Tatizo liliotukumba na linaloendelea kutukumbuka ni nidhamu kwenye Ulinzi, wakati wa Ramos na hata Alaba walikuwa wanaweka kabisa line, hutakiwi kuvuka huo mstari, ila kwasasa hakuna wa kumwambia mwezie hilo jambo, tulifungwa magoli mawili kutokana na hiyo hali, la kwanza kupitia kwa Mendy, na la pili kwa Vazquez.
Ancelloti ni kweli ametupa vingi, ila ana shida moja tu hajui kubadilika na wakati., ana ile hali ya kutokubali kubadilika aka kumuamini mchezaji hata kama hana anachompatia., hao vijana tulionao wana uwezo mzuri tu kama watapata mtu sahihi wa kuwatumia inavyotakiwa, shida inatokea ni kuwa kuna baadhi itabidi waanzie bench, hapo ndipo Ancelloti anapokuwa muoga.