Richmond kutikisa Bunge

hapa ni jk na lowasa,sasa naona lowasa anataka kumwaga mboga. Dah natamani makinda aipitishe hiyo hoja,na hapo rostam lazima ajitokeze wazi.
 
Hoja ya Richmond imeendelea kuzua mjadala katika Serikali na Bunge. Hoja ya kutaka mjadala huo kufunguliwa imetawala katika vikao vya kamati ya wabunge wa chama hicho pamoja na kamati ya uongozi wa bunge. Kila upande kati ya makundi mawili lile la makamanda wa ufisadi na la watuhumiwa wa ufisadi inazungumzia hoja hiyo huku Spika wa Bunge akikwepa katika mkutano wake na waandishi wa habari jana kuzungumzia kwa undani suala hilo. Hoja hii pamoja na suala la nyongeza ya posho, kurejeshwa kwa sheria ya mabadiliko ya katiba na utekelezaji wa maazimio ya bunge juu ya wizara ya nishati na madini zinatarajiwa kuleta mijadala mikali katika mkutano wa bunge unaoendelea.

PM

Hii sheria umri wake tokea Raisi atie saini hauzidi miezi miwili, tayari wabunge walishatumia pesa nyingi kuanzia kwenye kamati, kuchukua maoni ya wadau na mjadala wa Bunge zima; hivi kweli watakapokaa tena kujadili sheria hili watalipwa tena hizo 200,000 wakati kama wasingeingiza ushabiki wa vyama wangekuja na sheria inayotekelezeka bila marekebisho? Mimi nahisi tunaibiwa
......Enyi Wabunge kama kweli mnaipenda nchi yenu msipokee posho kwa ajili ya kupitia sheria hii ya marekebisho ya katiba. Mkandarasi akikosea kwenye kazi yake mkatabata unamwajibisha kurudia kazi yake, nyie mmepitisha sheria imeshindikana kuitekeleza kweli mlipwe tena kuirekebisha?
 
Hii ni kali ngoja tuone mwisho hivi aka ka mama akataki mkuu ambaye hakukutana barabaran na Lowasa aumbuke?
 
lowassa anatapa tapa tu,hii kitu haitamsaidia kama anavyodhani..sana sana atazidi kujivua nguo na makyembe anaonekana kuwa fiti sasa maana lengo lilikua asiwepo hoja itakaporudi bungeni!
Mbona kule Dodoma kwenye kikao cha NEC Lowassa aliumwaga ukweli na JK akawa anatikisa kichwa ikiwa ni ishara ya kukubali? Ok, je ni kwanini JK alishindwa/kashindwa kumjibu Captain Lowassa?
 
Nijuavyo mimi hakuna mtu ndani ya CCM mwenye uwezo wa kupambana na Captain wa jeshi, Lowassa.Time will tell.
 
Iyo ni politics strategy ya chadema,kwa vyovyote ccm ikiloba impitishe MAMVI 2015 ikulu ni kiulaiiiini.aftrow MAMVI ataanika na kuanikwa pia,bora aepushie mbali coz HATA HUYU ALOINGIZWA KTK USPIKA KWA NIABA YA 'KUIMBA' anam2mia
 
Nimepitia mtandao wa mbunge wa Ubungo JOHN MNYIKA na kukuta ameweka hadharani hoja yake binafsi kuhusu Richmond. Katika mtandao huo ameeleza kuwa Hoja hiyo ikipewa nafasi ya kuwasilishwa na kujadiliwa itaongeza msukumo wa utekelezaji wa maazimio ya bunge na hivyo kuchangia katika mapitio ya mikataba yenye kuongeza bei ya umeme; kuweka mfumo wa kulihusisha bunge katika maandalizi ya mikataba yenye maslahi ya taifa ikiwemo katika mafuta, gesi asilia na ujenzi na kuwezesha uwajibikaji na hatua kamili kuchukuliwa kwa waliohusika na ufisadi na uzembe uliolisababishia hasara taifa.
 
mm nalifikiri ndani ya Ukumbi wa Bunge kumbe kwenye twitter, facebook yake mwaga zaidi ameweka wapi?
 
