gilbert35
JF-Expert Member
- Nov 20, 2021
- 247
- 474
- Thread starter
- #101
Riwaya: Anga ya Washenzi
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.
Msimu Wa Nne
Sehemu ya 07&08
Majira ya Saa nane usiku ndani ya nyumba ya Dokta Yusha kulikuwa na kikao kizito. Kikao hiki kilihudhuriwa na watu watano. Wawili wa kike ambao ni Cara na Elizabeth Neville. Huku watatu wa kiume ni Dokta Yusha, Gilbert Mwaitika wakiwa pamoja na Mwanasheria Mlevi.
"Hali halisi ndio hiyo ndugu zangu, mchana nikiwa nazungumza naye aliniambia atanipigia maana kuna jambo ameliona na halielewi hivyo nikakata simu" Gilbert Mwaitika alisema.
"Panapopambazuka asubuhi na mapema inabidi niongozane na Elizabeth Neville katika jengo la Uchumi maana hii waleti imeshatupa jibu juu ya muhusika wa mauaji ya Mawazoo. Alama ya Damu iliyoonekana kwenye kitambulisho inaonekana ni ya Mawazoo. Ahsante Dokta kwa kutusaidia katika utambuzi wa hili. Tanzania inazidi kukua katika teknolojia kila kukicha, kwani miaka ya nyuma ilikuwa ni ngumu kugundua damu ni ya nani hadi uchukue na damu ya mhusika kisha uzipime zote.
"Kingine ni kuhusu yule mtoto wa Henry. Ni ngumu sana kumtoa ile kill plug aliyowekewa katika ubongo wake. Nilichofanya ni kumficha kule chini ya ardhi pasipo na mtandao ili asiweze kuuwawa kirahisi. Hii nyumba kwa kweli Dokta uliitengeneza kiutaaalam sana. Hata mtu akikutafuta katika mtandao kama upo kule chini huwezi patikana katu. Na ndipo tulipomhifadhia pia Festus baada ya kubaini pia anacho kifaa karibu na moyo wake kinachoonyesha ni wapi alipo. Inabidi pia tujitahidi kutafuta namna ya kuondoa kifaa hicho maana nilipokifwatilia kupitia mtandao, taarifa zinaonyesha ni kifaa ambacho kina uwezo pia wa kuondoa uhai wa mtu kama atapandikiziwa katika kiungo chochote kilicho ndani ya mwili kama vile figo, moyo, ini, na kadhalika. Maana huwa kinapasuka. Ili kipasuke kinahitaji muunganiko wa kimtandao kutoka kwa mpandikizaji na kifaa hicho. Kama tungechelewa kujua haya naamini Festus angekuwa ni marehemu sasa hivi." Cara alieleza vizuri na kwa urefu zaidi.
Waliendelea kuzungumza pamoja, lakini Elizabeth Neville alikuwa ni kama vile hayupo pale, hakuwa akielewa kinachozungumziwa pale. Kichwani alikuwa amebeba neno moja tu. Daniel
Ni Asubuhi na mapema ndani ya mji wa Moshi. Jua lilichomoza mapema mno na lilikuwa ni kali pia. Asubuhi hii iliwakuta Mwanasheria Mlevi pamoja na Elizabeth Neville nje ya jengo la Uchumi Plaza. Walizama ndani ya viunga vya uchumi na kuangaza macho huku na kule. Mara wakasikia wakiitwa na mlinzi mmoja.
"Mnahitaji kwenda wapi? Mmewahi sana maana ofisi nyingi huwa zinafunguliwa saa mbili asubuhi, na sasa ndio kwanza saa moja kasoro" Mlinzi alieleza. Alikuwa amebeba bastola yake mkononi, katika mfuko wa shati yake ya sare kulikuwa na nembo ya K4A Security ambayo ni kampuni binafsi ya ulinzi na usalama.
"Tuna shida na Exaud Kimbori. Sisi ni maofisa kutoka jeshi la polisi, vitambulisho vyetu ni hivi. Habari yako Mr." Mwanasheria Mlevi akasema na kutoa salamu.
