BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,789
- 288,013
Mwenyezi Mungu angekupa uhai zaidi basi ungegundua kwamba nchi yetu si maskini kabisa tuna utajiri mkubwa sana wa rasilimali ambazo kama zingetumika vizuri nchi yetu ingekuwa mbali sana kimaendeleo. Na pia baada ya kusikia na kufahamu ufisadi mkubwa uliofanywa na Viongozi mbali mbali toka CCM basi ungebadili kauli yako na kusema Kiongozi bora wa Tanzania ni lazima atoke nje ya CCM maana hao wote waliotoka CCM wameendeleza ufisadi mkubwa na kuongeza kwa kiwango kikubwa gharama za maisha ya ya kila siku kwa Watanzania. Mwenyezi Mungu ailaze roho yako mahali pema peponi~AMEN.
Last edited by a moderator: