John Haramba
JF-Expert Member
- Feb 4, 2022
- 365
- 1,373
Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) limeamua mchezo wa mwisho wa Hatua ya Makundi wa Kombe la Shirikisho Afrika katika ya wenyeji Simba dhidi ya Union Sportive Gendarmerie Nationale (US Gendarmerie) kuwa utachezwa saa nne usiku.
Hiyo itakuwa ni mara ya kwanza kwa mchezo wa soka ngazi ya labu kuchezwa muda huo katika Uwanja wa Mkapa Jijini Dar es Salaam.
“Ili kutoa nafasi kwa mashabiki wetu wa aina zote kupata muda mzuri wa kuja uwanjani kushangilia timu yao, mchezo wetu wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USGN utakuwa ni saa 4:00 usiku,” Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally.
Ahmed Ally ameongeza kuwa kuhusu suala la usalama kila kitu kipo vizuri na Jeshi la Polisi limeahidi kuwa litaongeza askari wa usalama kwa ajili ya mchezo huo.
Maamuzi ya kuupeleka mchezo huo muda huo ni kwa kuwa wanataka michezo yote ya Kundi D chezwe muda mmoja.
Mchezo mwingine wa kundi hilo ni RS Berkane ya Morocco dhidi ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast ambapo timu zote nne zina nafasi ya kusonga hatua ya Robo Fainali.
Hiyo itakuwa ni mara ya kwanza kwa mchezo wa soka ngazi ya labu kuchezwa muda huo katika Uwanja wa Mkapa Jijini Dar es Salaam.
“Ili kutoa nafasi kwa mashabiki wetu wa aina zote kupata muda mzuri wa kuja uwanjani kushangilia timu yao, mchezo wetu wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya USGN utakuwa ni saa 4:00 usiku,” Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Klabu ya Simba, Ahmed Ally.
Ahmed Ally ameongeza kuwa kuhusu suala la usalama kila kitu kipo vizuri na Jeshi la Polisi limeahidi kuwa litaongeza askari wa usalama kwa ajili ya mchezo huo.
Maamuzi ya kuupeleka mchezo huo muda huo ni kwa kuwa wanataka michezo yote ya Kundi D chezwe muda mmoja.
Mchezo mwingine wa kundi hilo ni RS Berkane ya Morocco dhidi ya ASEC Mimosas ya Ivory Coast ambapo timu zote nne zina nafasi ya kusonga hatua ya Robo Fainali.