"Ohoo..! Salama kabisa kamanda. Bila shaka mnamuulizia yule meneja wa hili tawi la NMB bank hapa Uchumi." Mlinzi yule akasema, wakatingisha vichwa vyao kwa pamoja kuafiki ni huyohuyo wanayemuulizia.
"Kama ni yeye basi tangu jana alipotoka hapa majira ya saa sita mchana hajarejea hadi sasa. Labda muwasiliane nae kwa njia ya simu" Mlinzi akasema
"Unaweza kunisaidia kunielekeza anaishi mtaa gani hapa mjini ndugu yangu?" Mwanasheria akasema kwa sauti ya chini kidogo huku akimsogelea kwa karibu zaidi mlinzi yule.
"Si unajua lakini ni mwiko katika kazi?" Mlinzi akadokeza.
"Nalijua hilo ndio maana naomba unisaidie ndugu yangu. Tutalindana hivyohivyo si unajua tena?" Mwanasheria akasema huku akimpatia mkono wake mlinzi yule, na kumbe katika mkono alishika noti moja ya Shilingi Elfu kumi ya kitanzania. Mlinzi yule akatoa maelekezo ni wapi bwana Exaud anaishi, ilikuwa sio mbali sana na pale. Si hivyo tu, na nambari yake ya simu walipewa na mlinzi yule.
Baada ya kutoka pale wakamtafuta Cara kwenye simu na kumpata. Elizabeth ndiye aliyepiga.
"Cara tusaidie jambo moja sasa hivi, Mwanasheria kuna simu anaipiga hivi sasa, tafadhali ifuatilie huyo anayepigiwa yupo wapi kwa wakati huu."
Mwanasheria akapiga nambari ile aliyopatiwa, kwa bahati nzuri ilikuwa ikiita. Iliita hadi ikakata. Akapiga mara ya pili, safari hii ikapokelewa.
"Haloo.. Unazungumza na Joseph Urio, bila shaka ninazungumza na Exaud Kimbori Meneja wa NMB katika tawi dogo lililopo hapa Uchumi Plaza" Mwanasheria alikuwa akiongea.
"Bila shaka ni mimi. Karibu nikusaidie" Sauti ikasikika simuni ikisema. Mwanasheria akatabasamu baada ya kusikia. Akaitazama saa yake ya mkononi na kisha akamtazama Elizabeth Neville. Elizabeth naye hapohapo akamcheki Cara. Baada ya sekunde tano hivi Elizabeth Neville akampa Mwanasheria ishara ya kuendelea kuzungumza kupoteza muda ili Cara afanikiwe kule alipo. Mwanasheria bila kusita akafanya hivyo.
"Kuna swala la kibiashara ningependa kujadiliana nawe, ni kuhusiana na kazi yako pia katika maswala ya kibenki. Tafadhali nijuze ni wakati gani tunaweza kuonana hapa ofisini kwako au sehemu nyingine tuzungumze." Mwanasheria akasema.
"Samahani kwa hilo. Kwa sasa nipo Mkoani Tanga kikazi tangu jana, hivyo naomba nitafute kesho kutwa." Meneja Exaud alisema na kisha simu kukatwa. Mwanasheria alimtazama Elizabeth Neville huku akiduwaa. Elizabeth Neville alikuwa akitabasamu kwa mbali, na kwa mbali alionyesha huzuni pia.
"Cara anasema mnara unasoma PANAMA Hotel. Bila shaka ile anuani aliyotupatia yule mlinzi ilikuwa sahihi. Twende Panama Hotel sasa hivi" akasema Elizabeth Neville, haraka wakageuza gari na kuelekea barabara ya kuelekea soko la vyakula Mbuyuni. Mbele kidogo wakakunja kulia barabara inayowapeleka moja kwa moja Panama Hotel.
Dakika mbili tu mbele walifika mbele ya Jengo la Panama Hotel. Lilikuwa ni jengo la ghorofa nane kwenda juu. Walishuka kwenye gari, wakajitazama kama wapo sawa, wakaingia ndani kuelekea mapokezi.
