Reginald Mengi: Ipo siku Mafisadi wataongoza nchi

Reginald Mengi: Ipo siku Mafisadi wataongoza nchi

dosama

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2010
Posts
912
Reaction score
959
Mwenyekiti wa makampuni ya IPP bwana Reginald Mengi amesema kwa hali ya kisiasa inavyoendelea ipo siku mafisadi wataongoza nchi kwa kuwa mpaka leo hawajachukuliwa hatua zozote za kuwakamata na kuwafungulia mashataka. Na serikali imekaa kimya
 
Anajitokeza taratibu mwisho wa siku katiba ikiruhusu mara huyooo kwa tiketi ya mgombea binafsi
 
Mpaka dakika hii tunayoongea tayari hii nchi inaongozwa na mafisadi.... wake up Mengi!
 
Mengi kapiga kiroba nini ? Hajui nchi inaongozwa na watu wa aina gani.
 
Anazeeka vibaya sasa huyu mengi, ina maana hajui kuwa tunaongozwa na mafisadi na mazungu wa unga siku nyingi..!?? he must be kidding me..!
 
Kuanzia mkuu wa kaya ni fisadi... au anamaanisha kuna aina nyingine ya mafisadi ambayo itakua hatari zaidi ya hawa tuwaonao sasa ivi?
 
Mengi naye ni fisadi asitudanganye, angalia taarifa za kituo chake cha ITV inavyopendelea mafisadi.
 
...walimtisha akakaa kimyaaa,sasa amekuja kivingine wakati ukweli anaujua,Mzee wangu Mengi lets be serius bhanaa....
 
Mwenyekiti wa makampuni ya IPP bwana Reginald Mengi amesema kwa hali ya kisiasa inavyoendelea ipo siku mafisadi wataongoza nchi kwa kuwa mpaka leo hawajachukuliwa hatua zozote za kuwakamata na kuwafungulia mashataka. Na serikali imekaa kimya
Hata yeye ni fisadi kama hao anaowalalamikia...

Anatumia vyombo vyake vya habari kujikomba kwa watawala ili wamfichie maovu yake. Tanzania mpya baada ya kumtoa mkoloni mweusi wote hawa mafisadi watamulikwa tu. Hivi zile tuhuma zake zilizopelekwa na Rostam TAKUKURU hazina feedback??? Hawa wanajuana...
 
Mzee Mengi binafsi huwa nakuheshimu. Ila hapa sasa heshima yangu kwako imeanza kupungua kabisa. Wacha Unafiki simama hazarani kama siku za nyuma uliposimama bila woga na kututajia Mafisadi PAPA akiwemo MANJI.

Usimumunye maneno wataje hao mafisadi unao wahisi kuwa kuna siku wanaweza kutawala nchi. Si useme tu wazi kuwa Unamzungumzia LOWASSA kwani ndie tunaona akijitahidi Misikitini na Makanisani kujisafisha ili aweze kuwa rais 2015 huku wakati ni FISADI PAPA!!
 
wanaongoza na anawachangia mamilioni mara kwa mara , sasa anamlalamikia nani ? Bali sisi cdm tutahakikisha tunaikomboa nchi hii kutoka mdomoni mwa mamba, hata kama yeye ataendelea kutumia mihela yake kuwasaidia .
 
Mwenyekiti Mtendaji wa IPP, Dk. Reginald Mengi, amesema ikiwa mafisadi hawatadhibitiwa, iko hatari wakajiimarisha kufikia hatua ya kuiongoza nchi siku zijazo.

“Wala rushwa wakubwa ni kina nani na wako wangapi? Ukiniuliza mimi nitakwambia hawazidi wanne, wanafahamika ila sitawataja kwa leo,” alibainisha.

Alisema rushwa kubwa ipo nchini na tuendako ana wasiwasi kuwa wala rushwa wakubwa ndiyo watatawala nchi kupitia matakwa yao kwa nchi kuongozwa na kutawaliwa na watu wasioonekana wala kujulikana.

“Ni watu wenye nguvu wanajipenyeza hadi katika vyombo vya dola, mtu anaweza kupoteza kazi kwa uamuzi wao,” alisema.

Chanzo: Nipashe
 
Mara ngapi tena??!! Utawala uliopo umewekwa na kina nani na kwa matokeo yapi??!! Tutabaki kuwa taifa la wadanganyika!!
 
Back
Top Bottom