Ripoti ya "ajabu" ya NAPE huko Houston...!

Ni ajabu na inashangaza..,

Katika ziara ya Nape inayoendelea hivi sasa nchini marekani kumekuwa na matukio mbalimbali ambayo katika zama za sasa na upepo wa kisiasa ulivyo hasa ndani ya CCM ni sawa kuyaita matukio hayo kuwa ni ajabu na yasiyotegemewa hasa kwa mtu kama Nape kulingana na umri wake na hata nafasi yake. Miongoni mwa matukio hayo nitayataja baadhi, ambayo Nape ameonyesha uwezo mkubwa wa kisiasa na uelewa wa siasa za kimataifa na mahusiano ya kidplomasia, pale alipofanikiwa kwa mara moja kumaliza mgogoro ambao ulidumu kwa muda mrefu baina ya watanzania waliopo jimbo la texas jijini houston, mgogoro ambao ulishindwa kumalizika hata pale ambapo Rais alifanya ziara nchini humo hivi karibuni. Uwezo huu wa Nape kumaliza mgogoro mkubwa na tata kwa watanzania hao kwa muda mchache umeonekana ni wa ajabu kwani wengi walishindwa hapo kabla,alinukuliwa mmoja wa watanzania waishio jijini humo anayejulikana kwa jina la bwana Kittoga.......


Kwa hiyo unatutangazia kuwa Raisi Kikwete ana uwezo mdogo wa siasa za kimataifa, mahusiano na diplomasia kwa kushindwa kutatua mgogoro huo wa Houson?. Ina maana Nape ni za di ya Kikwete? Hayo siyo matusi ya rejareja kwa mwenyekiti wenu?

Kwanza elewa kuwa mgogoro huo wa Houston siyo wa kimataifa na wala hahuhitaji diplomacy katika kutatua.
 
inasikitisha!
Kama watanzania hao waliridhika na majibu ya nape, huku wakijua waziwazi hali halisi ya mtanzania wa kawaida, basi nashawishika kuzua shaka juu ya uzalendo wao, na huenda walifika tanzania zamani mno!

du kijana anajitahidi mwache na yeye atanue kwani silva head akija sijui atajificha wapi
 
Ni ajabu na inashangaza..,

Katika ziara ya Nape inayoendelea hivi sasa nchini marekani kumekuwa na matukio mbalimbali ambayo katika zama za sasa na upepo wa kisiasa ulivyo hasa ndani ya CCM ni sawa kuyaita matukio hayo kuwa ni ajabu na yasiyotegemewa hasa kwa mtu kama Nape kulingana na umri wake na hata nafasi yake. Miongoni mwa matukio hayo nitayataja baadhi, ambayo Nape ameonyesha uwezo mkubwa wa kisiasa na uelewa wa siasa za kimataifa na mahusiano ya kidplomasia, pale alipofanikiwa kwa mara moja kumaliza mgogoro ambao ulidumu kwa muda mrefu baina ya watanzania waliopo jimbo la texas jijini houston, mgogoro ambao ulishindwa kumalizika hata pale ambapo Rais alifanya ziara nchini humo hivi karibuni. Uwezo huu wa Nape kumaliza mgogoro mkubwa na tata kwa watanzania hao kwa muda mchache umeonekana ni wa ajabu kwani wengi walishindwa hapo kabla,alinukuliwa mmoja wa watanzania waishio jijini humo anayejulikana kwa jina la bwana Kittoga.

Nape pia alisisitiza kwa watanzania wa houston hasa wanaCCM kuwa lazima chama kisogezwe kwa wanachama kiutendaji na kimaamuzi na kusisitiza kuwa hilo ni agizo la Halmashauri kuu ya Taifa ya CCM. Hivyo kuwataka wafungue matawi zaidi ili kuwafikia wengi zaidi kwa ukaribu na urahisi zaidi wa kufuatilia na kushughulikia shughuli za chama.