Pale mapokezi walikutana na Dada mmoja mnene. Baada ya salamu wakagundua dada yule ni mchaga kutokana na lafudhi yake.
"Naam Karibuni sana Panama Hotel" Dada yuke akawakaribisha tena kwa ukarimu.
"Ahsante sana Dada. Sisi ni maofisa wa polisi, kuna mtu wetu yupo hapa hivyo tumekuja kumchukua. Vitambulisho vyetu ni hivi unaweza kuvitazama." Elizabeth Neville akasema huku akimpatia dada yule wa mapokezi kitambulisho chake. Mwanasheria naye akatoa chake na kumwonyesha asome huku akiangaza macho yake kuelekea kwenye ngazi za kupandishia juu.
Dada yule pia akaonyeshwa kitambulisho cha Exaud Kimbori. Macho ya dada huyo yalionyesha ni kweli alikuwa akimfahamu mtu huyo, lakini kabla hajasema kitu ikasikika sauti ya mtu akijikohoza nyuma yao.
"Hey Lady. Natoka, naomba mtu yoyote akija kuniulizia hapa mwambie sijaonekana hapa tangu jana, pia nitaarifu." Mtu yule akasema, na kumbe mtu huyo alikuwa ni Exaud Kimbori.
Naam, hatimaye Exaud Kimbori kajileta kiulaini mbele ya wapelelezi. Nini kitajiri? Watafanikiwa kumkomboa Daniel Mwaseba? Leo Jioni tutafunga ukurasa wa msimu wa nne. Usikose saa kumi na moja jioni hapahapa. Cha kufanya ni like na kukoment pia alika marafiki zako waufollow ukurasa huu.
Msimu wa tano wa Riwaya yetu ya Anga ya Washenzi unapatikana kwa Tshs 700 tu. Lipa kwenda M pesa namba 0765824715 au TigoPesa namba 0678824073 kisha njoo whatsapp kwa namba 0621249611 nikutumie.
Sent from my Infinix X655C using JamiiForums mobile app
Imeandikwa na Gilbert Evarist Mushi
Phone: 0765824715.
Msimu Wa Nne
Sehemu ya 07&08
Majira ya Saa nane usiku ndani ya nyumba ya Dokta Yusha kulikuwa na kikao kizito. Kikao hiki kilihudhuriwa na watu watano. Wawili wa kike ambao ni Cara na Elizabeth Neville. Huku watatu wa kiume ni Dokta Yusha, Gilbert Mwaitika wakiwa pamoja na Mwanasheria Mlevi.
"Hali halisi ndio hiyo ndugu zangu, mchana nikiwa nazungumza naye aliniambia atanipigia maana kuna jambo ameliona na halielewi hivyo nikakata simu" Gilbert Mwaitika alisema.
"Panapopambazuka asubuhi na mapema inabidi niongozane na Elizabeth Neville katika jengo la Uchumi maana hii waleti imeshatupa jibu juu ya muhusika wa mauaji ya Mawazoo. Alama ya Damu iliyoonekana kwenye kitambulisho inaonekana ni ya Mawazoo. Ahsante Dokta kwa kutusaidia katika utambuzi wa hili. Tanzania inazidi kukua katika teknolojia kila kukicha, kwani miaka ya nyuma ilikuwa ni ngumu kugundua damu ni ya nani hadi uchukue na damu ya mhusika kisha uzipime zote.
