RC Hapi: Mimi ni mtu hatari, usiniudhi, usinichezee!

RC Hapi: Mimi ni mtu hatari, usiniudhi, usinichezee!

Nikirudi shule nianzie kusoma level gani?
Grade 4 inawatosha ninyi wabongo mkaanze kusoma nini maana ya yafuatayo

1) wewe ni nani?? Upo hapa duniani kwa dhumuni gani??

2) utu ni nini ??

3) haki zako za msingi na wajibu wako uwapo popote duniani

4) maana ya siasa na demokrasia ni nini?? nk

Ukishayajua haya utayajua mengi zaidi
 
Vyama vya upinzani ni adui namba moja wa taifa la Tz katika udikteta wa awamu ya jpm?
Naona nguvu nyingi sana zinatumika kuudhibiti kuliko juhudi za kudhibiti ujinga na maradhi. Shule hazina walimu wa kutosha wala vitabu lakini fedha zinapelekwa kununua wapinzani ( oil chafu, kwa mujibu wa Nepi Nnauye). Shule za serikali zinazalisha zero kwa juhudi lakini serikali inahangaika na wapinzani. Ipo siku dikteta wetu atakamatwa ashitakiwe the Hague kwa unyama dhidi ya raia wake.
 
Vipi wale waliokuwa wakimuita jk dhaifu..walikuwa wanastahili kumuita vile?? Au shida ni pale mtu anapojinasibu kama yeye hachezewi?
Baba wa watu walimdhihaki sana mungu anawalipa. Lakini JK alisema uongozi ukiwa wa vijana moto utawaka
 
Ni baadhi ya maneno yaliyotamkwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa,mdogo wangu na Mwanasheria mwenzangu Ally Hapi. Alikuwa akielekea kutoa amri ya kukamatwa,kuwekwa ndani,kuhojiwa na kufikishwa mahakamani kwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa na Diwani wa Viti Maalum huko Iringa kwa tiketi ya CHADEMA.

Kadiri ya clip ya video niliyoitazama kwa MillardAyo,kuna Mzee mmoja alilalamika kwa RC Hapi kuwa amebomolewa nyumba yake kwa amri ya Mwenyekiti na Diwani huyo wa CHADEMA. Mlalamikaji akajitambulisha kama Mwenyekiti wa Tawi la CCM.Mwanamama mhusika alijitetea bila mafanikio. Akakamatwa na askari wa kike wa JWTZ baada ya kukosekana kwa askari wa kike wa Polisi.

Kimsingi,maneno ya aina hiyo yamekuwa ya kawaida kwa Wakuu wa mikoa na wilaya nchini. Yana tija gani? Yaendelee?
Mkuu ungeeleza pia kuwa katika hiyo Hugo mzee kika nyumba anayokwenda kupanga huyu diwani akiwapiga mkwara wenye nyumba ili huyo mzee alale nje.
Kusena clip hiyo inasikitisha kuona MTU kwa matakwa take anaweza kuchukuwa mgambo na kwenda kubomoa nyumba ya MTU bila idhini ya mahakama.
 
Kama yanamfurahisha bwana wao, yaendelee tu.

Kwanza naona watu wameanza wameanza kuzoea tayari mfumo pofu huu.
 
Ni baadhi ya maneno yaliyotamkwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa,mdogo wangu na Mwanasheria mwenzangu Ally Hapi. Alikuwa akielekea kutoa amri ya kukamatwa,kuwekwa ndani,kuhojiwa na kufikishwa mahakamani kwa Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa na Diwani wa Viti Maalum huko Iringa kwa tiketi ya CHADEMA.

Kadiri ya clip ya video niliyoitazama kwa MillardAyo,kuna Mzee mmoja alilalamika kwa RC Hapi kuwa amebomolewa nyumba yake kwa amri ya Mwenyekiti na Diwani huyo wa CHADEMA. Mlalamikaji akajitambulisha kama Mwenyekiti wa Tawi la CCM.Mwanamama mhusika alijitetea bila mafanikio. Akakamatwa na askari wa kike wa JWTZ baada ya kukosekana kwa askari wa kike wa Polisi.

Kimsingi,maneno ya aina hiyo yamekuwa ya kawaida kwa Wakuu wa mikoa na wilaya nchini. Yana tija gani? Yaendelee?
wamelewa madaraka
 
Back
Top Bottom