RC Chalamila avunja mkataba wa Serikali na JWTZ wa ujenzi wa ofisi za halmashauri za Busokelo

johnthebaptist

JF-Expert Member
May 27, 2014
83,915
141,879
Mkuu wa mkoa wa Mbeya Albert Chalamila amevunja mkataba wa ujenzi wa jengo la halmashauri ya Busokelo mkoani Mbeya kati ya serikali na kampuni ya JWTZ Mzinga.

Chalamila amesema ujenzi huo ulioanza mwaka 2018 umekuwa ukisuasua hivyo pamoja na kwamba wajenzi hao ni chombo cha dola hawezi kuwavumilia. Amewataka halmashauri ya Busokelo kutafuta mkandarasi mwingine haraka na ujenzi uendelee mara moja.

Naye msimamizi wa ujenzi huo kutoka jeshini Mzinga Kanali Jackson amesema ujenzi huo umekuwa ukisuasua kwa sababu halmashauri hiyo imekuwa ikitoa fedha kwa kuchelewa sana na hakukuwa na namna ya kuendelea na ujenzi wakati fedha hakuna.

Source Eatv habari!

Maendeleo hayana vyama
 
Chalamila ni kiumbe mjanja mjanja sana! Isije ikawa ameshatafuta mzabuni mwingine ili ale 10% ya faster faster! Maana huu ni mwaka wa uchaguzi.

Maamuzi yanaonekana ni ya kukurupuka kabisa. Yaani Msimamizi ameeleza wazi ya kwamba Halmashauri imekua ikitoa fedha za ujenzi kwa kusua sua! Badala ya kumkomalia DED atoe hela za ujenzi kwa wakati, yeye anaamua kuwadhalilisha Wanajeshi wetu!!
 
Tulisema Jeshi liachwe lisishiriki siasa, kazi za kiraia na biashara za moja kwa moja na serikali, maana itakuja tokea hivi ionekane jeshi linashindwa vitu vidogo vidogo sana.

Jeshi lishiriki mambo ya dharura tu! Madhara tutayaona mbele!
Ndio dharau inapoanzia hapo,bado waanze kufokwa hadharani
 
Hivi huyu RC anatambua hadhi ya JWTZ hata mbele ya aliyemteua? Katika taasisi ambazo huogopeka hata kwa viongozi wakuu wa nchi ni jeshi.

Kwa kuwa Chalamila kalianzisha yeye mwenyewe, basi ni lazima aanzev kujiandaa kisaikolojia kwa lolote lile. Maana Mkuu kwa sasa inaonyesha mambo ya uchaguzi hayamweki ktk "mood" nzuri, kwa hiyo ikitokea "stress" ya zaidi kwake, ni lazima atumbue wasaidizi wake wenye kujipendekeza mno kwake na kufanya teuzi mpya.

Shauri zake, oohoo ajifunze kwa mwenzake Gambo.
 
Kuna kosa gani Kwani? Hao walivyopewa Kazi washaonesha kusuasua kwanini asiwapige chini

Ova
 
Hivi huyu RC anatambua hadhi ya JWTZ hata mbele ya aliyemteua? Katika taasisi ambazo huogopeka hata kwa viongozi wakuu wa nchi ni jeshi.

Kwa kuwa Chalamila kalianzisha yeye mwenyewe, basi ni lazima aanzev kujiandaa kisaikolojia kwa lolote lile. Maana Mkuu kwa sasa inaonyesha mambo ya uchaguzi hayamweki ktk "mood" nzuri, kwa hiyo ikitokea "stress" ya zaidi kwake, ni lazima atumbue wasaidizi wake wenye kujipendekeza mno kwake na kufanya teuzi mpya.

Shauri zake, oohoo ajifunze kwa mwenzake Gambo.
Hadhi ya JW haiathiriwi na kuvunjwa mkataba wa ujenzi. Kama kweli kasi ya ujenzi haiendi inavyopaswa bila sababu basi ni halali tu mkataba kuvunjwa.
Cha msingi ni uchunguzi tu kufanyika ili kubaini madai yao au ya RC ni yapi yenye ukweli.
 
Back
Top Bottom