mapengo junior
JF-Expert Member
- Jun 28, 2011
- 1,135
- 276
- Thread starter
- #161
SIMULIZI; BALAA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010
SEHEMU YA SABINI
Masaa matano ndani ya gari yake aina ya Toyota corolla yalitosha kumfikisha mpelelezi mahiri nchini Tanzania, Daniel Mwaseba katika mji mdogo wa kitalii, Kilwa Masoko. Mji ambao kwa sasa ulikuwa umechafuka kwa matukio mauji ya kutisha sana pamoja na upotevu wa maiti katika hospitali ya wilaya ya Kilwa, iliyopo katika mji wa Kilwa Kivinje, kilometa chache tu toka mji wa Kilwa Masoko. Daniel Mwaseba alitafuta hoteli nzuri ya kupumzika kabla hajaanza shughuli, miongoni mwa shughuli ngumu zaidi alizowahi kuzifanya Daniel Mwaseba katika kuitetea Tanzania dhidi ya hila zote za watu wabaya. Hoteli ya kitalii ya Kimbilio nd'o lilikuwa jibu lake. Hoteli iliyokuwa kandokando mwa bahari ya Hindi, katika fukwe nzuri na safi za pwani ya Jimbizi ama JB kama wenyeji wa Kilwa walivyozoea kuziita. Katika hoteli hiyo Daniel Mwaseba alipokelewa kwa ukarimu wa hali ya juu. Kama zilivyo mila na desturi za watu wa Kilwa. Mhudumu wa kike aliyevaa sare za hoteli hiyo, sketi fupi ya bluu isiyofika katika magoti na shati safi jeupe. Mhudumu huyo alimpeleka Daniel Mwaseba katika chumba safi na kikubwa, namba 53 alifanikiwa kusoma namba pale mlangoni wakati akiingia ndani ya chumba hiko, waliingia ndani na yule Mhudumu aliyejitambulisha kwa jina la Irene. Irene alimuelekeza Daniel vitu mbalimbali kuhusu chumba kile kisha akaondoka. Alivyobaki peke yake Daniel Mwaseba akajilaza chali katika kitanda kipana cha kitanda kile. Akiwa amelala pale kitandani maandishi yote yaliyoandikwa na mwandishi asiyejulikana jina katika gazeti la Shupavu yalijirudia katika kichwa chake.
Siku nzima Daniel Mwaseba aliimaliza pale Kimbilio hoteli. Alipata kila alichokihitaji katika hoteli ile.
Jioni alienda katika fukwe nzuri ya jimbiza aliyokuwa anaisikia sifa zake, hakuwahi kufika katika fukwe hiyo ingawa alishawahi kwenda mara kadhaa Kilwa, alipigwa na upepo mwanana wa bahari. Hakuwa na haja ya kwenda kutembea mjini, alikuwa anaujua sana mji wa Kilwa. Alishakuja katika harakati zake nyingi sana za kipelelezi. Alitulia ufukweni hadi giza lilivyoanza na kurudi katika hoteli aliyofikia.
Siku iliyofuata ilikuwa ni siku ya balaa sana katika mji wa Kilwa Masoko. Wanafunzi mia moja wa shule ya Msingi Masoko hawakujulikana walipoenda. Ilikuwa balaa hasa. Mji nzima wa Kilwa ilikuwa ni vilio. Vilio toka kwa wazazi wa watoto waliopotea, vilio toka kwa ndugu wa watoto waliopotea. Jeshi la polisi wilayani Kilwa liliingia tena kazini angalau tu kupata fununu tu kwa kilichotokea kwa watoto hao mia moja wa shule ya Msingi Masoko. Hadi jioni haikupatikana fununu yoyote. Taarifa ilikuwa ileile. Kwamba watoto mia moja hawatolala majumbani mwao usiku ule. Watalala wapi, lilikuwa swali gumu ambalo jeshi la polisi na wazazi wa watoto hao hawakuwa wanaweza kulijibu.
Siku hiyo mbaya ikapita, ikaja siku nyingine mpya. Baada ya siku tatu tangu watoto wapotee katika shule ya Msingi Masoko. Hakukuwa na taarifa yoyote juu ya watoto wale waliopotea. Siku hiyo ya tatu ikaja na jipya, watoto kumi na saba toka katika shule ya Sekondari Kilwa walipotea. Matukio yote hayo yalifikia sikio la Daniel Mwaseba na kumfanya Daniel Mwaseba atabasamu. Tabasamu la kishujaa akijua kwamba kazi aliyokuwa anaipenda zaidi hapa duniani imeanza...
ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA
MWANDISHI; HALFANI SUDY
SIMU; 0757 633010
SEHEMU YA SABINI
Masaa matano ndani ya gari yake aina ya Toyota corolla yalitosha kumfikisha mpelelezi mahiri nchini Tanzania, Daniel Mwaseba katika mji mdogo wa kitalii, Kilwa Masoko. Mji ambao kwa sasa ulikuwa umechafuka kwa matukio mauji ya kutisha sana pamoja na upotevu wa maiti katika hospitali ya wilaya ya Kilwa, iliyopo katika mji wa Kilwa Kivinje, kilometa chache tu toka mji wa Kilwa Masoko. Daniel Mwaseba alitafuta hoteli nzuri ya kupumzika kabla hajaanza shughuli, miongoni mwa shughuli ngumu zaidi alizowahi kuzifanya Daniel Mwaseba katika kuitetea Tanzania dhidi ya hila zote za watu wabaya. Hoteli ya kitalii ya Kimbilio nd'o lilikuwa jibu lake. Hoteli iliyokuwa kandokando mwa bahari ya Hindi, katika fukwe nzuri na safi za pwani ya Jimbizi ama JB kama wenyeji wa Kilwa walivyozoea kuziita. Katika hoteli hiyo Daniel Mwaseba alipokelewa kwa ukarimu wa hali ya juu. Kama zilivyo mila na desturi za watu wa Kilwa. Mhudumu wa kike aliyevaa sare za hoteli hiyo, sketi fupi ya bluu isiyofika katika magoti na shati safi jeupe. Mhudumu huyo alimpeleka Daniel Mwaseba katika chumba safi na kikubwa, namba 53 alifanikiwa kusoma namba pale mlangoni wakati akiingia ndani ya chumba hiko, waliingia ndani na yule Mhudumu aliyejitambulisha kwa jina la Irene. Irene alimuelekeza Daniel vitu mbalimbali kuhusu chumba kile kisha akaondoka. Alivyobaki peke yake Daniel Mwaseba akajilaza chali katika kitanda kipana cha kitanda kile. Akiwa amelala pale kitandani maandishi yote yaliyoandikwa na mwandishi asiyejulikana jina katika gazeti la Shupavu yalijirudia katika kichwa chake.
Siku nzima Daniel Mwaseba aliimaliza pale Kimbilio hoteli. Alipata kila alichokihitaji katika hoteli ile.
Jioni alienda katika fukwe nzuri ya jimbiza aliyokuwa anaisikia sifa zake, hakuwahi kufika katika fukwe hiyo ingawa alishawahi kwenda mara kadhaa Kilwa, alipigwa na upepo mwanana wa bahari. Hakuwa na haja ya kwenda kutembea mjini, alikuwa anaujua sana mji wa Kilwa. Alishakuja katika harakati zake nyingi sana za kipelelezi. Alitulia ufukweni hadi giza lilivyoanza na kurudi katika hoteli aliyofikia.
Siku iliyofuata ilikuwa ni siku ya balaa sana katika mji wa Kilwa Masoko. Wanafunzi mia moja wa shule ya Msingi Masoko hawakujulikana walipoenda. Ilikuwa balaa hasa. Mji nzima wa Kilwa ilikuwa ni vilio. Vilio toka kwa wazazi wa watoto waliopotea, vilio toka kwa ndugu wa watoto waliopotea. Jeshi la polisi wilayani Kilwa liliingia tena kazini angalau tu kupata fununu tu kwa kilichotokea kwa watoto hao mia moja wa shule ya Msingi Masoko. Hadi jioni haikupatikana fununu yoyote. Taarifa ilikuwa ileile. Kwamba watoto mia moja hawatolala majumbani mwao usiku ule. Watalala wapi, lilikuwa swali gumu ambalo jeshi la polisi na wazazi wa watoto hao hawakuwa wanaweza kulijibu.
Siku hiyo mbaya ikapita, ikaja siku nyingine mpya. Baada ya siku tatu tangu watoto wapotee katika shule ya Msingi Masoko. Hakukuwa na taarifa yoyote juu ya watoto wale waliopotea. Siku hiyo ya tatu ikaja na jipya, watoto kumi na saba toka katika shule ya Sekondari Kilwa walipotea. Matukio yote hayo yalifikia sikio la Daniel Mwaseba na kumfanya Daniel Mwaseba atabasamu. Tabasamu la kishujaa akijua kwamba kazi aliyokuwa anaipenda zaidi hapa duniani imeanza...
ITAENDELEA MUNGU AKIPENDA