RC Arusha vs kituo cha redio kilichomhoji Lema

RC Arusha vs kituo cha redio kilichomhoji Lema

ndiyo maana inabidi tukomae na hii katiba mpya ili kuondoa uozo wa ma-rc, ma-dc..

kabisa. Anajua kapewa kishkaji hakuna wa kumuhoji! Ndo maana analeta ubabe mbuzi. Hazitakiwi kabisa kuwepo kwenye katiba. Zinafuja pesa bure.
 
Ndio maana tunataka katiba mpya ili kama sio kufuta kabisa hivi vyeo basi wawekewe mipaka ya utendaji! Wanapewa vyeo kishkaji halafu vinawalevya halafu wanafanya upuuzi..

Vijana tunatakiwa tujiweke mstari wa mbele kudai na kupigania katiba tunayoitaka ili wajinga kama hawa wasipate nafasi ya kutudhalilisha tena. Sisi ndio tunaoadhirika zaidi. Fikiria kama rc akiamuru kituo hicho kifungwe ni vijana wangapi watakosa ajira! Ni wangapi watakuwa ombaomba? Tutajikuta tunakimbiana mjini!
 
Nchi hii kama hamjajua inaongizwa kijeshi! Wakuu wa mikoa na DC wengi ni maafisa aidha wastaafu au UWT kutoka jeshini au wale maraia. Hili limekuwa kikwazo kikubwa sana kiutendaji hasa mikoa yenye upinzani mkubwa.
Ukichunguza mikoa kama Mbeya na Arusha inaongozwa na hao niliowataja hapo juu ambao wanajiona wapo juu ya sheria. Ndiyo maana mikoa hiyo iko political unrest. Ni imani yangu Arusha machafuko makubwa sana yanakuja endapo RC huyo hata acha kasumba yake ya kijinga aliyokuja nayo ya kutumika upande mmoja badala ya wananchi.
Mbona kipindi kulipokuwa na mgomo wa dala dala nasikia alikwenda Triple A FM kuwajulisha wanachi juu uharamu wa mgomo huo na kuwatoa wasiwasi hali itakuwa shwari.
Mbona watu hawakuilalamikia radio hiyo, au kwa sababu inamilikiwa na mmasai mmoja kada wa CCM?
Hoja ya msingi ni yeye kuomba kumbu kumbu ya mazungumzo hayo ili kama G. Lema ataona alikosea amburuze mahakamani badala ya kuingilia uhuru wa vyombo vya habari.
 
ndo tatizo la tz..jitu lilikwa sijuo pishi magereza unalipa u rc linaweweseka tu nakuwehuka katika maamuzi..ndo maana watu wanawaingiza vijiti matakoni kama walivomfanya gadafi

Chezo wewe ni mwenzangu kabisaa una hasira ya ukweli nimeona. Hawa watu subiri maandamano yaanze mbona wako kwenye list/.
 
Mbona kahama FM na karagwe Fm hayo ni mambo ya kawaida tu , hapo arusha kuna nini mpaka kila mkuu anaona lema kawaharibia mambo
 
Yalimshinda Bokasa na Idd Amini. Na Gadhafi yakamfanya alie kama mtoto wakati anakichungulia kifo. Huyu jamaa atayaweza?
 
Katika hali isiyotarajiwa leo majira ya saa 9 mkuu wa mkoa Arusha aliamuru uvamizi katika kituo cha redio ( jina sikulinasa lakini sio triple A).

Madai ni kuwa kituo hicho kilifanya mahojiano na mh. Lema na akatumia nafasi hiyo kumtukana RC. Polisi walifanya upekuzi na kusikiliza kumbukumbu za kipindi hicho na kuwahoji baadhi ya wafanyakazi kwa karibia masaa matatu. Kisha waliondoka wakidai watarudi kama watabaini kuna kosa lilitendeka.

SOURCE WAPO FM.

