RIPOTI: Gaddafi aliuawa kimakosa

Bujibuji Simba Nyamaume

JF-Expert Member
Feb 4, 2009
74,870
155,833
RIPOTI: ‘GADDAFI ALIUAWA KIMAKOSA’
Raia wa Libya sasa hivi wanaishi maisha ya tabu ukilinganisha na kipindi cha utawala wa Kanali Gaddafi.

LONDON:
Ripoti ya Kamati ya Bunge Uingereza imekosoa hatua ya Uingereza na Ufaransa kuingilia kati na kusaidia kuondolewa madarakani kwa Kanali Muammar Gaddafi nchini Libya mwaka 2011.

Kamati hiyo ya Mambo ya Nje ilisema Uingereza iliongeza chumvi ilipokuwa inaeleza hatari ambazo zingewakumba raia baada ya Serikali ya Gaddafi kuanza kukabiliana na maasi.

Mpango wa kuingia kati kusaidia mwishowe ulitumika kama fursa ya kubadilisha utawala, ripoti hiyo ilisema. Pia, ripoti hiyo inamtuhumu aliyekuwa Waziri Mkuu David Cameron kwa kukosa kuandaa mkakati mahususi kuhusu Libya.

Wabunge hao walisema jambo hilo lilisababisha kutokea kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe, mgogoro wa wahamiaji, ukiukwaji wa haki za kibinamu na kukua kwa kundi la wapiganaji wa Kiislamu wanaojiita Islamic State Afrika Kaskazini.
Msemaji wa Serikali ya Uingereza ametetea Serikali na kusema muungano wa mataifa ya Kiarabu, Arab League, na Umoja wa Mataifa, wote waliunga mkono hatua hiyo ya kijeshi.

Gaddafi aliuawa na waasi 20 Oktoba, 2011 na kuwaacha raia wa nchi yake wakiteseka baada ya kutetereka kwa uchumi wa nchi hiyo hali inayochangia kuongezeka kwa wakimbizi barani Ulaya.

Habari kutoka Libya zilisema kwamba Gaddafi alifariki dunia baada ya kujeruhiwa kichwani na miguuni alipokuwa akijaribu kutoroka kutoka Sirte.

Habari zaidi zilisema kuwa Gaddafi akiwa kwenye msafara mkubwa wa magari alijaribu kutoroka punde baada ya wanamapinduzi wa Libya kuutwaa mji huo.

Baadaye ndege za kivita za Nato ziliufuata msafara huo na kuudondoshea mabomu na Gaddafi alijeruhiwa kichwani na miguuni.

Kuuawa kwa Gaddafi kulithibitishwa na kamanda wa ngazi za juu wa jeshi la wanamapinduzi, Abdel Majid Mlegta kwa kusema ushahidi wa picha na video ulitolewa hadharani. Gaddafi aliiongoza Libya tangu alipompindua Mfalme Idris I, katika mapinduzi yasiyo ya umwagaji damu, wakati huo akiwa na miaka 27

Alipata umaarufu mkubwa kutokana na nguo alizopenda kuvaa, huku akiongozana na walinzi wa kike. Kiongozi huyo wa Libya, pia anadhaniwa kuwa na mbinu nzuri za kisiasa, kwa kuweza kuirejesha Libya kutokana na kutengwa kidiplomasia duniani.

Alipokuwa kijana alivutiwa na kiongozi mzalendo wa Misri, Gamal Abdel Nasser, alipokuwa akishiriki katika maandamano dhidi ya Israel wakati wa mtafaruku wa Suez mwaka 1956.

DONDOO:
Rais wa zamani wa Marekani, Ronald Reagan alimwita Gaddafi ‘mad dog’ yaani ‘mbwa kichaa’.
Kutoka katika Gazeti la Mwananchi la leo ukurasa wa 32 ukielezea habari za Afrika.
 
Gaddafi sasa ndiye mwenye sifa ya kuwa dikteta wa kweli! Alihakikisha wananchi wenzake wa Libya wanaishi maisha mazuri na bora kabisa kuwahi kutokea duniani!

Siyo hawa madikteta uchwara waliotamalaki kwenye bara letu la Afrika na ambao wanajinufaisha wenyewe tu na jamaa zao wa karibu huku kundi kubwa la wananchi wengine wakiishi maisha ya kulialia, kuungaunga na ya kutishwatishwa.
 
Kuna kundi linawapenda sana mabeberu Kuliko wanavyoipenda Nchi yao
Ila mi Sijawahi kumkubali gadafi alikuwa anamsaidia mla nyama za watu Id amin ili tushindwe vita
Lkn kwa uongozi mathubutu wa Nyerere tulimchapa
Gadaff alikuja kutulipa wajanja wakaipiga ile hela, Gadaff katufanyia mengi sana tuwe na shukrani kwa maadui zetu....
 
Kuna kundi linawapenda sana mabeberu Kuliko wanavyoipenda Nchi yao

Ila mi Sijawahi kumkubali gadafi alikuwa anamsaidia mla nyama za watu Id amin ili tushindwe vita
Lkn kwa uongozi mathubutu wa Nyerere tulimchapa
Tulimchapa baada ya mabeberu wa uingereza kumsaidia Nyerere hao hao mabeberu wa uingereza walimsaidia asipinduliwe Nyerere.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
 
Hao jamaa waongo na wanafiki sana. Walikua wanajua fika kwamba Gadafi hakuwa na makosa ila walikusudia kumuua kwa kutoa visingizio vya kuhalalisha uharamia wao wa kupora mafuta ya Libya kama walivyofanya kwa Iraq

Kama kweli wanajutia jinai hiyo na dhulma waliowafanyia Walibya basi hebu waondoke huko na wache kuchota mafuta ambayo wanayapora kwa kuyachimba kiulafi na kuyasafirisha kupitia bandari ya Beghaz
 
Gaddafi sasa ndiye mwenye sifa ya kuwa dikteta wa kweli! Alihakikisha wananchi wenzake wa Libya wanaishi maisha mazuri na bora kabisa kuwahi kutokea duniani!

