Hapo ni sawa na viwanja viwili vya mita 19 kwa 25, na mita 19 kwa 20
Ili usiharibu eneo lako, nyumba usiiweke kati kati ya kiwanja. Chagua eneo moja wapo kati ya hilo la 19x25 au la 19x20 ili eneo lingine ufanyie mambo mengine (kama kujenga nyumba za kupangisha, kufugia n.k)
Mbali na hivyo, pia hutakiwi kuiweka kati kati katika hicho kiwanja utakachochagua kwa kuwa nafasi itakayobaki kushoto/kulia na nyuma/mbele utakuwa umeigawa mara mbili.
Mfano katika mita 19, ukitoa mita 8 ya nyumba inabaki mita 11 kwahivyo unaweza ukaacha nafasi ndogo ya njia ubavu mmoja ili ubaki na nafasi kubwa ubavu mwingine. Unaweza ukaacha mita 2 ubavu mmoja, ukabaki na mita 9 ubavu mwingine ambapo utaweza tena kuweka jengo lingine kama vile jiko la nje, mnara wa tank la maji/store n.k
Ukija upande wa mbele/nyuma, ukichukua mita 25 ukatoa mita 8 ya nyumba unabaki na mita 17 ambapo unaweza ukaacha mita 10 mbele kwa ajili ya parking na nyuma ukaacha mita 7 kwa ajili ya nafasi ya makaro ya choo. Kumbuka karo la choo linatakiwa liwe mbali kidogo na nyumba na pia liwe mbali na ukuta wa fence. Usije ukaacha mita 1 kati ya karo na nyumba, mana karo likishuka kidogo tu nyumba nayo itapata lift kutokana na kutikisika kwa msingi [emoji846]