Inasemekana chaguo la Ben plus Mangula lilikuwa Dr. Salim, wazushi wa mambo wanadokeza kwamba Mzee Salim hakuwa na mpango wa kugombea Urais, bali aliombwa na mzee Ben plus Mangula afanye hivyo.
Habari zisizo rasmi zinazidi kudai kuwa, Mangula alipoona JK anabeba umaarufu sana alitaka kumnyima form ya upresidaa, Mzee Mwinyi ndiye aliyewaomba akina Ben na Mangula wampe form JK ili wananchi ndo waamua hatma yake. Na hiyo ndiyo sababu kubwa ya kwanini JK anambeba sana Mzee Mwinyi, na pia hiyo ndiyo sababu kubwa ya JK kumtosa Mangula.
Mtu mwenye akili japo ya darasa la saba tu asingefikiria kabisa kwamba Mangula aachwe kabisa asipewa hata kanafasi kadogo, kwa kazi kubwa aliyoifanya. Halafu you can just imagine, unamtoa Mangula unamuweka Makamba, hata mtoto mdogo hawezi kufanya hivyo.
Wakuu Katika sakata hilo Samuel Malechela alifokewa na kingunge kama mtoto mdogo kwani kamati kuu ilikuwa imemshitukia mkulu wa sasa.Japokuwa alikuwa amepenya na kupata fomu.Kingunge anabebwa na mkuu kwa ajili hiyo lugha ya kebehi aliyoitumia kumfokea malechela sitaki kuiweka hapa itawachefueni, ndo kwa maana alipewa zawadi ya uwaziri wa kuteuliwa pamoja na Thomas Apson Mwang'onda kwa ajili ya kumshukuru baba yake ambaye kwa sehemu fulani alisfanikisha kumweka mkuu madarakani.