Recipe ya Kauzu wa Kigoma

Toa vichwa (hii kwa mimi japo wenyewe wa Kigoma hawatoi),
Chemsha maji ya moto weka dagaa zako kiasi cha upendacho, acha wakae kwenye hayo maji ya moto huku waandaa viungo vingine,

Kata kitunguu maji cha kutosha,
Nyanya chungu na Bamia (ukipenda)
Karoti na Hoho (ukipenda)
Nyanya maji,
Ndimu au Limao,
Mafuta ya Mawese/Alizeti/Pamba/Mzeituni
Waweza kuweka tui la nazi au Karanga,
Chumvi,

Jinsi ya kupika,
Toa dagaa zako kwenye maji waweke pembeni,
Weka chombo chako cha kupikia kwenye moto, kikipata moto weka mafuta kiasi, weka dagaa zikaange kama dakika mbili au tatu maji maji yakauke, weka vitunguu maji, kaanga hadi viive, weka nyanya chungu, bamia, karoti na hoho, changanya vizuri mchanganyiko wako hadi viive, kisha weka nyanya maji na chumvi changanya acha ziive,
Baada ya dakika tano utaweka limao/ndimu na maji kidogo acha tena kwa dakika tatu hakikisha viungo vyako yaan nyanya chungu na bamia vimeiva kisha epua tayari kwa kuliwa,

Kama utahitaji kuweka tui la nazi au karanga basi hapo ndio muda wake sahihi, badala ya kuweka maji kidogo utaweka tui na kulipoza lisikatike hadi liive na tayari kwa kuliwa,

Waweza kula kwa Ugali, Wali hata Chapati.
 
Toa vichwa (hii kwa mimi japo wenyewe wa Kigoma hawatoi),
Chemsha maji ya moto weka dagaa zako kiasi cha upendacho, acha wakae kwenye hayo maji ya moto huku waandaa viungo vingine,

Kata kitunguu maji cha kutosha,
Nyanya chungu na Bamia (ukipenda)
Karoti na Hoho (ukipenda)
Nyanya maji,
Ndimu au Limao,
Mafuta ya Mawese/Alizeti/Pamba
Waweza kuweka tui la nazi au Karanga,
Chumvi,

Jinsi ya kupika,
Toa dagaa zako kwenye maji waweke pembeni,
Weka chombo chako cha kupikia kwenye moto, kikipata moto weka mafuta kiasi, weka dagaa zikaange kama dakika mbili au tatu maji maji yakauke, weka vitunguu maji, kaanga hadi viive, weka nyanya chungu, bamia, karoti na hoho, changanya vizuri mchanganyiko wako hadi viive, kisha weka nyanya maji na chumvi changanya acha ziive,
Baada ya dakika tano utaweka limao/ndimu na maji kidogo acha tena kwa dakika tatu hakikisha viungo vyako yaan nyanya chungu na bamia vimeiva kisha epua tayari kwa kuliwa,

Kama utahitaji kuweka tui la nazi au karanga basi hapo ndio muda wake sahihi, badala ya kuweka maji kidogo utaweka tui na kulipoza lisikatike hadi liive na tayari kwa kuliwa,

Waweza kula kwa Ugali, Wali hata Chapati.
Asante sana; umetoa maelezo ya kina sana, na katika wiki mbili zijaziojiunge na mimi hapa tena nikulteee mrejesho.

-Kich.
 
Kwa miaka 20 sasa huwa ninampikia shemeji yako Asprin mapishi haya nikiyokueleza na anaridhika.
Dagaa wa kigoma walivyo wagumu, usiwaroweke halafu ukawatose kwenye mafuta hahaha hapo utatoa nyama ngumu kama ya goti ndio maana wengi walikua hawapendi kula kumbe walikosea jinsi ya kuandaa.

Ni kweli hawana michanga lakini wanarowekwa ili walainike kidogo na wanatoswa kwenye mafuta kwanza ili kukata shombo ya dagaa vivyo hivyo kwa dagaa wa mwanza, ukiweka nyanya zikaiva halafu ukaja kuweka dagaa hilo shombo lake itasababisha familia nzima ichukie dagaa.
 
Dagaa wa kigoma walivyo wagumu, usiwaroweke halafu ukawatose kwenye mafuta hahaha hapo utatoa nyama ngumu kama ya goti ndio maana wengi walikua hawapendi kula kumbe walikosea jinsi ya kuandaa...
Asante sana kwa kuwa mambo murua kabisa; Sky Eclat amenihakikishia kuwa amekuwa anamchangia hivyo mme wako kwa miaka 20 sasa na mambo yao yanazidi kung'ara.

Kesho nitaaanza na ushuri huu halafu nitaleta mrejesho; ila swali langu je kwa vile siwezi kupata mafuta ya mawese, je ni haki nitumie mafuta ya mizeituni? Mafuta ya nazi huwa siyapendi sana ingawa naweza kuatumia pia.
 
Asante sana kwa kuwa mambo murua kabisa; Sky Eclat amenihakikishia kuwa amekuwa anamchangia hivyo mme wako kwa miaka 20 sasa na mambo yao yanazidi kung'ara. Kesho nitaaanza na ushuri huu halafu nitaleta mrejesho; ila swali langu je kwa vile siwezi kupata mafuta ya mawese, je ni haki nitumie mafuta ya mizeituni? Mafuta ya nazi huwa siyapendi sana ingawa naweza kuatumia pia.
Eeh mafuta ya Mzeituni hayana shida pia,

 
Loweka dagaa kwa saa moja na uwaoshe kutoa mchanga. Weka mafua jikoni yakipata moto kaanga vitunguu, vikiwa tayari weka dagaa, malizia na nyanya chungu, ndimu na chumvi.
Niko kwenye hatua za mwisho mwisho kutekeleza recipe yako; I am serious Swali langu ni je ndimu niweke tui la ndimu au vipande vya ndimu, na iwe ni ndimu kiasi gani kwa mlo wa watu wawili wa kawaida? Ji nisiweke pilipili?
 
Niko kwenye hatua za mwisho mwisho kutekeleza recipe yako; I am serious Swali langu ni je ndimu niweke tui la ndimu au vipande vya ndimu, na iwe ni ndimu kiasi gani kwa mlo wa watu wawili wa kawaida? Ji nisiweke pilipili?
Tui la ndimu tu
 
Tui la ndimu tu
Je nikiweka zile pilipili kubwa sijui zinaitwaje pamoja na bamia itakuwa ni sawa tu havitaharibu recipe yako?

1619532662524.png
1619532730298.png
 
Sky Eclat na wote mliochangia kwenye thread hii, ninawapa mrejesho. Nilifuata maelekezo ya Sky Eclat pamoja na mabadiliko mado0go madogo hapa na pale nikaweka ingredients zifuatazo. Kama una njaa usisome usije kuchafua sakafu kwa udenda

1633569249364.png

Baadaye nikachemsha mafuta ya mzeituni na kuchanganya viungo.

1633569481681.png



Nikamalizia kwa kusonga Ugali kwenda na kauzu hao. Usiniulize ni nini kilichofuatia kwani baaya ya muda mfupi tu sifuria zote zilikuwa
tupu.
 

Attachments

  • IMG_1060.mp4
    11.3 MB

Similar Discussions

Back
Top Bottom