BLACK MOVEMENT
JF-Expert Member
- Mar 11, 2020
- 2,704
- 6,499
Moja ya Changamoto inayo wakabili watu wengi ni suala zima la Mitaji ya kufanyia Biashara, Mitaji ni Kilio cha kila mtu, hasa watu ambao hawana uwezo wa kwensa kukopa Benki na pia hata kama uwezo wa kukopa Benki ungekuwepo ila bado mitaji haitoshi.
Wachina niliwahi soma andiko lao moja kwamba unakuta kampuni moja ina share holder 400 wamegawanyika humo humo kuna Wahasibu, Marketing Officer, IT, Wanashera, Wapishi na kadhalika yaani wamekamilika.
Ulaya kipindi Viwanda tunavyo viona leo hii vya madawa na vyakula na kadhalila ni ya Ushirika walianza, walianza kama ushirika na baadae wakatanua na kufungua Makampuni ambazo ziko hadi leo hii.
Tumeona Wasomali wana Umoja sana, wanachangishana Pesa na kufungua kampuni na kweli kampuni husimama, Waarabu hivyo hivyo, Wahindi hivyo hivyo.
Wakenya pia na Waganda nimeona, Binafisi nina rafiki zangu Wakenya wako Tanzania wanafanya mambo ya IT jamaaa walijichanga wako watatu, wakajichanga na kufungua kampuni ya IT, pia wapo ambao nawajua wamejichanga, ingawa kule kwao hii ni kawaida sana, Waganda pia.
Njoo Sasa kwetu Watanzania, yaani hata ndugu tumbo moja pacha ukiwaeleza swala la kuunganisha nguvu hawakuelewi kabisa, yaani hata Kijana kuunganisha nguvu na Baba yake mzazi au Mama yake mzazi bado haiwezekani. Tumekuwa na sababu nyingi sana kubwa kuliko yote ni UMANIFU hii ndo ngao yetu kuu ya kuto kuunganisha mitaji.Lakini mbona kwenye starehe tunaaminiana sana na kuchangishana?
Ni kawaida Tanzania kukuta ndugu wawili Familia Moja wana Biashara za ku compete, mfano ndugu familia moja wote wana Mabasi na yana compete, Wana maduka yana Compete, na kadhalika, hawa ukiwaambia waunganishe mitaji hawakuelewi kabisa.
Investors wengi wanao kuja Tanzania kama hawajakopa basi unakuta wamejichanga, hata Wazungu, unakuta wa mejichanga wanne au watatu na kufungua kampuni Tanzania.Hatutaweza kushindana na wawekezajinwa nje kama hii vita tutaipigana kila mtu kivyake. Niambie kuna Kampuni ipi ya ujenzi inaweza shindana na zile za Wachina au Wajapani? Ipo? Tuna utitiri wa kampuni za ujenzi ila kamwe hazifikirii kuungana na kuwa na kampuni moja strong ya kushindana.
Sisi unakuta kila mtu anataka afuge kuku angalau 500 wa nyama au mayai, Ila je tutaweza kusindana na wawekezaji wanao kuja Tanzania wanafungua Shamba la kuku na kwa siku wana chinja kuku 100, 000? Wanakusanya trei 5000 za mayai kwa siku? Tutawaweza?Kule Tanga naambiwa kuna mchina anafuga Broiler akupeleka sokoni ni kwanza mzigo wake uishe nyie wengine ndo muanze kuuza na unakuta hapo sisi mtu ana kuku 49 ndo anapeleka sokoni.
Sisi Gradute na pesa zetu za Boom tumejibana tutaweza toboa bi a kuungana?
Tunaweza fanya nini?
Nadhani ifike wakati tuache hizi sababu kwamba hatuaminiani, tutazungukana na kadhalila. Kama ndo hivyo basi tunaweza fanya haya;
- Kuweka mikataba yote kwenye maandishi, n kujenga kiwango cha juu kabisa cha uwazi, ni kweli tunapenda janja janja lakini, tunaweza fanya kitu, tunaweza weka misingi ya juu kabisa ya uwazi, shida pia ni uwazi, uwazi tunakuwa hatuna wa kutosha.
