Stephano Mgendanyi
JF-Expert Member
- May 16, 2020
- 1,900
- 944
RIDHIWAN KIKWETE AENDELEA KUKAGUA MIRADI YA MAENDELEO CHALINZE.
Chalinze, Pwani.
Mbunge wa Chalinze ndugu Ridhiwanii Kikwete ameendelea na ziara yake ya Kijiji Kwa Kijiji katika jimbo la Chalinze Kwa lengo la kuhamasisha wananchi kushiriki kwenye shughuli za maendeleo pamoja na kukagua miradi mbalimbali inayotekelezwa na serikali, wananchi na ofisi ya Mbunge katika ngazi za vijiji.
Ndugu Ridhiwani amebainisha ya kuwa “Maendeleo ya maeneo yetu yanategemea utayari na utashi wetu, sisi ndio wanufaika wa kwanza wa kila jambo na kila Mradi hivyo ushiriki wetu Kwenye miradi hii utaongeza chachu na kutoa hamasa Kwa serikali kuona kuwa sisi wananchi tuko tayari kushirikiana Kwa pamoja Kwa ajili ya Maendeleo”
“Maendeleo hayana itikadi, hayabagui ila matunda yake ni manufaa ya jamii yetu sote na vizazi vyetu hivyo ni wajibu wetu kuhakikisha tunajenga Chalinze ambayo tunatamani kuiona Miaka michache ijayo na jambo hili linawezekana tukiamua kutokea kwenye kaya zetu, vijiji vyetu, kata zetu hadi ngazi ya jimbo”....... Ridhiwani Kikwete
Ziara ya ndugu Ridhiwani katika Kijiji cha Mnindi kimekuwa ni chachu ya ujenzi wa Chalinze yenye Umoja Kwa kuunganisha wananchi na kuwajengea morali ya kushiriki Kwenye shughuli za maendeleo.
#SamiaNaTanzania
#RizNaChalinze
#KaziIendelee2030