Rekodi za ukoo za kwako ni zipi?

Pesa ndo itafanya kila mtu akukumbuke....

Ndio pesa na pia ukimsaidia mtu connection akafanikiwa maishani
Hiyo nimeiona sana pia hata kutoa kuwa ref wa mtu

Kweli kwa kweli hata vijijini mtu akifanya sherehe akaita watu wee huyo ni ana pesa then kama kawa
 
baba angu alishika rekodi ya kuja dar wa kwanza na kuwa msomi mkubwa sana hakuna ndugu yake hata mmoja aliyemfikia mpaka leo, labda miaka ijayo. na kweli vikao lazima vilikuwa viwe kwetu.na ilikuwa hivo sababu wadogo zake walikuwa kijijini na waliokuwa mjini ni watoto wa hao wadogo zake kwa hiyo yeye ndio alikuwa mkubwa hapa mjini heshima ilizingatiwa.

Mie kwa uzao wa baba nashika rekodi ya kusoma bado stage moja nimfikie mdingi.ila vikao havifanyiki kwangu kabisa tunafanyia kwa wakubwa wetu.napenda tunavyoheshimiana mdogo lazima uheshim mkubwa hata kama anaishi ki aje
 
mi nataka niweke rekodi ya kuoa demu wa kireno ambaye ndo napiga piga now!!
 
Inachekesha lakini hii kitu ipo sana....

Unakuta kuna mtu anaheshimika mno kwenye ukoo wao...
Ukiuliza unapata majibu very interesting....

Mimi huwa naaita kuweka rekodi kwenye ukoo..lol

utakuta mtu anaheshimika kwa kuwa kwenye ukoo yeye alikuwa

1.wa kwanza kufika daresalaam.
2.kufika chuo kikuu
3.kwenda ulaya...
4kupanda ndege na kadhalika .......

Swali ni hili je wewe mwana jf kwenye ukoo wenu una rekodi gani unashikilia???????????????????lol

msione aibu hebu mje share na sisi hapa???????

Mie nashikilia rekodi zote hizo with exception ya kwenda majuu..ila Dar ndiko nilikozaliwa.
 
Mimi wananiheshimu maana Wa kwanza kuijua JF.


sipati picha huo ukoo wenu lol

inawezekana kila unachoongea wewe hakuna anaebisha
hata ukisema serikali kesho itakuja na sera mpya ya kitu fulani
wanaitikia tu lol
 
ha haa basi hata kumiliki simu ya mkononi waweza kuwa we ulikuwa wa kwanza sio???????

Hahahahaha lol! Boss hapo pia nashikilia rekodi :)...katika ukoo wenu sidhani kama kuna aliyevunja rekodi ya kwenda masafa marefu kufukuzia nanihii hahahahah lol! si unakumbuka ile story ya Mlandizi!? hahahahaha lol! mpaka leo hii kila nikikumbuka huwa nacheka sana lol!
 
Hahahahaha lol! Boss hapo pia nashikilia rekodi :)...katika ukoo wenu sidhani kama kuna aliyevunja rekodi ya kwenda masafa marefu kufukuzia nanihii hahahahah lol! si unakumbuka ile story ya Mlandizi!? hahahahaha lol! mpaka leo hii kila nikikumbuka huwa nacheka sana lol!

ha ha haa
sikufikiria hilo aisee
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Mi nilikuwa wa kwanza kwenye Ukoo wetu kujiunga JF,,,, LOL
 
Mimi nashikilia rekodi ya kufeli darasa la saba, kufeli fom foo, kufeli fom siksi na hatimaye kupata bahati ya kuja ughaibuni (kwa kutumia bank statements za Salamander) na kuwa wa kwanza katika familia kuwa mbeba maboksi.

hahahahahah lol
 
Back
Top Bottom