Rev. Peter Msigwa MB.Iringa Mjini

Wa kusoma

JF-Expert Member
Joined
Jul 30, 2011
Posts
3,454
Reaction score
2,984
Naombeni kama kuna mwenye contact za huyu jamaa anipatie kuna jambo nataka nimtume kule Bungeni. Au ngoj niliweke hapa. Kuna mtoto wangu aliitwa kufanya Interview ya TANESCO iringa June mwaka huu.Baada ya ile Interview alitumiwa barua akaambiwa kazi amepata ila asubiri ataitwa, sasa kuanzia mwaka jana huyu kijana hataki kutafuta kazi nyingine anashinda nyumbani akisubiri Tanesco wamwite akafanye kazi Iringa. Nataka Rev. Msigwa aniulizie hili jambo kwa Ngeleja.
 
Hilo haina ulazima wa kupelekwa bungeni!Fahamu bunge haliwezi jadili interest za mtu moja,chakufanya mtafutie mwanao kazi aache ujinga wa kukaa ovyo!!!atasubiri nafasi tanesko mpaka yesu arudi!!!!!!!Nchi inawenyewe!
 
Mtoto wako na wewe mwenyewe mnaonekana akili zenu haziko sawa
 
Mmefatilia TANESCO wakaikana hiyo barua? Au Mnasubili wawafuate? Fatilia kwanza mjue shaida iko wapi?
 
Wewe na huyo mtoto wote_wa kusoma,...mkimaliza masomo mtaacha.
 
Mkuu kweli we hamnazo huyo Msigwa akishamwambia Ngeleja itasaidia nini?Nenda kwa afisa mwajiri wa Tanesco Iringa kamuulize hayo maswali uone majibu yake kwanza dogo wako anaonekana kilaza tu........... na ni changa la macho alikupiga hakuna cha kazi hapo
 
Duuh!
sidhani kama ni kazi ya mbunge kumtafutia mwanao kazi
 
hahaha mwambie mwanao aendelee kukaa nyumbani ale ugali wa bure hadi azeeke
 
Due to the reason beyond our control,It was decided to forfeit those job vacancies,sorry for any inconvenience!

Ipo siku TANESCO watajibu hivyo!
 
wewe kweli kilaza hata hutoi ushahuri kwa mwanao.... sasa baba gani wewe?
watakukameron wewe na mwanao....
 
Huko Iringa naskia mna ardhi nzuri na kubwa ya kulima,nendeni hata ofisi ya kijiji wawape sehemu muanze kilimo kwa maana hata kazi za ofisi hamtaziweza nyinyi make kama hata mbwembe za kutafutia kazi hamzijuhi hiyo kazi pia haiwafai vinginevyo mwendelee kuangalia video na kubadilisha chaneli wewe na mwanao
 
kweli elimu ya uraia inahitajika ili wananchi wajue kazi ya mbunge ni nini kama hali imefikia hapo! ushauri wangu mwambie mwanao asubili hadi umeme wa uhakika upatikane nchini ndio wamuajili.
 
Akipiga cm kule Tanesco anaambiwa asubirie wamezuiwa kuajiri kwa sbb y ISHU YA jAIRO
 

Mkuu huyo mtoto mbona umekula hasara! Ana tabia kama za wayahudi wasioamini kuwa Yesu alishakujaga duniani. Yaani ameamua kungojea huo ujio wa kazi ya Tanesco, mwambie aendelee kusubiri, heri kama angepewa barua ungesema kuna mahali pa mbunge kuanzia, vp kama hiyo simu alopigiwa ni magumashi? Mwambie aamke kichwani, atafute kazi nyingine na kama hiyo ya tanesco naipenda sana, basi wakimuita ataacha hiyo atakayokuwa nayo then aende huko iringa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…