Tulimumu
JF-Expert Member
- Mar 11, 2013
- 14,395
- 13,272
Siyo kweli soma hapa!
Kampuni ya The Guardian Ltd wapata mkurugenzi mpya.
Mkurugenzi mtendaji wa ITV na Radio One amekabidhi rasmi ofisi ya The Guardian baada ya kupatikana kwa mkurugenzi mpya Bwana Richard Mgamba ambaye atakuwa mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya The Guardian Ltd, kazi ambayo ameianza mara moja.
Wakizungumza mara baada ya mkurugenzi mpya kukabidhiwa ofisi na kuanza kazi mara moja, baadhi ya viongozi wa kampuni ya The Guardian Ltd wamesema kuteuliwa kwa Bwana Richard Mgamba kuwa mkurugenzi mtendaji wa The Guardian itasababisha kampuni hiyo kuendelea kufanya vizuri zaidi kutokana na uwezo mkubwa wa mkurugenzi huyo.
Baadhi ya wafanya kazi wa kampuni ya The Guardian Ltd wamepokea kwa mikono miwili uteuzi wa mkurugenzi Richard Mgamba huku wakisema kuwa kutokana na uwezo mkubwa wa Bwana Richard Mgamba, mabadiliko ya kampuni yao yatakuwa makubwa katika tasnia ya habari hapa nchini.
Uteuzi wa Bwana Mgamba umefanywa na mwenyekiti wa makampuni ya IPP Dakta Reginard Mengi baada ya aliyewahi kuwa mkurugenzi wa kampuni hiyo Bwana Kiondo Mshana kustaafu mwishoni mwa mwaka jana 2014, ambapo mkurugenzi mtendaji wa ITV Radio One Joyce Mhavile alishika nafasi hiyo kwa kipindi cha miezi sita yaani kuanzia mwezi January hadi June 2015 kabla ya kuteuliwa kwa mkurugenzi mpya Richard Mgamba anayeanza kazi rasmi.
Source ITV habari 02/07/2015
Kampuni ya The Guardian Ltd wapata mkurugenzi mpya.
Mkurugenzi mtendaji wa ITV na Radio One amekabidhi rasmi ofisi ya The Guardian baada ya kupatikana kwa mkurugenzi mpya Bwana Richard Mgamba ambaye atakuwa mkurugenzi mtendaji wa kampuni ya The Guardian Ltd, kazi ambayo ameianza mara moja.
Wakizungumza mara baada ya mkurugenzi mpya kukabidhiwa ofisi na kuanza kazi mara moja, baadhi ya viongozi wa kampuni ya The Guardian Ltd wamesema kuteuliwa kwa Bwana Richard Mgamba kuwa mkurugenzi mtendaji wa The Guardian itasababisha kampuni hiyo kuendelea kufanya vizuri zaidi kutokana na uwezo mkubwa wa mkurugenzi huyo.
Baadhi ya wafanya kazi wa kampuni ya The Guardian Ltd wamepokea kwa mikono miwili uteuzi wa mkurugenzi Richard Mgamba huku wakisema kuwa kutokana na uwezo mkubwa wa Bwana Richard Mgamba, mabadiliko ya kampuni yao yatakuwa makubwa katika tasnia ya habari hapa nchini.
Uteuzi wa Bwana Mgamba umefanywa na mwenyekiti wa makampuni ya IPP Dakta Reginard Mengi baada ya aliyewahi kuwa mkurugenzi wa kampuni hiyo Bwana Kiondo Mshana kustaafu mwishoni mwa mwaka jana 2014, ambapo mkurugenzi mtendaji wa ITV Radio One Joyce Mhavile alishika nafasi hiyo kwa kipindi cha miezi sita yaani kuanzia mwezi January hadi June 2015 kabla ya kuteuliwa kwa mkurugenzi mpya Richard Mgamba anayeanza kazi rasmi.
Source ITV habari 02/07/2015