Ndo madhara ya kugawa madaraka kwa wasio na sifa za kuongoza.
Huyo mkuu wa mkoa hata ubalozi wa nyumba kumi hawezi kuongoza
 
Mkurugenzi wa kituo hicho cha sunrise ndiye aliyefanya mahojiano na mh. g lema (Mb), siku hiyo lema alieleza mambo Mengi pamoja na kuhusu kukamatwa kwake kila mara. nakumbuka mh lema alizungumzia kuhusu mgogoro wa umeya, napia rc anataka kukuza mgogoro badala ya kutatua, hapo ndipo alipotumia neno mjinga. mwandishi alimuomba mh lema afute usemi wake huo wa kumwita rc mjinga!! mh lema akasema "rangi nyekundu acha iitwe nyekundu na nyeusi iitwe nyeusi". maoni yangu, mwandishi hakuwa na shida ila rc amtafute lema apambane naye kuliko kuongeza idadi ya maadui.

Kama ushahidi upo kwamba mh. Lema ndiye alimuita RC mjinga, kwanini sasa aanze kutumia kodi zetu vibaya kwa kuendesha ubabe dhidi ya kituo cha redio?
Kama kweli RC anajiamini, kwa nini asimuulize mh. Lema mwenyewe, au keshaona Lema majimarefu sasa anatafuta maji ya kina kifupi ili avuke mto!?
 
Eh,
magesa!au kwakuwa ni mwenyekiti wa kamat ya ulinz na usalama?

Hilo laweza kuwa sababu, lakini najiuliza hivi ukiwa mwenyekiti wa kamati fulani maana yake wewe ndiyo ufaidike zaidi kuliko wengine? inanikumbusha kauli mbalimbali zinazotolewa na wanasiasa ambao kwa mtazamo wangu wameishiwa hoja, kwamba kama yeye au mzazi wake ama mmojawapo katika ukoo alishiriki kupigania uhuru basi ndiyo bora kuliko wananchi wengine wote waliopo hivyo kuona ndiyo pekee wanaofaa kuwa viongozi. Najiuliza kwamba hivi kila mtu akiamka na kupigania uhuru wake binafsi hali itakuwaje kwa kuwa matarajio ilikuwa wananchi wote wawe huru na kuwa na haki kuongoza na kuongozwa lakini nionavyo sasa sivyo katika nchi nyingi za kiafrika. Nashindwa kutofautisha kati ya utawala wa wazalendo na utawala wa wageni kwa maana ya wazungu na wengine wasio wenyeji wa Afrika. Je kuna haja ya kuendelea na hali hii kweli? kwamba mwenyekiti anaamrisha wasachiwe badala ya kupeleka malalamiko katika vyombo vinavyohusika kwa maana ya TCRA? Hivi kila mmoja akitumia nafasi yake kunufaika hali itakuwaje?
 
WanaApolo wa siku hizi waoga wanatembea tu na ma-cruiser, wangekuwa ni wale wa zamani wanaotembea na Baja angeshasepeshwa huyo

Hao ni wa Afgem.
Wagumu bado wapo.
Kikinuka, utawaona.
 
Hivi Mulongo ni mkuu wa Mkoa au Jambazi?
 
Mkurugenzi wa kituo hicho cha sunrise ndiye aliyefanya mahojiano na mh. g lema (Mb), siku hiyo lema alieleza mambo Mengi pamoja na kuhusu kukamatwa kwake kila mara. nakumbuka mh lema alizungumzia kuhusu mgogoro wa umeya, napia rc anataka kukuza mgogoro badala ya kutatua, hapo ndipo alipotumia neno mjinga. mwandishi alimuomba mh lema afute usemi wake huo wa kumwita rc mjinga!! mh lema akasema "rangi nyekundu acha iitwe nyekundu na nyeusi iitwe nyeusi". maoni yangu, mwandishi hakuwa na shida ila rc amtafute lema apambane naye kuliko kuongeza idadi ya maadui.

"Jambo la msingi ni hicho kituo cha redio kitueleze wazi wazi mahojiano yao" Wakuu muelewe kwamba RC wapya walioteuliwa na JK wamepewa special deal ya kupambana na CHADEMA na kuvunja nguvu ya mzee wa Richmond kwa hiyo ni lazima huyo RC wa Arusha apambane vilivyo ili kulipa fadhila. Arusha kuweni macho.
 
Back
Top Bottom