Siyo hawa madikteta uchwara waliotamalaki kwenye bara letu la Afrika na ambao wanajinufaisha wenyewe tu na jamaa zao wa karibu huku kundi kubwa la wananchi wengine wakiishi maisha ya kulialia, kuungaunga na ya kutishwatishwa.
Late Gaddafi aliendesha nchi kama familia yake japo ilitafsiriwa kama u dictator maana hakuwa na msalia mtume na mtu aliyetaka kumyumbisha wether alikuwa wrong or right, in the same manner ndio ambavyo baba zetu wanasakamwa kuwa na mfumo dume kuwa simba mjengoni ila linapokuja swala la kupenda familia yani mke na watoto kupata mahitaji yao yotr muhimu na kuimarisha nidhamu hawanaga mpinzani.

Huwa naona Libyans were stupid punks, ila ndivyo ilivyo huwa thamani ya wema huonekana mtenda wema akiwa hayupo.

Gadaffi aliitwa dictator na kundi la watu waliokuwa hawamkubali na hawapendi aendelee kutawala Libya kama raisi,mbali na hapo ni watu waliokuwa wanatamnaitafsiri kama chuki binafsi tu...Ila that never hides the fact kwamba the guy was generous.
 
Kifo cha Gaddafi ilikuwa anataka kubadilisha mfumo wa ufanyaji biashara duniani kuachana na dollar na kuanza kutumia dhahabu/ mfumo mwingine kwahiyo Gaddafi aliingilia maslahi ya Marekani. Si unajua us dollars ndio pesa ya kibiashara duniani. Gaddafi asingingilia mfumo wa us dollars angekuwa hai.
RIPOTI:
‘GADDAFI ALIUAWA KIMAKOSA’
Raia wa Libya sasa hivi wanaishi maisha ya tabu ukilinganisha na kipindi cha utawala wa Kanali Gaddafi.
LONDON:
Ripoti ya Kamati ya Bunge Uingereza imekosoa hatua ya Uingereza na Ufaransa kuingilia kati na kusaidia kuondolewa madarakani kwa Kanali Muammar Gaddafi nchini Libya mwaka 2011.
Kamati hiyo ya Mambo ya Nje ilisema Uingereza iliongeza chumvi ilipokuwa inaeleza hatari ambazo zingewakumba raia baada ya Serikali ya Gaddafi kuanza kukabiliana na maasi.
Mpango wa kuingia kati kusaidia mwishowe ulitumika kama fursa ya kubadilisha utawala, ripoti hiyo ilisema. Pia, ripoti hiyo inamtuhumu aliyekuwa Waziri Mkuu David Cameron kwa kukosa kuandaa mkakati mahususi kuhusu Libya.
Wabunge hao walisema jambo hilo lilisababisha kutokea kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe, mgogoro wa wahamiaji, ukiukwaji wa haki za kibinamu na kukua kwa kundi la wapiganaji wa Kiislamu wanaojiita Islamic State Afrika Kaskazini.
Msemaji wa Serikali ya Uingereza ametetea Serikali na kusema muungano wa mataifa ya Kiarabu, Arab League, na Umoja wa Mataifa, wote waliunga mkono hatua hiyo ya kijeshi.
Gaddafi aliuawa na waasi 20 Oktoba, 2011 na kuwaacha raia wa nchi yake wakiteseka baada ya kutetereka kwa uchumi wa nchi hiyo hali inayochangia kuongezeka kwa wakimbizi barani Ulaya.
Habari kutoka Libya zilisema kwamba Gaddafi alifariki dunia baada ya kujeruhiwa kichwani na miguuni alipokuwa akijaribu kutoroka kutoka Sirte.
Habari zaidi zilisema kuwa Gaddafi akiwa kwenye msafara mkubwa wa magari alijaribu kutoroka punde baada ya wanamapinduzi wa Libya kuutwaa mji huo.
Baadaye ndege za kivita za Nato ziliufuata msafara huo na kuudondoshea mabomu na Gaddafi alijeruhiwa kichwani na miguuni.
Kuuawa kwa Gaddafi kulithibitishwa na kamanda wa ngazi za juu wa jeshi la wanamapinduzi, Abdel Majid Mlegta kwa kusema ushahidi wa picha na video ulitolewa hadharani.
Gaddafi aliiongoza Libya tangu alipompindua Mfalme Idris I, katika mapinduzi yasiyo ya umwagaji damu, wakati huo akiwa na miaka 27.
Alipata umaarufu mkubwa kutokana na nguo alizopenda kuvaa, huku akiongozana na walinzi wa kike.
Kiongozi huyo wa Libya, pia anadhaniwa kuwa na mbinu nzuri za kisiasa, kwa kuweza kuirejesha Libya kutokana na kutengwa kidiplomasia duniani.
Alipokuwa kijana alivutiwa na kiongozi mzalendo wa Misri, Gamal Abdel Nasser, alipokuwa akishiriki katika maandamano dhidi ya Israel wakati wa mtafaruku wa Suez mwaka 1956.
DONDOO:
Rais wa zamani wa Marekani, Ronald Reagan alimwita Gaddafi ‘mad dog’ yaani ‘mbwa kichaa’.
Kutoka katika Gazeti la Mwananchi la leo ukurasa wa 32 ukielezea habari za Afrika.
 
Back
Top Bottom