Remembering Precision Air vs Dr. Lwaitama

Remembering Precision Air vs Dr. Lwaitama

Nyati

JF-Expert Member
Joined
Mar 6, 2009
Posts
2,528
Reaction score
1,917
Wakuu nipo mwanza Airport naona Dr. Lwaitama naye yupo hapa na ana ticket ya Precision kuelekea Bukoba, ngoja nitawataarifu kama atapokea maelekezo kwa Kiingereza ama atakataa tena tuwezejua kama dawa ilimwingia vizuri ama la. Tumeisha- "check in" tunasubiri kupanda baada ya saa moja kama MUNGU atapenda nitawataarifu.

Nawasilisha.
 
Huyo mzee mtata sana ..... hafanyi jambo bila kujiuliza mantiki yake.....hiki kichwa sijui tunakitumiaje sasa hivi kama taifa.....
 
Ha ha ha. ..

Lile vagi sijui liliishia wapi?....

Hata mimi sikujua lilivyoisha ila leo ilikuwa shwari



Safiri salama mkuu..

Tumefika salama mkuu

Huyo mzee mtata sana ..... hafanyi jambo bila kujiuliza mantiki yake.....hiki kichwa sijui tunakitumiaje sasa hivi kama taifa.....
Kwa ujumla naona wametoka droo, maelekezo yalikuwa ya lugha zote mbili yaani kiswahili na Kiingereza, wakati binti anatoa maelezo kwa kiswahili Dr. alitikisa kichwa kukubali jambo lililopelekea yule binti kutoa tabasamu. Dr. leo hakuwa na makeke bali alitulia tuli na wale mabinti walikuwa waki treat kwa heshima kubwa. Emergency exit hakukaa abiria yeyote kwani ndege ilikuwa na siti nyingi wazi. Dr. alikaa jirani na mzungu ambaye dk zote kama 25 hivi za safari alikuwa anamfundisha kiswahili, yule binti wa kizungu alisema anafanya kazi FHI. Mimi nilikaa nyuma yao.
Nawasilisha Update
 
Siku zote maelekezo si kwa lugha zote mbili jamani?
 
Wakola waitu mshaija obakise bantu bona gera katoma ishunju ishozi mgana
 
Siku zote maelekezo si kwa lugha zote mbili jamani?

Wanatumia lugha zote mbili ila ikitokea umekaa emergency exit kuna maelezo ya ziada unapewa yanakuwa kwa kithungu yaani atakuja mhudumu kukupa maelezo ya ziada na yanakuwa ya kithungu hata kama waswahili mpo wote, hapo ndio ilikuwa historia ya hilo tifu lake
 
Back
Top Bottom