masssaiboi
JF-Expert Member
- Feb 10, 2009
- 636
- 132
Nimetoka kuangalia pambano la bondia mtanzania aitwaye Obote Ameme na kijana mdogo wa kizungu, pambano limefanyika nchini Uswiss na lilikuwa linaonyeshwa na kituo cha Sky sports hapa UK. Lilikuwa ni pambano la utangulizi kabla ya pambano la Bingwa Klitchiko na lilikuwa la raundi nne.
Kwa kweli jamaa amejitaidi kwa kiasi chake lakini ukilinganisha na mtoto aliyekuwa anacheza naye wala hamfikii kabisa. Katika suala la ufundi wa kupigana bado yuko nyuma sana kwani muda mwingi alikuwa anajikunjamania tu.
Pia alikuwa na msaidizi mmoja tu ukilinganisha na mwenzie aliyekuwa na watatu, nilichosikia kutoka kwa huyo mshkaji ktk raundi zote nne ni pale alipomwambia maneno haya tu ''mbavu hizo mbavu hizo, we unaweka gadi tu atakuumiza mwenzio''
Mie simlaumu huyu bondia ila lawama ni kwa wanasiasa wetu kwa kushindwa kuendeleza vipaji, jamaa alivyoonekana ni kama vile hakuwa na msaada wowote kutoka wizara husika na mara zote walipokuwa wanaitaja Tanzania nilijisikia vibaya sana tu.
Kwa kweli jamaa amejitaidi kwa kiasi chake lakini ukilinganisha na mtoto aliyekuwa anacheza naye wala hamfikii kabisa. Katika suala la ufundi wa kupigana bado yuko nyuma sana kwani muda mwingi alikuwa anajikunjamania tu.
Pia alikuwa na msaidizi mmoja tu ukilinganisha na mwenzie aliyekuwa na watatu, nilichosikia kutoka kwa huyo mshkaji ktk raundi zote nne ni pale alipomwambia maneno haya tu ''mbavu hizo mbavu hizo, we unaweka gadi tu atakuumiza mwenzio''
Mie simlaumu huyu bondia ila lawama ni kwa wanasiasa wetu kwa kushindwa kuendeleza vipaji, jamaa alivyoonekana ni kama vile hakuwa na msaada wowote kutoka wizara husika na mara zote walipokuwa wanaitaja Tanzania nilijisikia vibaya sana tu.