Redio Free Afrika, magazeti na Kiswahili

Msongoru

JF-Expert Member
Apr 16, 2008
306
24
Jamani! naamini sana katika ukimya lakini safari hii yamenishinda..... Katika kipindi chake cha asubuhi cha Watanzania tusikilize magazeti, sidhani kama uongozi wa redio hiyo unasikiliza kila siku ama la! Kuna mtangazaji mmoja anaitwa Christina Mbezi, kiswahili chake ni cha kupotosha...

Nisingelalamika sana kama angekuwa anazungumzia au anasoma magazeti hayo nyumbani kwake, ila kwa sababu ya jamii, nadhani hatutendewi haki mtu huyu kuendelea kupotosha lugha yetu kwa muda mrefu kiasi hicho. Amekua akipotosha maneno, mfano Mhariri anasoma mharili! Dalesaram, safali, laisi, uhulu, na maneno mengine mengi ambayo kwa hadhi ya chombo kama hicho sidhani kama ni sawa kulifumbia macho.....

Nimeandika haya nikijua moja kati ya dhima ya vyombo vya habari ni kukuza lugha yetu adhimu, la kama uongozi utaona ni sawa, pengine kwa kuwa hakuna chombo kinachosimamia hayo, basi waendelee. Hata hivyo lazima nikirikwamba ni kwa huyo mmoja tu, wengine wote wamekuwa wasomaji wazuri, wakiitumia lugha sawasawa!
 
Tatizo vyombo vyetu vingi vya habari kama si vyote hawana uwezo wa kuajiri wataalam,hilo ndilo tatizo kubwa kwao unakuta watangazaji wengi wana uelewa mdogo sana, mtu kafeli form 4 ndiye mtangazaji,utakuta mtu mpaka kipindi kinaisha kazi kujisifia tu,
 
kuweni waungwana bana hayo ni mambo ya lafudhi tu na ndo maana hata kiingereza kinatofautiana kutokana na mahali kinapozungumzwa so la muhimu pale ni kwamba ujumbe unafika kwa wakati muafaka acheni kuwa wakosoaji wa kila kitu as if nyie ndo waswahili wa kweli.
 
kuweni waungwana bana hayo ni mambo ya lafudhi tu na ndo maana hata kiingereza kinatofautiana kutokana na mahali kinapozungumzwa so la muhimu pale ni kwamba ujumbe unafika kwa wakati muafaka acheni kuwa wakosoaji wa kila kitu as if nyie ndo waswahili wa kweli.
Mkuu, tofautisha kati ya lafudhi na kukosea neno. Hicho anachokifanya huyo mtangazaji ni makosa msingi katika usanifu wa lugha, siyo lafudhi. Lafudhi ni kitu kingine. Angeweza kutamka maneno vizuri lakini akawa na lafudhi mfano ya kisukuma, kihaya, nk. Hiyo inakubalika.
 
Ajabu ni kwamba uongozi ama wahariri hawachukui hatua!! kama umeshaona mtangazaji fulani ana tatizo fulani, kwa nini asipewe mahala ambapo hapahitaji kusoma sana!!!!!!! au ashauriwe awe mwandishi badala ya kutangaza!!
 
Kuna jamaa huwa ananichekesha sana anasema wamejaa kama pishi la mchele.
Alafu anamalizia makinika nasi.
Lakini uchambuzi wao ni mzuri sana mm naupenda sana.
 
Kuna jamaa huwa ananichekesha sana anasema wamejaa kama pishi la mchele.
Alafu anamalizia makinika nasi.
Lakini uchambuzi wao ni mzuri sana mm naupenda sana.

Ni kweli hata mimi nawependa sana, huwa sikoso kuwasikiliza kila saa 12:30 asubuhi! ila nikishasikia tu Christina Mbezi, huwa nasikia hasira!! najiuliza ni mimi tu ina maana waongozaji hawasikii wakabadilika?
 
Ni kweli hata mimi nawependa sana, huwa sikoso kuwasikiliza kila saa 12:30 asubuhi! ila nikishasikia tu Christina Mbezi, huwa nasikia hasira!! najiuliza ni mimi tu ina maana waongozaji hawasikii wakabadilika?