- Tuachane na Tamaaa, hizi ndo chanzo kikuu cha watu kusingizia uaminifu uaminifu kumbe ni tamaa tupu.
- Tuachane na kushindana kutaka kuwafurahisha ndugu, jamaa na marafiki, moja ya sababu ni kwamba kila mmoja anataka aonekane mbele ya jamii kwamba anamiliki biashara ya pekeee yake, ana basi lake, ana Daladala lake mwenyewe, ana duka lake mwenyewe, ana kampuni yake mwenyewe ya ujenzi.
- Tuajiri Managment, kama tunaona shida basi tunaunganusha mitaji na kuweka menejiment na sisi tunakaa pembeni kabisa Managemnet ndo inafanya kazi, hii ni nzuri sana ila ni ni kwa wenye mitaji mikubwa tu. Wenye mitaji wanaweza weka Management na ikawa inafanya kila kitu wao wakawa wanapelekewe report tu.
-Tukae tuwaze competition tunazo pata na pia zijazo, na tukisha ziwaza tuache kuwaza hasi, na tuunganishe mitaji.
Ndugu zangu ukweli ni kwamba hatutaweza compete na wageni kama kila mtu ataenda kivyake vitani, hatutaweza na hii vita hatutashindwa, tutashindwa hii vita, wanakuja Wawekezaji kama Wachina wana mitaji mikunwa sana na wameungana wanafungua Biashara na bidhaa zao na huduma ni cheap, sisi hatutaweza.Tusipo acha hii kasumba ya kwamba ohoo Watanzania hawaaminiani, mara wezi, mara sijui nini hatutaweza vita ya Biashara.
Lazima tuache neno hatuaminiani, inakuwaje ni sisi tu? Wakenya, Waganda, wote hao wanaamininiana isipo kuwa sisi? Whay?
"Nzi akiacha mambo ya ajabu anaweza tengeneza asali, na sisi siku tukiacha mambo ya ajabu ya visingizio tunaweza watoa jasho wachina"
Karibuni.
Wachina niliwahi soma andiko lao moja kwamba unakuta kampuni moja ina share holder 400 wamegawanyika humo humo kuna Wahasibu, Marketing Officer, IT, Wanashera, Wapishi na kadhalika yaani wamekamilika.
Ulaya kipindi Viwanda tunavyo viona leo hii vya madawa na vyakula na kadhalila ni ya Ushirika walianza, walianza kama ushirika na baadae wakatanua na kufungua Makampuni ambazo ziko hadi leo hii.
Tumeona Wasomali wana Umoja sana, wanachangishana Pesa na kufungua kampuni na kweli kampuni husimama, Waarabu hivyo hivyo, Wahindi hivyo hivyo.
Wakenya pia na Waganda nimeona, Binafisi nina rafiki zangu Wakenya wako Tanzania wanafanya mambo ya IT jamaaa walijichanga wako watatu, wakajichanga na kufungua kampuni ya IT, pia wapo ambao nawajua wamejichanga, ingawa kule kwao hii ni kawaida sana, Waganda pia.
Njoo Sasa kwetu Watanzania, yaani hata ndugu tumbo moja pacha ukiwaeleza swala la kuunganisha nguvu hawakuelewi kabisa, yaani hata Kijana kuunganisha nguvu na Baba yake mzazi au Mama yake mzazi bado haiwezekani. Tumekuwa na sababu nyingi sana kubwa kuliko yote ni UMANIFU hii ndo ngao yetu kuu ya kuto kuunganisha mitaji.Lakini mbona kwenye starehe tunaaminiana sana na kuchangishana?
Ni kawaida Tanzania kukuta ndugu wawili Familia Moja wana Biashara za ku compete, mfano ndugu familia moja wote wana Mabasi na yana compete, Wana maduka yana Compete, na kadhalika, hawa ukiwaambia waunganishe mitaji hawakuelewi kabisa.