Lakini jambo lingine ambalo pia liliwashangaza wengi ni upeo binafsi wa Nape pale ilipofika wasaa wa maswali ya papo kwa hapo.,ambapo Nape alitumia muda mwingi wa mkutano wake katika hili ambapo watanzania hao wa houston walipata kuuliza juu ya hali halisi ya uchumi na maisha ya watanzania, ndipo Nape alipowaeleza kwa undani juu ya changamoto zinazoikabili serikali ya awamu ya nne na chama kama taasisi inayoisimamia serikali na pia kuelezea mafanikio yaliyopatikana chini ya CCM, kwa namna ya kipekee kabisa ya ufafanuzi na tafsiri sahihi ya matukio yanayoendelea Tanzania.

Na ilipofika wakati wa kuelezea juu ya falsafa ya chama inayotawala vichwa vya wengi nae Nape aliitolea maelezo, kuwa ni dhana iliyopotoswa sana kitafsiri hasa na wapinzani lakini aliwahakikishia kuwa hiyo ni falsafa ya mabadiliko makubwa katika chama yenye kulenga kubadili taswira mbaya ya chama na kukipa chama nguvu mpya kiutendaji na maamuzi na pia umaarufu zaidi na kukubalika hasa kwa vijana.

Alisisitiza kuwa "falsafa ya kujivua gamba na vita vya ufisadi ndani ya Tanzania ni vitu vinavyoenda sambamba,kwani zote vita dhidi ya matumizi mabaya ya rasilimali za nchi"

Aidha alimalizia kwa kuwataka Wana CCM kutumia matawi yao ya Chama kuwaunganisha Watanzania badala a kugeuka vijiwe vya majungu na kubaguana kwa vigezo vyovyote vile, huku akiwataka kuweka Utanzania wao kwanza kuliko itikadi na tofauti zao malimbali.

Nape anaendelea na ziara yake nchini Marekani yenye lengo la kukagua uhai wa chama, ambapo atatembelea Columbus-Ohio, New York na atamalizia Washington Dc, kabla ya kurejea nchini Tanzania wiki ya kwanza ya mwezi Novemba.

Chakula cha mabata (pumba)...
 
Ni ajabu na inashangaza..,

Katika ziara ya Nape inayoendelea hivi sasa nchini marekani kumekuwa na matukio mbalimbali ambayo katika zama za sasa na upepo wa kisiasa ulivyo hasa ndani ya CCM ni sawa kuyaita matukio hayo kuwa ni ajabu na yasiyotegemewa hasa kwa mtu kama Nape kulingana na umri wake na hata nafasi yake. Miongoni mwa matukio hayo nitayataja baadhi, ambayo Nape ameonyesha uwezo mkubwa wa kisiasa na uelewa wa siasa za kimataifa na mahusiano ya kidplomasia, pale alipofanikiwa kwa mara moja kumaliza mgogoro ambao ulidumu kwa muda mrefu baina ya watanzania waliopo jimbo la texas jijini houston, mgogoro ambao ulishindwa kumalizika hata pale ambapo Rais alifanya ziara nchini humo hivi karibuni. Uwezo huu wa Nape kumaliza mgogoro mkubwa na tata kwa watanzania hao kwa muda mchache umeonekana ni wa ajabu kwani wengi walishindwa hapo kabla,alinukuliwa mmoja wa watanzania waishio jijini humo anayejulikana kwa jina la bwana Kittoga.

Nape pia alisisitiza kwa watanzania wa houston hasa wanaCCM kuwa lazima chama kisogezwe kwa wanachama kiutendaji na kimaamuzi na kusisitiza kuwa hilo ni agizo la Halmashauri kuu ya Taifa ya CCM. Hivyo kuwataka wafungue matawi zaidi ili kuwafikia wengi zaidi kwa ukaribu na urahisi zaidi wa kufuatilia na kushughulikia shughuli za chama.

Lakini jambo lingine ambalo pia liliwashangaza wengi ni upeo binafsi wa Nape pale ilipofika wasaa wa maswali ya papo kwa hapo.,ambapo Nape alitumia muda mwingi wa mkutano wake katika hili ambapo watanzania hao wa houston walipata kuuliza juu ya hali halisi ya uchumi na maisha ya watanzania, ndipo Nape alipowaeleza kwa undani juu ya changamoto zinazoikabili serikali ya awamu ya nne na chama kama taasisi inayoisimamia serikali na pia kuelezea mafanikio yaliyopatikana chini ya CCM, kwa namna ya kipekee kabisa ya ufafanuzi na tafsiri sahihi ya matukio yanayoendelea Tanzania.

Na ilipofika wakati wa kuelezea juu ya falsafa ya chama inayotawala vichwa vya wengi nae Nape aliitolea maelezo, kuwa ni dhana iliyopotoswa sana kitafsiri hasa na wapinzani lakini aliwahakikishia kuwa hiyo ni falsafa ya mabadiliko makubwa katika chama yenye kulenga kubadili taswira mbaya ya chama na kukipa chama nguvu mpya kiutendaji na maamuzi na pia umaarufu zaidi na kukubalika hasa kwa vijana.

Alisisitiza kuwa "falsafa ya kujivua gamba na vita vya ufisadi ndani ya Tanzania ni vitu vinavyoenda sambamba,kwani zote vita dhidi ya matumizi mabaya ya rasilimali za nchi"

Aidha alimalizia kwa kuwataka Wana CCM kutumia matawi yao ya Chama kuwaunganisha Watanzania badala a kugeuka vijiwe vya majungu na kubaguana kwa vigezo vyovyote vile, huku akiwataka kuweka Utanzania wao kwanza kuliko itikadi na tofauti zao malimbali.

Nape anaendelea na ziara yake nchini Marekani yenye lengo la kukagua uhai wa chama, ambapo atatembelea Columbus-Ohio, New York na atamalizia Washington Dc, kabla ya kurejea nchini Tanzania wiki ya kwanza ya mwezi Novemba.
mbona juzi nape alionekana yupo class.na huko anawadanganya tu mana hawajui jinsi wa2 wanavyoteseka huku hasa vijijini kwa kulinda mafisadi
 
watu wanakosa cha kuandika
mtanzania kwa umaskini wako huku nchi ikiuzwa na kubakiwa mashimo unaandika pumba za kumsifia mtu kasuluhisha mgogoro wa kitoto
hilo lina faida gani kwa tanzania? kiuchumi? kisiasa au kijamii??
kwa akili za mfukoni utabakia kuwa maskini hata wa mawazo.
 
mi naomba akasuruishe Arusha uvccm aone km hawajamtoa nduki, au asuluhishe magamba mzalendo(sita,kyembe na wengine) na magamba ufisadi(mapacha3) hapo nitamuaminia kinoma
 
Kwanini wategemee majibu ya NAPE wakati wao wenyewe wanaweza wakatembelea nchini, au kufanya tafiti ndogo tu za hali ya uchumi na kipato kwa Mtanzania?
Huenda kweli wengi walioko huko ni watoto wa zile familia bora...ambapo matatizo wanafanya kuyasikia kama simulizi katika kitabu cha NGANO ZA KALE.

we mbona unajikoti mwenyewe!?!?!
 
Yeye nape anajua kusuluisha ya nje tu ya ndani yanamshinda basi abaki huko huko aeendelee kuwadanganya hao vilaza wake.
 
Ila mi nampongeza kwa kuonyesha ukomavu wa kidemokrasia kwa kuwapokea vijana wa chadema waliodamana na mabango na kuwakaribisha akisema wametumia hako yao ya kidemokrasia kuonyesha hisia zao na kufikisha ujumbe wao na akawahakikishia ujumbe umefika,lowassa ama jk ama yeyote huko ccm anaweza kuwa na uvumilivu wa kisiasa kama huyu kijana??tuliona hapa yale maandamano ya washington jk alivyoyahujumu kwa kutumia tax payer money!!huyu dogo mi namtabiria kuja kushika nafasi ya juu kabisa hapa nchini,wekeni maneno yangu kama akiba,mwenye kununa anune mwenye kucheka acheke,nape anatusumbua cdm vichwa vyetu!
 
Baada ya CCM kumtuhumu Nape kuisambaratisha zaidi CCM badala ya kuijenga wakaamua wamweke kiporo kwanza kwa kisingizio cha kwenda kuchukua nondoz za uongozi, maana akibaki ni sawa na toto tundu lisilosikia wala kuambilika, wakimshika shati asiende Arusha huyo anatafuta upenyo na kundi lake wanaibukia Mwanza. Mwanza walipomshtukia na kupiga mayowe, hapakuwa na jinsi ila haraka haraka kumpeleka kushikishwa adabu kwa Obama. Huko kalishika kundi dogo la vijana pungufu ya 15 na kujiita anasuluhisha migogoro. Nape mwenyewe ni chanzo cha migogoro atawezaje kuluhisha migogoro aliyoianzisha mwenyewe? Nape ni pandikizi babu kubwa la CCJ ndani ya CCM ndio maana wanazidi kugongana vichwa kila kukicha bila kumtambua mchawi wao. Kiwalacho CCM ki nguoni mwao.
 
Yaani I am so embarassed na nilichokisoma hapa, leo ndio nakubali kwamba huyu mtoto Nape ni empty. kwanza hii hadithi yake ya Houston siielewi maana haina kichwa wala miguu, tunajua amepewa trip kumpooza juu ya manung'uniko yake ya kutoswa katika sakata la kujivua gamba. Sisi wote tulisikitishwa na kudhalilishwa kwake na chama chake lakini sasa inaonyesha kwamba alistahili kutoswa. Maswali ya moja kwa moja kwa ndugu Nape, kwanza je ni kweli kuna mpango wa kukuvua gamba kwa kukunyang'anya cheo cha ukatibu mwenezi kwa kuwa umeonekana umeshidndwa kazi ndio maana leo hii Wassira anafanyakazi zako? Hivi ni wapi umeweka mipaka kati ya kazi za chama chako na zile za serikali yetu ambayo haikuhusu kabisa ki utendaji? Hii ndio tatizo la kutokua na msimamo, hivi hujioni kwamba umegeuzwa kideo na chama cha ko na wewe badala ya kutafuta kurudisha heshima yako na baba yako, unacheza makida makida? Nape chati yaki ilipanda sana baada ya mdahalo, sisi vijana tulianza kuone tumepata mwanaharakati mwanasiasa mwenye msimamo, japo ulipwaya kwa kuonekana dhahiri kushindwa kutetea ufisadi na ushenzi wa chama chako, lakini ulionekana walau unakubali kuwa chama chako kimeshindwa katika mambo mengi, sasa mbona umepoteza muelekeo kabisa na hivyo pia mvuto?
 
Eti mgogoro wa Watanzania Houston! Wabongo kwa kujipa umuhimu, as if anyone gives half a shyt kuhusu mgogoro Houston.
 
hivi nani anaweza kunionyesha ofisi za matawi ya democrats na republicans hapa tanzania?

hahahahahahahhaaaaaaaaa! Sisi waswazi ndio zetu! Eti anaenda kukagua matawi ya chama marekani! Matawi ya magamba houston na texas yatatusaidia nini sie, kama haya tu yaliyopo kwa mtogole na lumumba hayatusaidii kitu?
 
kwa mujibu wa magazeti ya elo tar 02 Nov 2011, CCM inaendesha mkutano usiokuwa wa Kikatiba wa wenyeviti a mikoa, lengo la mkutano huo ni kuizika rasmi hoja ya kujivua gamba. Ndio maan dogo akapelekwa marekani ili awe mbali ni kikao hiki. Huo ndio mwanzo wa kumuondoa hapa nchini kwa kumpatia ubalozi na ili kuizika rasmi agenda ya kujivua gamba.
 
NAPE+NAUYE.jpg


Nimekerwa sana na kitendo cha huyu kijana Nape Nauye ambaye ni katibu wa Itikadi na Uenezi wa chama tawala huko home CCM, nashindwa kuelewa nini hasa kilimleta hapa Marekani? huku akijua fika kuwa maisha ni magumu hapa yeye kwa kuwatumia baadhi ya vibaraka wao wakatupotosha tukadhani huyu dogo anakuja kuongelea maswala ya uchumi na hali ya maisha huko home, just imagine nimetoka Newyork mpaka Huston for nothing! nothing , hakuna la maana aliloongea Nape, yaani kanikera! eti kasema tufungue matawi ya CCM, what is it? .....hey kwani Republican wana matawi Bongo? huyu vipi lakini?
 
Back
Top Bottom