Excellent move Mnyika.
Mkuu Aweda, kuna kitu naona kama sio sawa pengine wadau wanaweza kufafanua. Kama utakumbuka watuhumiwa wa Richmond wamekuwa wanataka sana swala Richmond lirudi tena bungeni lakini juhudi zao hakifuka mahali. Sasa Mnyika ana ajua chochote kuhusu jitihada hizo? Something is not right. Umakini unahitajika maana upo uwezekano watu wakajipenyeza kwenye hii hoja binafsi.
 
Acha irudi maana inaweza isaidie kufungua yale ambayo Mwakyembe alishindwa kuyatoa hadharani na yanahatarisha uhai wake sasa.
 
Acha irudi maana inaweza isaidie kufungua yale ambayo Mwakyembe alishindwa kuyatoa hadharani na yanahatarisha uhai wake sasa.

Yeye si alijifanya anaipenda ccm kuliko uhai wake? Mwache yamkute
 
Mnyika anataka El achafuke tena wakati amekwisha jisafisha makanisani ready kwa uraisi 2015 akitumia njia za mwenzake aliyefanikiwa nae anazitumia hizo mbinu akidhani watanzania bado ni wajinga na hawajifunzi kutokana na makosa
 
Mwakyembe atajilaumu kwa kushindwa kuyaweka yote hadharani sasa yamecost,acha hoja ilirudi mpaka mchawi ajulikane na Watanzania wote.EL alishapasuka kila kitu rais anajua,sasa ndo wakati wake kuweka mambo hadharani ili awasulubu wale wote wanaohusika
 
Suala la Richmond kurudi bungeni, naliona kwa mtazamo tofauti kidogo.

Kwanza imelenga kumsafisha EL, Kwasababu zipo tetesi kuwa toka awali mama Makinda aliposhawishiwa na kundi la EL kugombea uspika, nia ilikuwa ni kumpata mtu atakayeirudisha Richmond bungeni ili sitta , mwakiyembe na kundi lao waonekane walichemsha ktk kulitia taifa hasara, kuleta migogoro isiyoisha ndani ya chama na serikali n.k.

Pili nachelea kusema kuwa Mnyika katumwa!!, ama kwakujua au kwakutokujua. nitaeleza.

Ikiwa katumwa akiwa anajua. Hii huenda ni dhamira ya chama chake (chadema). Kuwa, kimemtuma apeleke hoja hiyo ya Richmond bungeni ili EL asafishwe ili chadema ijihakikishie ushindi 2015 endapo ccm itampitisha El, kwakuwa wamekuwa wakiamini kuwa nguvu ya El kwa Umama ni ndogo ukilinganisha na nguvu ya cdm.

Pia upo uwezekano wa mnyika kutumwa bila ya yeye (mnyika) kujijua kwamba katumwa. El ni mtu anayefanya siasa za kiwango cha juu sana, ana mtandao mpana sana vijana kwa wazee, ndani ya chama chake na ndani ya vyama vya ushindani (upinzani), hivyo ni rahisi hoja hii ya Richmond kufikishwa kwa mnyika kupitia kwa marafiki zake (mnyika) au hata yeye mwenyewe kwa namna moja au nyingine bila Mnyika kulitambua hilo.

Naamini hoja hii ya Richmond kurudishwa bungeni, haikosi mkono wa mafisadi. Naamini hoja hii ilifikishwa kwa Mnyika bila ya yeye kujua, akidhani hoja imeletwa na wazalendo wenzake. Lakini yote kheri coz it is just a political strategy for both political party!!.


Senzota,

Asante kwa maoni yako. Vuta subira hoja hii iingie bungeni. Kwa sasa bado sijawasilisha hoja na maelezo ya hoja. Nilichowasilisha ni taarifa ya hoja tu. Lakini ukitaka kufahamu msimamo wangu kuhusu suala hili unaweza ukarejea tu makala yangu ambayo niliiandika mwaka 2009; miaka kadhaa iliyopita kuhusu suala hili. Nakushauri, uisome mwanzo mpaka mwisho halafu urudi tena kuchangia kama bado maoni yako yatakuwa ni haya haya: JOHN MNYIKA: Richmond, Dowans and Operesheni Safisha Mafisadi

JJ
 
Back
Top Bottom