"Kingine ni kuhusu yule mtoto wa Henry. Ni ngumu sana kumtoa ile kill plug aliyowekewa katika ubongo wake. Nilichofanya ni kumficha kule chini ya ardhi pasipo na mtandao ili asiweze kuuwawa kirahisi. Hii nyumba kwa kweli Dokta uliitengeneza kiutaaalam sana. Hata mtu akikutafuta katika mtandao kama upo kule chini huwezi patikana katu. Na ndipo tulipomhifadhia pia Festus baada ya kubaini pia anacho kifaa karibu na moyo wake kinachoonyesha ni wapi alipo. Inabidi pia tujitahidi kutafuta namna ya kuondoa kifaa hicho maana nilipokifwatilia kupitia mtandao, taarifa zinaonyesha ni kifaa ambacho kina uwezo pia wa kuondoa uhai wa mtu kama atapandikiziwa katika kiungo chochote kilicho ndani ya mwili kama vile figo, moyo, ini, na kadhalika. Maana huwa kinapasuka. Ili kipasuke kinahitaji muunganiko wa kimtandao kutoka kwa mpandikizaji na kifaa hicho. Kama tungechelewa kujua haya naamini Festus angekuwa ni marehemu sasa hivi." Cara alieleza vizuri na kwa urefu zaidi.
Waliendelea kuzungumza pamoja, lakini Elizabeth Neville alikuwa ni kama vile hayupo pale, hakuwa akielewa kinachozungumziwa pale. Kichwani alikuwa amebeba neno moja tu. Daniel
Ni Asubuhi na mapema ndani ya mji wa Moshi. Jua lilichomoza mapema mno na lilikuwa ni kali pia. Asubuhi hii iliwakuta Mwanasheria Mlevi pamoja na Elizabeth Neville nje ya jengo la Uchumi Plaza. Walizama ndani ya viunga vya uchumi na kuangaza macho huku na kule. Mara wakasikia wakiitwa na mlinzi mmoja.
"Mnahitaji kwenda wapi? Mmewahi sana maana ofisi nyingi huwa zinafunguliwa saa mbili asubuhi, na sasa ndio kwanza saa moja kasoro" Mlinzi alieleza. Alikuwa amebeba bastola yake mkononi, katika mfuko wa shati yake ya sare kulikuwa na nembo ya K4A Security ambayo ni kampuni binafsi ya ulinzi na usalama.
"Tuna shida na Exaud Kimbori. Sisi ni maofisa kutoka jeshi la polisi, vitambulisho vyetu ni hivi. Habari yako Mr." Mwanasheria Mlevi akasema na kutoa salamu.
"Ohoo..! Salama kabisa kamanda. Bila shaka mnamuulizia yule meneja wa hili tawi la NMB bank hapa Uchumi." Mlinzi yule akasema, wakatingisha vichwa vyao kwa pamoja kuafiki ni huyohuyo wanayemuulizia.
"Kama ni yeye basi tangu jana alipotoka hapa majira ya saa sita mchana hajarejea hadi sasa. Labda muwasiliane nae kwa njia ya simu" Mlinzi akasema
"Unaweza kunisaidia kunielekeza anaishi mtaa gani hapa mjini ndugu yangu?" Mwanasheria akasema kwa sauti ya chini kidogo huku akimsogelea kwa karibu zaidi mlinzi yule.
"Si unajua lakini ni mwiko katika kazi?" Mlinzi akadokeza.
"Nalijua hilo ndio maana naomba unisaidie ndugu yangu. Tutalindana hivyohivyo si unajua tena?" Mwanasheria akasema huku akimpatia mkono wake mlinzi yule, na kumbe katika mkono alishika noti moja ya Shilingi Elfu kumi ya kitanzania. Mlinzi yule akatoa maelekezo ni wapi bwana Exaud anaishi, ilikuwa sio mbali sana na pale. Si hivyo tu, na nambari yake ya simu walipewa na mlinzi yule.
Baada ya kutoka pale wakamtafuta Cara kwenye simu na kumpata. Elizabeth ndiye aliyepiga.
"Cara tusaidie jambo moja sasa hivi, Mwanasheria kuna simu anaipiga hivi sasa, tafadhali ifuatilie huyo anayepigiwa yupo wapi kwa wakati huu."
Mwanasheria akapiga nambari ile aliyopatiwa, kwa bahati nzuri ilikuwa ikiita. Iliita hadi ikakata. Akapiga mara ya pili, safari hii ikapokelewa.
"Haloo.. Unazungumza na Joseph Urio, bila shaka ninazungumza na Exaud Kimbori Meneja wa NMB katika tawi dogo lililopo hapa Uchumi Plaza" Mwanasheria alikuwa akiongea.
