Ukienda kununua kiwanja, tafuta kiwanja ambacho marefu na mapana yake yanawiana kiasi flani mfano 20m x 25m, 30m x 30m n.k (kiwanja kisiwe chembamba mfano 10m x 20m n.k)
Maeneo mawili yanaweza kufanana square meters lakini yakatofautiana mzunguko (circumference). Sasa eneo zuri katika hayo mawili ni lile ambalo linakuwa na mzingo mdogo
Mfano
Kiwanja "A" (20m x 30m)
Eneo= 20m x 30m = 600m²
Mzingo = (20m + 30m)×2 = 100m
Kiwanja "B" (40m x 15m)
Eneo = 40m x 15m = 600m²
Mzingo = (40m + 15m)×2 = 110m
Kiwanja "A" kina mzingo wa mita 100, wakati kiwanja "B" kina mzingo wa mita 110 kwa hivyo kama ungekuta hivi viwanja ndio vimebaki huko site, basi kiwanja kizuri ni kiwanja "A", pia hata ukijenga uzio (fence), kiwanja "A" kitatumia tofali chache kulinganisha na kiwanja "B" lisha ya vyote kuwa na SQM zinazofanana
Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane