukoni mwa suruwali
yake, mara ile simu aliyoweka line yake, ikatoa
mlio wa betri kukosa chaji ya kutosha, na JM
akaizima kabisa. Akatoka nje akifunga mlango kwa
nje, akaiendea ile pikipiki ya marehemu, akatoka
nayo hadi nje, akalifunga lile geti kwa funguo na
kuondoka na ufunguo wa nyumba na wa geti,
pamoja na ile silaha akatokomea zake, akielekea
Vinguguti kwa fida Hussein!
12.
WADAU WETU, KITABU CHA BARUA KUTOKA JELA
KIPO MITAANI, KUPATA KHATMA YA JM
TAFADHALI PATA NAKALA YAKO SASA ILI
KUMUUNGISHA MWANDISHI. ASANTENI SANA
KWA KUWA SOTE TANGU MWANZO HADI HAPA.