Pesa ndo itafanya kila mtu akukumbuke....
Huduma utaweza?nataka kuweka ya wake watatu....lol
Inachekesha lakini hii kitu ipo sana....
Unakuta kuna mtu anaheshimika mno kwenye ukoo wao...
Ukiuliza unapata majibu very interesting....
Mimi huwa naaita kuweka rekodi kwenye ukoo..lol
utakuta mtu anaheshimika kwa kuwa kwenye ukoo yeye alikuwa
1.wa kwanza kufika daresalaam.
2.kufika chuo kikuu
3.kwenda ulaya...
4kupanda ndege na kadhalika .......
Swali ni hili je wewe mwana jf kwenye ukoo wenu una rekodi gani unashikilia???????????????????lol
msione aibu hebu mje share na sisi hapa???????
ha haa basi hata kumiliki simu ya mkononi waweza kuwa we ulikuwa wa kwanza sio???????
Hahahahaha lol! Boss hapo pia nashikilia rekodi ...katika ukoo wenu sidhani kama kuna aliyevunja rekodi ya kwenda masafa marefu kufukuzia nanihii hahahahah lol! si unakumbuka ile story ya Mlandizi!? hahahahaha lol! mpaka leo hii kila nikikumbuka huwa nacheka sana lol!
Mimi nashikilia rekodi ya kufeli darasa la saba, kufeli fom foo, kufeli fom siksi na hatimaye kupata bahati ya kuja ughaibuni (kwa kutumia bank statements za Salamander) na kuwa wa kwanza katika familia kuwa mbeba maboksi.