REDET walishazungumza mapema! Watu wakawakejeli kwamba eti wanatumiwa!! Gazeti la Tanzania Daima likadai eti REDET inatumiwa na Kikwete; kwamba REDET wanapotoa utafiti kuonesha kukubalika kwa Kikwete kunajenga saikolojia ya wapiga kura wamchague Kikwete!! Aibu zaidi, Tanzania Daima waliibuka na tahariri iliyoikandia REDET; kwavile tu ripoti hiyo ya REDET ilionesha Kikwete angeshinda kwa asilimia nyingi endapo uchaguzi mkuu ungefanyika wakati wa utafiti uliokuwa umefanyika na REDET!
Bila shaka Tanzania Daima wangekubaliana na utafiti wa REDET endapo ungesema CHADEMA kingeshinda!! Wakati Tanzania Daima walipotoka na tahariri ya kukejeli utafiti wa REDET, walisahau kwamba siku chache tu kabla ya hapo wao walikuwa wameibuka na kura za maoni zilikuwa zimeendeshwa humu JF!
Hata wana CCM nao wakaupinga utafiti wa REDET, kisa tu kilitabiri mabaya kwa wabunge kadhaa kwamba wangepigwa chini!! KIKO WAPI? Nyota njema imeonekana asubuhi! Asubuhi asubuhi, tayari wabunge kadhaa wa CCM wamegalagazwa hata kabla ya uchaguzi mkuu wenyewe bado! Nasikia karibi wabunge 50 chali na game bado linaendelea! Hao ni wale waliopteza mikononi mwa wana-CCM wenzao! Je, ni wangapi kwa waliosalia watakaopoteza viti vyao kwa upinzani?!
Mimi si Mwana CCM, CHADEMA wala REDET; ila ningependa kuwashauri Watanzania kujenga utaratibu wa kuamini tafiti zetu! Sina hakika, lakini naamini REDET imeundwa na wasomi hivyo kubeza tafiti zao ni kubeza umuhimu wa wasomi wetu.
Bila shaka Tanzania Daima wangekubaliana na utafiti wa REDET endapo ungesema CHADEMA kingeshinda!! Wakati Tanzania Daima walipotoka na tahariri ya kukejeli utafiti wa REDET, walisahau kwamba siku chache tu kabla ya hapo wao walikuwa wameibuka na kura za maoni zilikuwa zimeendeshwa humu JF!
Hata wana CCM nao wakaupinga utafiti wa REDET, kisa tu kilitabiri mabaya kwa wabunge kadhaa kwamba wangepigwa chini!! KIKO WAPI? Nyota njema imeonekana asubuhi! Asubuhi asubuhi, tayari wabunge kadhaa wa CCM wamegalagazwa hata kabla ya uchaguzi mkuu wenyewe bado! Nasikia karibi wabunge 50 chali na game bado linaendelea! Hao ni wale waliopteza mikononi mwa wana-CCM wenzao! Je, ni wangapi kwa waliosalia watakaopoteza viti vyao kwa upinzani?!
Mimi si Mwana CCM, CHADEMA wala REDET; ila ningependa kuwashauri Watanzania kujenga utaratibu wa kuamini tafiti zetu! Sina hakika, lakini naamini REDET imeundwa na wasomi hivyo kubeza tafiti zao ni kubeza umuhimu wa wasomi wetu.