Investors wengi wanao kuja Tanzania kama hawajakopa basi unakuta wamejichanga, hata Wazungu, unakuta wa mejichanga wanne au watatu na kufungua kampuni Tanzania.Hatutaweza kushindana na wawekezajinwa nje kama hii vita tutaipigana kila mtu kivyake. Niambie kuna Kampuni ipi ya ujenzi inaweza shindana na zile za Wachina au Wajapani? Ipo? Tuna utitiri wa kampuni za ujenzi ila kamwe hazifikirii kuungana na kuwa na kampuni moja strong ya kushindana.
Sisi unakuta kila mtu anataka afuge kuku angalau 500 wa nyama au mayai, Ila je tutaweza kusindana na wawekezaji wanao kuja Tanzania wanafungua Shamba la kuku na kwa siku wana chinja kuku 100, 000? Wanakusanya trei 5000 za mayai kwa siku? Tutawaweza?Kule Tanga naambiwa kuna mchina anafuga Broiler akupeleka sokoni ni kwanza mzigo wake uishe nyie wengine ndo muanze kuuza na unakuta hapo sisi mtu ana kuku 49 ndo anapeleka sokoni.
Sisi Gradute na pesa zetu za Boom tumejibana tutaweza toboa bi a kuungana?
Tunaweza fanya nini?
Nadhani ifike wakati tuache hizi sababu kwamba hatuaminiani, tutazungukana na kadhalila. Kama ndo hivyo basi tunaweza fanya haya;
- Kuweka mikataba yote kwenye maandishi, n kujenga kiwango cha juu kabisa cha uwazi, ni kweli tunapenda janja janja lakini, tunaweza fanya kitu, tunaweza weka misingi ya juu kabisa ya uwazi, shida pia ni uwazi, uwazi tunakuwa hatuna wa kutosha.
- Tuachane na Tamaaa, hizi ndo chanzo kikuu cha watu kusingizia uaminifu uaminifu kumbe ni tamaa tupu.
- Tuachane na kushindana kutaka kuwafurahisha ndugu, jamaa na marafiki, moja ya sababu ni kwamba kila mmoja anataka aonekane mbele ya jamii kwamba anamiliki biashara ya pekeee yake, ana basi lake, ana Daladala lake mwenyewe, ana duka lake mwenyewe, ana kampuni yake mwenyewe ya ujenzi.
- Tuajiri Managment, kama tunaona shida basi tunaunganusha mitaji na kuweka menejiment na sisi tunakaa pembeni kabisa Managemnet ndo inafanya kazi, hii ni nzuri sana ila ni ni kwa wenye mitaji mikubwa tu. Wenye mitaji wanaweza weka Management na ikawa inafanya kila kitu wao wakawa wanapelekewe report tu.
-Tukae tuwaze competition tunazo pata na pia zijazo, na tukisha ziwaza tuache kuwaza hasi, na tuunganishe mitaji.
Ndugu zangu ukweli ni kwamba hatutaweza compete na wageni kama kila mtu ataenda kivyake vitani, hatutaweza na hii vita hatutashindwa, tutashindwa hii vita, wanakuja Wawekezaji kama Wachina wana mitaji mikunwa sana na wameungana wanafungua Biashara na bidhaa zao na huduma ni cheap, sisi hatutaweza.Tusipo acha hii kasumba ya kwamba ohoo Watanzania hawaaminiani, mara wezi, mara sijui nini hatutaweza vita ya Biashara.
Lazima tuache neno hatuaminiani, inakuwaje ni sisi tu? Wakenya, Waganda, wote hao wanaamininiana isipo kuwa sisi? Whay?
"Nzi akiacha mambo ya ajabu anaweza tengeneza asali, na sisi siku tukiacha mambo ya ajabu ya visingizio tunaweza watoa jasho wachina"
Karibuni.