Ray Kigosi awatolea povu watanzania, kisa unafiki wao

halafu wewe ray mambo yakujiita the greatest uache!!
we ujiite the greatest kwa muvi gani hasa? au huko kusema neno pumbaaavuu kila movi.
kama wewe the greatest sasa akina denzel au kiefer sutherland a.k.a jack buer wajiitaje? maana hawa muvi zao zapendwa dunia nzima wakati ww hata hapo Uganda Hawakutambui
Eti kisa kila muvi anapojifanya kachukia akigeuziwa kibao mara moja kachuchumaa kuomba msamaha...
 
ray piga kazi acha kulia lia mkubwa
kanumba alikua ngwiji kwenye hii industry
nyie mnauza tu surabna kuanza kuponda ila hamna lolote ,mnasikitisha sana hamuwezi kujisimamia na kujiamin mmebaki kulialia tu na kufuata upepo
Jibu hoja
 
Mbona huelewi wewe... bongo movie ipi unaiongelea ????!!!!

Pamoja na povu lote mnalotoa lakini ukweli utabaki pale pale...

KANUMBA AMEONDOKA NA BONGO MOVIE YAKE...
Hakuna ukweli wowote kanumba hakucheza movie peke yake
 
Kwa sasa hakuna kitu tusiwe tunapindisha maneno, sio wote ambao hatukumuunga mkono Kanumba wale wachache waliosema ivo ndio amewajumuisha ila kiukweli Kanumba alikuwa bora sana tena sana
Mbona na yeye aliiga movie za kinigeria kwa mfano dangerous desire n.k
 
Kupitia ukurasa wake wa Instagram Ray ametoa ujumbe ambao unalenga kutoa uelewa kwa mashabiki hasa wa filamu na muziki nchini ambao wamekuwa wakiponda juhudi za mastaa wa Kitanzania Huku akitolea mfano wa Kanumba na Diamond platnumz

Ray Kigosi ameandika…
1. Kanumba alipoanza kuona mwanga wa kufanikiwa bila kujali juhudi zake kuna watu walimuita Freemanson, Mara anatumia nguvu za Giza. that is to say films zake hazikuwa nzuri but ziliuza sababu ya nguvu za Freemanson na nguvu za giza!!

2. Kanumba alipoenda Big Brother alipondwa Sana na kuitwa bogus kwa Madai hajui kiingereza, Ni watanzania Hawa Hawa walibebea bango hili huku baadhi ya waandishi uchwara wakieneza ujinga huu bila kujali juhudi zake. But Leo wanamsifia hakuna Kama Kanumba!

3. Kuna wakati Kanumba alionekana wazi kuvunjwa moyo na kukatishwa tamaa kwa
kuonekana juhudi zake si kitu. But Alisema maneno machache Kuwa mtanikumbuka kama si Leo basi Ni Kesho.And alichosema kimetimia, wale wale waliokuwa wakisema Ni Freemanson bila hata kujali juhudi zake kwenye game Leo ndio kwa unafiki wanasema hakuna Kama Kanumba !HAO NDIO BINADAMU NA TABIA ZAO Je, Kanumba kaondoka na Bongo Movie yake ya Freemanson ? Kama wengine mnavyodhani industry Ni Mtu sio system !

4. Diamond Platnumz nae baada ya kuona Njia ya mafanikio kuna watanzania, wasanii wenzake na hata baadhi ya wanahabari wanasema Ni Freemanson, wengine
wanaonyesha chuki ya wazi kwake. Wanasema Hana muziki mzuri, Mara Ni Kiki tu ambazo hata Kanumba alikuwa akiripotiwa magazetini na kina Wema.Hawaoni juhudi na thamani ya Diamond sasa ! Hatuombi baya limpate Diamond ili kudhibitisha tabia na unafiki wa binadamu. But HAO NDIO BINADAMU siku zote hawana Jema unafiki ni sehemu ya Maisha.

5. Kila siku Ni kuzua hii na kile, Mara ooh Diamond Ni mchawi, kasema mleteni huyo mganga wangu mkashindwa kumleta, akajitokeza mganga fake sijui na Madai juu Kuwa Diamond atashuka kimuziki kwa sababu ananipuuza niliyempa nyota, Diamond akasema sawa namtegemea Mungu. Miaka 4 sasa tangu yaliyoitwa ya mganga Diamond hashuki ndio anazidi kupaa. HAO NDIO BINADAMU kusema lolote Ni haki Yao.

Kazi za Kanumba sasa zinapewa thamani na ubora uliovuka mipaka na viwango ambao hakupewa kipindi yupo hai ! HAO NDIOBINADAMU na tabia zao. Ni tabia tu ya baadhi ya watu kubebea mabango mabaya ya Mtu au uzushi na kuacha mazuri yake then baadaye wakishikwa Uchawi wanageuza walichoamini Ni nyeusi kiwe nye.
View attachment 501515
View attachment 501518
acha kutafuta huruma , kaza msuri watu wataitikia , shida kubwa nyingine nayoiona kwenu ni KUTEKWA NA WANASIASA. HAPO MNASHINDWA KUJITAMBUA MATOKEO YAKE MNAKERA MASHABIKI WENU HATIMAYE WANAWAKIMBIA. KUWENI NA MSIMAMO SIASA WAACHIENI WENYEWE SIO KUTUMIKA KWA MUDA MFUPI KWA MASLAHI YAO , KISHA WANAAACHIA MADONDA YANAYOCHELEWA KUPONA.
 
Back
Top Bottom