May our enemy work unknowingly in our favour

Simbamteme

JF-Expert Member
Sep 10, 2011
784
2,063
Katika baa moja nchini Marekani aliingia mwanamme mmoja MZUNGU na kukuta bar ina watu wengi sana na imejaa WAZUNGU TUPU kasoro mmama mmoja ambaye alikuwa BLACK..yule jamaa baada ya kuingia akasema kwa nguvu sana "Bartender,wahudumie vinywaji watu wote katika hii bar kasoro huyu mama Mweusi"..Baada ya watu wote kuhudumiwa,yule BLACK WOMAN akamgeukia yule Mzungu na kumwambia "Thank you" huku akitabasamu

Mzungu kuona vile kwamba yule mama hajachukia kwa kitendo kile akamuita bartender kwa mara nyingine na kusema " Wahudumie wote chupa ya wine pamoja na chakula watu wote kasoro huyu mama mweusi"

Baada ya watu kuhudumiwa na kula,yule mmama akamgeukia yule Mzungu kwa mara nyingine na kumwambia "Thank you" huku akiwa a uso wa furaha

Mzungu kuona vile akajaa upepo..ikabidi aende kaunta akamuuliza Mhudumu mmoja pale,yule mama ni nani na kwa nini hajachukia kwa kitendo chake alichokifanya

Bartender akamjibu jamaa kuwa yule mama ndiye MMILIKI wa ile bar
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom