Rasimu ya Katiba inayopendekezwa 2014

Rasimu ya Katiba inayopendekezwa 2014

Chenge: uzalendo sio tunu ya taifa kwasababu mtu hazaliwi akiwa mzalendo, uzalendo unatengenezwa tena kwa muda mrefu. Chenge tena: moja ya uzalendo ni lugha ya taifa. My take. hivi mtu anazaliwa akiwa anajua lugha ya taifa, nisaidieni jamani nyie ambao angalau mlimaliza darasa la saba, mi hali yangu mbaya kielimu

Sio tatizo letu wewe kukosa elimu mkuu
 
Nilishawahi kuchangia rasimu ya katiba itapitishwa na tusije shangaa kwa wananchi pia ikapitishwa tena kwa kishindo. Na bado wananchi wakasahau na mambo yakaendelea tu. Swali langu moja tu KWA NINI ITUMIKE PESA NYINGI KWA JAMBO LILOKWISHA PANGWA HALI YA KUWA WANANCHI WENGI WAPO HALI MBAYA. SIDHANI KWA MUNGU LITAPITA HIVI HIVI. NAOGOPA AMANI SIKU MOJA IKAPOTEA NCHI HII. NI WAZO LANGU TU.
 
Wadau nimepitia Rasimu iliyowasilishwa kwa Mwenyekiti wa BMK kwa kweli ni kituko. Yaani ni kama ilani ya CCM wamejiandalia na si Katiba. Rais amebaki na Mamlaka yale yale ya kuteua hadi wakuu wa wilaya bila kudhibitishwa na chombo kingine. Kwa kifupi nakala ya rasimu hiyo ipo wadau msome then mje mtuambie kama kweli hii ndo rasimu ya katiba au ilani ya CCM.

Ungetegemea Chenge ajibane na ni fidafi nambari moja??
 
Mfano hai ni swala la tunu za taifa, CHENGE ni fisadi, unategemea atasema nn linapokuja swala kuficha hela nje, wakati yeye ndo alikuwa mtu wa kwanza kuanikwa wazi kuwa anaficha hela nje, ndo likaja swala la VIJISENTI
 
Kabla ya wakoloni kuigawa afrika, kulikuwa na nchi tanganyika? Tanzania ni zao na mawazo na mwelekeo wa watu huru wenye akili timamu. Hiyo tanganyika ni ya wakoloni.
 
Mfano hai ni swala la tunu za taifa, CHENGE ni fisadi, unategemea atasema nn linapokuja swala kuficha hela nje, wakati yeye ndo alikuwa mtu wa kwanza kuanikwa wazi kuwa anaficha hela nje, ndo likaja swala la VIJISENTI

Ni aibu aisee. Yaani kujipa favor hadi inatia simanzi.Suala la ile marufuku ya kufungua akaunti nje wameliondoa kwa kuwa linawabana.
 
Mfano hai ni swala la tunu za taifa, CHENGE ni fisadi, unategemea atasema nn linapokuja swala kuficha hela nje, wakati yeye ndo alikuwa mtu wa kwanza kuanikwa wazi kuwa anaficha hela nje, ndo likaja swala la VIJISENTI
Kumwamini mwizi ni pagumu hapo!!
 
sio habari mpya.haikutarajiwa kufanyika kazi yoyote ya maana chini ya uongozi wa ki.go.i.go.i wa sitta.ni laana kwa taifa kuwa na mtu kama sitta.
 
Mkuu tanganyika ipo njiani inakuja bado muda tu
 
Wadau nimepitia Rasimu iliyowasilishwa kwa Mwenyekiti wa BMK kwa kweli ni kituko. Yaani ni kama ilani ya CCM wamejiandalia na si Katiba. Rais amebaki na Mamlaka yale yale ya kuteua hadi wakuu wa wilaya bila kudhibitishwa na chombo kingine. Kwa kifupi nakala ya rasimu hiyo ipo wadau msome then mje mtuambie kama kweli hii ndo rasimu ya katiba au ilani ya CCM.
Mkuu kama unaweza kuibandika hapa iweke ili na sisi tupate pa kuanzia.kumsikiliza Chenge mi siwezi kabisa na si kuthubutu.
 
Kyenju, ndiyo maana tunapaswa kwenda mbali ili nchi hii iwe moja kwa kuwa na serikali moja. Kwame alishaliona hilo siku nyingi sana. Atabaki kuwa sahihi.
 
Si nia yangu ya kuzungumzia tabia binafsi ya mtu, lakini linapokuja suala kubwa na la kitaifa kama hili la kuandika Sheria Mama ya Nchi, hivi ndiyo CCM ilikosa mtu mwenye mikono misafi ya kutuandikia Katiba Mpya? Nimeipitia katiba yake mpaka nimeona aibu kama mtanzania kwa sababu imeandikwa huku mtu akijitazama dhamira yake na kuweka vitu ambavyo havita mgusa kwa sababu tayari amesha "chafuka mikono"!

Kama Taifa tujitazame, hivi Chenge anaweza kutuandikia Katiba ya Nchi....Kweli? HAPANA tumepotea! Vifungu vingi vinamuajibisha moja kwa moja mwananchi na inaelekeza sheria nyingine zitatungwa kumuwajibisha mwananchi. Haitofautiani na Katiba hii ya sasa, ambayo madaraka aliyopewa mwananchi ni kupiga kura kumchagua kiongozi kisha akae mita 200, asisogelee hata sanduku la kura mpaka baada ya miaka mitano!

Katiba ya Sitta na mwandishi wake Chenge, inatoa madaraka makubwa kwa viongozi na watendaji wa umma na wasiwajibishwe moja kwa moja na wananchi kwa mujibu wa katiba hii. Kama mwananchi tumenyimwa nguvu ya kikatiba ya kumuwajibisha kiongozi au mtumishi wa umma, basi wananchi tutaendelea na tabia ya "KULALAMIKA" kama awali, kwa maana hatuna nguvu ya kikatiba ya kutenda! Na tukisema "tutende", virungu, maji ya kuwasha na risasi zitatuangukia.

Hii ni Katiba iliyoandikwa na Viongozi kwa wananchi na si Katiba iliyotungwa toka maoni ya wananchi kwa viongozi. Tumerudi miaka 50 nyuma!
Mkuu hii iliyopitishwa ni Rasimu, sio Katiba!
 
Back
Top Bottom