RC Hapi: Mimi ni mtu hatari, usiniudhi, usinichezee!

RC Hapi: Mimi ni mtu hatari, usiniudhi, usinichezee!

Kwajinsi nilivoangalia ile clip ya mlalamikaji na mlalamikiwa, nafikili yule mama alitakiwa kuadhibiwa vikali sana ili iwe funzo kwa wengine kama yeye.

Haiwezekani mtu kuvunjiwa nyumba kwa maagizo ya mwenyekiti wa mtaa au diwani au meya. Eti hata mwanasheria, Injinia, Afisa mipango miji, Afisa aridhi, wote hawaelewi ila yeye huyo mama ndo anaelewa zaidi. Kibaya zaidi mzee wa watu kila anapokwenda kupanga mwenyekiti anakwenda kupiga biti.
 
viongozi wa bongo baba yao mmoja hivyo usishangae
 
Kuna haja ya wanaopewa dhamana ya madaraka kupimwa afya ya akili, kuwa na sessions na psychologists, kuwa na semina za mara kwa mara za maadili ya uongozi n.k...

Kauli kama zile ukizitoa nchi zilizoweka mbele utawala wa sheria, pengine sasa kuna kiongozi angekuwa anathibisha uhatari wake mbele ya jaji mahakamani...
 
Nchi yetu ina viongozi wachache sana,anajua misingi na kanuni za uongozi lakini hayo yote anayaweka kando.Yeye ni mtu hatari sana?,uhatari wake ni upi? .Rais wetu anayo kazi
 
Nchi yetu ina viongozi wachache sana,anajua misingi na kanuni za uongozi lakini hayo yote anayaweka kando.Yeye ni mtu hatari sana?,uhatari wake ni upi? .Rais wetu anayo kazi
Ni hatari kwa wale wanaonyanyasa wanyonge.
 
Viongozi wetu wanafanya haya kwa lengo linalofanana. Na si kwa mujibu wa sheria na utu wa Mtanzania
 
Taasisi moja muhimu sana duniani kuliko zote imedharauliwa siku hizi na kuonekana kuwa haina tija na haya ndo matokeo yake. Taasisi ya ndoa
 
Usiniudhi...usinichezee..
Ninachojua ni mtu mwenye misimamo isiyotetereka. Haamini sana katika mwanadamu. Alinyanyaswa sana na kina membe alipokuwa lumumba sababu alikataa kutumiwa. Na membe alimuambia utajua mi nani. Alidhani angekuwa rais.

Badae walitaka wamtoe lumumba wampeleke vichororoni sababu ya misimamo yake isioyumba. Hata hivyo sababu anaamini kila jambo ni la Mungu na si mwanadamu basi Magu akapita na kumteua DC na badae RC.

Huyo ndio Ally Happi. Muda utasema.
 
Ninachojua ni mtu mwenye misimamo isiyotetereka. Haamini sana katika mwanadamu. Alinyanyaswa sana na kina membe alipokuwa lumumba sababu alikataa kutumiwa. Na membe alimuambia utajua mi nani. Alidhani angekuwa rais.

Badae walitaka wamtoe lumumba wampeleke vichororoni sababu ya misimamo yake isioyumba. Hata hivyo sababu anaamini kila jambo ni la Mungu na si mwanadamu basi Magu akapita na kumteua DC na badae RC.

Huyo ndio Ally Happi. Muda utasema.
.mh
Huyu si aliwahi kuwa Iringa huyu?
Kwa huu wasifu na aliyoyafanya iringa,no thank u!
 
Ni baadhi ya maneno yaliyotamkwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa, mdogo wangu na Mwanasheria mwenzangu Ally Hapi. Alikuwa akielekea kutoa amri ya kukamatwa,kuwekwa ndani,kuhojiwa na kufikishwa mahakamani kwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa na Diwani wa Viti Maalum huko Iringa kwa tiketi ya CHADEMA.

View attachment 2306806

Kadiri ya clip ya video niliyoitazama kwa MillardAyo,kuna Mzee mmoja alilalamika kwa RC Hapi kuwa amebomolewa nyumba yake kwa amri ya Mwenyekiti na Diwani huyo wa CHADEMA. Mlalamikaji akajitambulisha kama Mwenyekiti wa Tawi la CCM.Mwanamama mhusika alijitetea bila mafanikio. Akakamatwa na askari wa kike wa JWTZ baada ya kukosekana kwa askari wa kike wa Polisi.

Kimsingi,maneno ya aina hiyo yamekuwa ya kawaida kwa Wakuu wa mikoa na wilaya nchini. Yana tija gani? Yaendelee?
Naye ameshughulikiwa na mwanamke leo..ngoma droo
 
Usiniudhi...usinichezee..
Alianza kama wenzake kina Sabaya na Makonda, ku personalize uongozi wa umma.
Uongozi wa umma siyo umimi.... mimi... mimi.... kama mwendazake.
Angekuwa broadminded angesalimika.

Na alisema atawashughuliki wazee wastaafu .....astakafulahi.... hao wamerudi!!
Kanyoa na kusuka kabisa!
 
Back
Top Bottom