Bora yule Lilian Mtono.
Jamaa RFA wapo juu kwenye uchambuzi naweza sema kuliko radio yoyote hicho kipindi mm huwa sikosi.
 
hata huyo Tom Chilala mwenyewe ni kimeo tu, kumbuka wakati akiwepo Egbart Mkoko , alikua msomaji makini na mahili wa magazeti katika kipindi kile, Chilala muoa wa kusoma habari zinazoikosoa serikali. Kwangu naona Mtono ni heri.
 
kuweni waungwana bana hayo ni mambo ya lafudhi tu na ndo maana hata kiingereza kinatofautiana kutokana na mahali kinapozungumzwa so la muhimu pale ni kwamba ujumbe unafika kwa wakati muafaka acheni kuwa wakosoaji wa kila kitu as if nyie ndo waswahili wa kweli.
Na tusipokemea hizo unazoziita lafudhi.............. basi hatutakuwa na lugha moja fasaha ya kiswahili..........Idadi ya makabila ndiyo itakuwa sawa na idadi ya "VISWAHILI".......... maana kila aina ya kiswahili itaonekana kwa lafudhi yake.........
 
Mkuu, tofautisha kati ya lafudhi na kukosea neno. Hicho anachokifanya huyo mtangazaji ni makosa msingi katika usanifu wa lugha, siyo lafudhi. Lafudhi ni kitu kingine. Angeweza kutamka maneno vizuri lakini akawa na lafudhi mfano ya kisukuma, kihaya, nk. Hiyo inakubalika.

sijui kama unajua lafudhi na sometimes she was affected by mother tongue language so its better hata mkipunguza majungu yasiyo na maana
 
Njoo huku mikoani ndo utakoma kusikiliza redio. Kifupi siku hizi hakuna anyejali kuhusu mambo hayo ya lafudhi na matamshi. Kwanza wengi wao hawajui hata umuhimu wa hiyo kazi yao ktk jamii. Usishangae kusikia mtangazaji anamsifia mpenzi wake au marafiki zake wa mtaani kwake tena kwa majina, mbaya zaidi anatumia a.k.a zao.
 
Ukimlinganisha na redio zingine bado yupo juu sana mambo ya lafudhi haya mbona humsemi mzee masako anapatia matamshi lakini anarefusha...cha msingi asipotoshe ukweli wa anachokisoma
 
Haha huwanacheka sana akitangaza huyoo Escrow anaiita eskoo...anapotosha kwa kweli...au ndio memo kazini!!??

Umenikumbusha Kibwana Dachi wa chanel ten huyo hakuna kitu asichochapia si magazeti wala habari...nafuu habari ila magazeti ni shidaa sana.
 
Na tusipokemea hizo unazoziita lafudhi.............. basi hatutakuwa na lugha moja fasaha ya kiswahili..........Idadi ya ndiyo itakuwa sawa na idadi ya "VISWAHILI".......... maana kila aina ya kiswahili itaonekana kwa lafudhi yake.........

Kaka hata siku moja huwezi kuchenji lafudhi ya mtu,. Na ndo maana hata katika mada ya Asili ya kiswahili kuna mada ndogo iitwayo lafudhi. Inafahamika wazi kabisa kuwa kiswahili kimetokana lugha za kibantu. Hivo bas kiswahili cha mngoni na kiswahili cha mangi wa arachuga lazma viwe na lafudhi tofauti. Hebu angalia lafudhi ya kiswahili cha mzanzibar unaweza mfananisha na mswahili wa tarime? Ndo maana ktk kiswahili tunasema kuna sabab ambazo znamfanya mtu asiwe mahiri katka lugha ya kiswahili.; mfano, athari ya lugha mama, mfano ukikutana na mnyakusa aliyekulia unyakyusani badala ya kukwambia, Naomba viatu vyangu. Atakwambia, Naomba fiatu fyangu. Kwake yeye yuko sawa na kumrekebsha huwez sabab keshaathirika na lugha mama. Hivo bas naomba nihitimishe kwa kusema Christina Mbezi co anapenda kusema hvo bali ndivo alivo na kumbadilisha huwezi. Na hiyo haimaanishi lugha ya kiswahili haitakuwa,, bro kwani wewe unauhakika kuwa huwa unaongea kiswahili kwa ufasaha bila kuharibu sarufi ya kiswahili hata siku moja? Imposible.
 
sijui kama unajua lafudhi na sometimes she was affected by mother tongue language so its better hata mkipunguza majungu yasiyo na maana

Unajua maana ya majungu wewe au umekariri! Hoja hapa ni usahihi wa lugha na sio lafudhi. Kama amekuwa affected kiasi hicho basi hiyo nafasi haimfai maana ata affect ňa wengine kama ilivyo ku-affect wewe.
Mtu analeta hoja ya maana wewe unaita majungu! Eti yasiyo na maana, kwani kuna majungu yenye maana! Ulipewa masikio mawili na mdomo mmoja ili usikilize zaidi kuliko kuongea.

Sikiliza ujifunze punguza ujuaji...
 
Back
Top Bottom