Ridhiwani Kikwete Kujenga Kiwanda Cha "Tiles" Chalinze

Home shopping Centre
Mimi nitafurahi sana kuona Mtanzania mwenzangu akiwekeza zaidi ya investor kutoka nje.

Lakini initia mashaka kuona pale mwekezaji anapokuwa anajificha ficha.

Kwa mfano, Twyford Ceramics hawajaweka wazi mwekezaji ni nani!
 
Twyford bathrooms ni kampuni maarufu sana ya iliyopo UK na ipo chini ya Geberit Group ya Europe.

Twyford ceramics Ltd ya hapa Tanzania bidhaa zao sasa hivi wana import kutoka China. Sidhani kama kuna huusiano wowote na Twyford ya UK ambayo walishakana bidhaa zao hazitoki China.

Wakurupukaji wengi humu.

Twyford ni generic tile makers wa uchina. Unahitaji kupita kkoo nusu saa tu kulijua hilo. Ni mwendelezo wa generic tile makers kama goodone etc. Ofcourse ni vikampuni vidogo visivyo na majina duniani na hata huko uchina vinakotoka.

Kutokana na hilo target yao kuu ni vinchi vyetu vidogo visivyo na purchasing power ya kununua expensive tiles and ceramics. Kutokana na soko kukua ni vema wao kufanya uzalishaji nchini. Kumbuka tiles nzito na volumetric.

Mtoa pesa sio ridhiwani,yeye ni muwezeshaji kama wanunge wote walivyo.
 
Wakurupukaji wengi humu.

Twyford ni generic tile makers wa uchina. Unahitaji kupita kkoo nusu saa tu kulijua hilo. Ni mwendelezo wa generic tile makers kama goodone etc. Ofcourse ni vikampuni vidogo visivyo na majina duniani na hata huko uchina vinakotoka.

Kutokana na hilo target yao kuu ni vinchi vyetu vidogo visivyo na purchasing power ya kununua expensive tiles and ceramics. Kutokana na soko kukua ni vema wao kufanya uzalishaji nchini. Kumbuka tiles nzito na volumetric.

Mtoa pesa sio ridhiwani,yeye ni muwezeshaji kama wanunge wote walivyo.
Hata hivyo good move. .
 
usimamizi makini unatakiwa tusije kuwa na vigae fake,yale ya ARV lilikuwa somo tosha
 
Kazi ya ubongo ni kufikiri,kupokea taarifa,na kutekeleza jambo kutokana na mawazo yaliyoujaza moyo.Mfano joka kubwa likiingia ndani ya nyoka hapohapo mwingine ataruka kujiokoa lakini fikiria mtu aishiye na kuchezea nyoka hatahangaika nini kumbe ni nyoka atasema hivyo.Kwa watanzania waliobaki kulalamika njaa mafisadi ,wakati vijana wengine wanalia njaa wengine wanaona fursa za kujenga Tanzania yenye viwanda.Hongera kwa mawazo chanya Rizone acha wanaolia njaa ukame,hata mvua ikinyesha kwenye maeneo yao hawataona fursa wataona matope na usumbufu.
 
Mbunge wa Jimbo la Chalinze Ridhiwani Kikwete ameanza harakati za kujenga kiwanda cha 'Tiles' katika jimbo lake ambacho kinaweza kuja kutoa ajira kwa watu zaidi ya elfu sita nchini.

Ridhiwan Kikwete amesema kazi yake ni kutafsiri malengo mema aliyonayo Rais John Pombe Magufuli ya kujenga Tanzania ya viwanda kwa vitendo na kudai lengo kubwa la kujenga kiwanda hicho ni pamoja na kutoa ajira kwa vijana na wakina mama.

"Kitakapokamilika Kiwanda cha Tiles Twyford- Chalinze kinataraji kuajiri wafanyakazi rasmi 2000+ na Wasio Rasmi 4000+ na hii kazi ninayofanya ni kutafsiri malengo mema aliyonayo Rais na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi kwa vitendo. Malengo makubwa ni kutoa ajira kwa vijana na wakina mama. Mungu anatusimamia tutafikia malengo tuliyojipangia" alisema Ridhiwan Kikwete.

Mbali na hilo Mh Ridhiwan Kikwete amedai kiwanda hicho kikikamilika malighafi zake za uendeshaji wa kiwanda hicho zitakuwa zikitoka Iringa, Kilimanjaro, Vikindu, Pugu, Morogoro na Tanga na kusema zaidi ya asilimia 90 ya malighafi zitakuwa zikitoka hapa hapa Tanzania.

"Malighafi Zitatoka Iringa, Kilimanjaro, Vikindu,Pugu, Morogoro, na Tanga. Yaani 90 percent inatoka Tanzania. kwa sasa akili, mwili na nguvu iko Chalinze. Inatakiwa nianze na Chalinze ndiyo nitabadili Tanzania kwa watu kuiga mfano wangu" alisisitiza Mh. Ridhiwan Kikwete

Source:Eatv News

Uongo mtupu na propaganda..... kiwanda ni cha wachina CCM hamna jeuri ya kujenga kiwanda chenu kama hata SUKITA ya kusaga unga iliwashinda
 
Hongera kwa mwekezaji!

Dola milioni 56 sio mchezo!
Kila Mbunge akiacha siasa na kufikiria na kufanya maendeleo, hivyo kila jimbo likawa na kiwanda, tutakuwa na viwanda vingapi baada ya miaka 6. Halafu 2020 tukarudi kwenye siasa
 
Back
Top Bottom