Real Madrid (‎Los Blancos) | Special Thread

Atheltic 1-1 Real Madrid (Goal: Isco) (Assist: Bale)


DnKZQ8NWwAICiU-.jpg:large
 
Yaani hawa Bilbao wameuza Kepa nafasi yake imechukuliwa na dogo mwingine moto. 16 shots but Real Madrid couldn't score. Naona nafasi ya De Gea kwenye National Team inavutwa shati.
 
HAYA ule utamu wa Ligi ya Mabingwa Ulaya umerudi tena. Safari hii mambo ni moto kwelikweli, maana ile hatua ya makundi tu inaanza, Liverpool inakipiga na Paris Saint-Germain.

Unaambiwa hivi, huo ni mtihani mzito kwa Kocha Jurgen Klopp, ambaye atapima kikosi chake kama kweli kipo vizuri kwa mapambano mazito baada ya kushinda mechi zake zote tano za kwanza kwenye Ligi Kuu England.

Mechi hiyo ngumu itapigwa leo Jumanne uwanjani Anfield, ambapo kutakuwa na shughuli nyingine pevu huko San Siro, wakati Inter Milan itakapoikaribisha Tottenham Hotspur.

Mechi nyingine kali itazishuhudia AS Monaco ikikipiga na Atletico Madrid, wakati Barcelona itakuwa na kibarua na PSV, huku Club Brugge ikiwa na kasheshe la kuikabili Borussia Dortmund na FK Crvena Zvezda itacheza na Napoli.

Kesho Jumatano kutakuwa na mechi nyingine kali kwelikweli, wakati Manchester City itakapocheza na Lyon, huku Real Madrid ikicheza na AS Roma. Man United nayo itaanzia ugenini kwa Young Boys, wakati Valencia itacheza na Juventus, huku Viktoria Plzen itacheza na CSKA Moscow na Shakhtar Donetsk itacheza na Hoffenheim. Kesho Jumatano pia kutakuwa na mechi kati ya Ajax itakayokuwa nyumbani kucheza na AEK Athens na Benfica itakipiga na Bayern Munich.
 
Back
Top Bottom