"Bila shaka ni mimi. Karibu nikusaidie" Sauti ikasikika simuni ikisema. Mwanasheria akatabasamu baada ya kusikia. Akaitazama saa yake ya mkononi na kisha akamtazama Elizabeth Neville. Elizabeth naye hapohapo akamcheki Cara. Baada ya sekunde tano hivi Elizabeth Neville akampa Mwanasheria ishara ya kuendelea kuzungumza kupoteza muda ili Cara afanikiwe kule alipo. Mwanasheria bila kusita akafanya hivyo.
"Kuna swala la kibiashara ningependa kujadiliana nawe, ni kuhusiana na kazi yako pia katika maswala ya kibenki. Tafadhali nijuze ni wakati gani tunaweza kuonana hapa ofisini kwako au sehemu nyingine tuzungumze." Mwanasheria akasema.
"Samahani kwa hilo. Kwa sasa nipo Mkoani Tanga kikazi tangu jana, hivyo naomba nitafute kesho kutwa." Meneja Exaud alisema na kisha simu kukatwa. Mwanasheria alimtazama Elizabeth Neville huku akiduwaa. Elizabeth Neville alikuwa akitabasamu kwa mbali, na kwa mbali alionyesha huzuni pia.
"Cara anasema mnara unasoma PANAMA Hotel. Bila shaka ile anuani aliyotupatia yule mlinzi ilikuwa sahihi. Twende Panama Hotel sasa hivi" akasema Elizabeth Neville, haraka wakageuza gari na kuelekea barabara ya kuelekea soko la vyakula Mbuyuni. Mbele kidogo wakakunja kulia barabara inayowapeleka moja kwa moja Panama Hotel.
Dakika mbili tu mbele walifika mbele ya Jengo la Panama Hotel. Lilikuwa ni jengo la ghorofa nane kwenda juu. Walishuka kwenye gari, wakajitazama kama wapo sawa, wakaingia ndani kuelekea mapokezi.
Pale mapokezi walikutana na Dada mmoja mnene. Baada ya salamu wakagundua dada yule ni mchaga kutokana na lafudhi yake.
"Naam Karibuni sana Panama Hotel" Dada yuke akawakaribisha tena kwa ukarimu.
"Ahsante sana Dada. Sisi ni maofisa wa polisi, kuna mtu wetu yupo hapa hivyo tumekuja kumchukua. Vitambulisho vyetu ni hivi unaweza kuvitazama." Elizabeth Neville akasema huku akimpatia dada yule wa mapokezi kitambulisho chake. Mwanasheria naye akatoa chake na kumwonyesha asome huku akiangaza macho yake kuelekea kwenye ngazi za kupandishia juu.
Dada yule pia akaonyeshwa kitambulisho cha Exaud Kimbori. Macho ya dada huyo yalionyesha ni kweli alikuwa akimfahamu mtu huyo, lakini kabla hajasema kitu ikasikika sauti ya mtu akijikohoza nyuma yao.
"Hey Lady. Natoka, naomba mtu yoyote akija kuniulizia hapa mwambie sijaonekana hapa tangu jana, pia nitaarifu." Mtu yule akasema, na kumbe mtu huyo alikuwa ni Exaud Kimbori.
Naam, hatimaye Exaud Kimbori kajileta kiulaini mbele ya wapelelezi. Nini kitajiri? Watafanikiwa kumkomboa Daniel Mwaseba? Leo Jioni tutafunga ukurasa wa msimu wa nne. Usikose saa kumi na moja jioni hapahapa. Cha kufanya ni like na kukoment pia alika marafiki zako waufollow ukurasa huu.
Msimu wa tano wa Riwaya yetu ya Anga ya Washenzi unapatikana kwa Tshs 700 tu. Lipa kwenda M pesa namba 0765824715 au TigoPesa namba 0678824073 kisha njoo whatsapp kwa namba 0621249611 nikutumie.
Sent from my Infinix X655C using JamiiForums mobile app