Wanabodi, nawasalimu kwa jina la JMT.
Ni hivi, mwaka 2015 katika vikao vya ndani ya CCM na hasa NEC vilipitisha majina 5 ya wagombea ambao ni Magufuli, Membe, January, Asha-Rose na Balozi Amina. Uhakika niliona ni kwamba JK alimtaka Membe aliyekuwa adui wa Lowassa ambaye jina lake lilikatwa.
Ghafla JK alipoingia ukumbini akakuta Emmanuel Nchimbi na Sofia Simba wakiongoza watu kuimba, "tuna Imani na Lowassa" kuashiria kutomuunga Membe.
JK alimuuliza ushauri Mkurugenzi wa TISS Othman Rashid kwamba afanye nini baada ya Mkapa kumwambia amkate Membe kwa kuwa amemkata Lowassa.
Jibu la Othman lilikuwa hivi: "Mh wewe ni Mkwere?", 'ndiyo'. Unamjua jongoo mdudu? JK akasema ndiyo. Othman akamuuliza, "umewahi kumkanyaga jongoo?' Jakaya, "yes" anaendelea, "anatoa harufu mbaya sana"
Othman akamwambia, "sasa fumba macho mkamate jongoo kwa mkono wako na umng'ate kwa meno yako, yaani mtoe Membe kwenye 5 Bora lasivyo chama kinakufia mkononi". Ulikuwa ni uamuzi mgumu sana. Membe akakatwa sawia na kijana January na Utamaduni wa kutowaamini wanawake embe dodo likamdondokea Magufuli badala ya Rose na Amina.
Ndugu zangu. Ziko taarifa kutoka kikao Cha Cabinet kilichopita kwamba ripoti ya taarifa za fedha alizotaka SSH za mwezi January to March ziko tayari na amekabidhiwa. Aliyechungulia ripoti hiyo amekuta jina la VP Mpango akiwa alihusika moja kwa mbili katika ufisadi. Kwamba wote watakaonywea kikombe Cha hasira ya mama ni pamoja na "kipenzi" chake, Philip Mpango. Swali: je, mama atafumba macho amng'ate jongoo? Amweke pembeni Makamu wake Mpango aliyemsifia hadharani kwa uadilifu au ataamua kufunika kombe mwanaharamu apite?
Ripoti hii ni kipimo Cha uadilifu na maamuzi magumu kwa mama Samia. Tusubiri.
#FreedomIsBack
Ni hivi, mwaka 2015 katika vikao vya ndani ya CCM na hasa NEC vilipitisha majina 5 ya wagombea ambao ni Magufuli, Membe, January, Asha-Rose na Balozi Amina. Uhakika niliona ni kwamba JK alimtaka Membe aliyekuwa adui wa Lowassa ambaye jina lake lilikatwa.
Ghafla JK alipoingia ukumbini akakuta Emmanuel Nchimbi na Sofia Simba wakiongoza watu kuimba, "tuna Imani na Lowassa" kuashiria kutomuunga Membe.
JK alimuuliza ushauri Mkurugenzi wa TISS Othman Rashid kwamba afanye nini baada ya Mkapa kumwambia amkate Membe kwa kuwa amemkata Lowassa.
Jibu la Othman lilikuwa hivi: "Mh wewe ni Mkwere?", 'ndiyo'. Unamjua jongoo mdudu? JK akasema ndiyo. Othman akamuuliza, "umewahi kumkanyaga jongoo?' Jakaya, "yes" anaendelea, "anatoa harufu mbaya sana"
Othman akamwambia, "sasa fumba macho mkamate jongoo kwa mkono wako na umng'ate kwa meno yako, yaani mtoe Membe kwenye 5 Bora lasivyo chama kinakufia mkononi". Ulikuwa ni uamuzi mgumu sana. Membe akakatwa sawia na kijana January na Utamaduni wa kutowaamini wanawake embe dodo likamdondokea Magufuli badala ya Rose na Amina.
Ndugu zangu. Ziko taarifa kutoka kikao Cha Cabinet kilichopita kwamba ripoti ya taarifa za fedha alizotaka SSH za mwezi January to March ziko tayari na amekabidhiwa. Aliyechungulia ripoti hiyo amekuta jina la VP Mpango akiwa alihusika moja kwa mbili katika ufisadi. Kwamba wote watakaonywea kikombe Cha hasira ya mama ni pamoja na "kipenzi" chake, Philip Mpango. Swali: je, mama atafumba macho amng'ate jongoo? Amweke pembeni Makamu wake Mpango aliyemsifia hadharani kwa uadilifu au ataamua kufunika kombe mwanaharamu apite?
Ripoti hii ni kipimo Cha uadilifu na maamuzi magumu kwa mama Samia. Tusubiri.
#FreedomIsBack