Rais wangu mpendwa nisaidie nataabika

Rais wangu mpendwa nisaidie nataabika

Inanda

Member
Joined
Dec 6, 2020
Posts
62
Reaction score
128
Mheshimiwa rais kwanza nikupongeze kwa kuchaguliwa kuongoza kwa muhula mwingine. Nakuombea kwa Mwenyezi Mungu akulinde, akupe hekima kama jinsi mfalme Selemani alivyoomba hekima, ili taifa hili liweze kusonga mbele. Miaka 5 umeiongoza kwa mafanikio makubwa hivyo ni matumaini yangu hii miaka 5 ijayo itakuwa yenye mafanikio zaidi.

Mheshimiwa rais, mimi ni msomi mwenye degree ya uhasibu, pia nina taaluma ya juu ya uhasibu yaani ni Certified Public Accountant (CPA). Ajira imekuwa ngumu sana, nimetafuta kazi kwa muda mrefu bila mafanikio. Umri unazidi kwenda na pia nina familia inayonitegemea.

Nimekuwa nikiendesha maisha yangu kwa tabu sana mpaka najihisi kukata tamaa. Mheshimiwa rais najua wasaidizi wako wanapitia hapa kama sio wewe mwenyewe, natumaini kupitia wao watakufikishia ombi langu, hivyo naomba unikumbuke mtanzania mwenzako. Wewe ni rais wa watanzania wote, maskini na matajiri.

Nakuomba unikumbuke mimi mnyonge ninayehangaika na maisha mheshimiwa Rais.

Natanguliza shukrani zangu za dhati na nakutakia utumishi mwema. Mungu akulinde.
 
Mkuu CPA umelipa ukiw katika ajira? Manake mdogo wako hapa ndo nachanganykiw kabisaaa.. Kam mpaka mtu kama wew amekwama kias hiki
 
Magufuli lengo Lake lilikuwa hili

Kutaabisha na kuhangaisha watu ili wampigie magoti na kulamba viatu ili wapate ajira

Tumefikia huku kweli?

Mtu anaanza hadi kumuomba raisi kazi, kweli?

Raisi anaombwa kazi na graduate???

Huku taasisi husika ambazo zilitakiwa kutengeneza ajira zipo???
 
Mheshimiwa rais kwanza nikupongeze kwa kuchaguliwa kuongoza kwa muhula mwingine. Nakuombea kwa Mwenyezi Mungu akulinde, akupe hekima kama jinsi mfalme Selemani alivyoomba hekima, ili taifa hili liweze kusonga mbele. Miaka 5 umeiongoza kwa mafanikio makubwa hivyo ni matumaini yangu hii miaka 5 ijayo itakuwa yenye mafanikio zaidi...
Pole sana kaka,, nikushauri kitu la bado hujafanya,,peleka CV yako kea Audit firms hata zile ndogo kwa ajili ya internship...CPA waweza pata pa kuanzia
 
Mheshimiwa rais kwanza nikupongeze kwa kuchaguliwa kuongoza kwa muhula mwingine. Nakuombea kwa Mwenyezi Mungu akulinde, akupe hekima kama jinsi mfalme Selemani alivyoomba hekima, ili taifa hili liweze kusonga mbele. Miaka 5 umeiongoza kwa mafanikio makubwa hivyo ni matumaini yangu hii miaka 5 ijayo itakuwa yenye mafanikio zaidi...
Daaah! Sitaki msemea huyo magu lakin yeye ndo katufikisha hapa ila Mungu awe pamoja nawe.

Lakini je una tumiA mtandao wa linkedin?
 
Pole sana kwa nyakati ngumu unazopitia Mungu akufanyie wepesi ufanikishe tamainio la moyo wako..!Naamini kesho yako haitakuwa kama jana🙏🙏🙏🙏🙏
 
Pole mkuu... taratibu utaizoea hiyo hali usihofu maana Binafsi nimekwisha izoea.

Elimu ya maikroskopu na vijidudu vyake imelala kwenye tranka store huko.
 
Mheshimiwa rais kwanza nikupongeze kwa kuchaguliwa kuongoza kwa muhula mwingine. Nakuombea kwa Mwenyezi Mungu akulinde, akupe hekima kama jinsi mfalme Selemani alivyoomba hekima, ili taifa hili liweze kusonga mbele. Miaka 5 umeiongoza kwa mafanikio makubwa hivyo ni matumaini yangu hii miaka 5 ijayo itakuwa yenye mafanikio zaidi....
Akikusaidia Wewe Mmoja hivi huku kuna Kundi Kubwa la Watu wenye Shida kama zako au zaidi yako unadhani atakuwa amelitatua tatizo Kiupana?
 
Km Mtu na degree yake anahaha njaa kali ajira Häkuna.
Hivi hawa ndugu zetu wanaoenda JKT tu kwel ndo watapata ajira!?
 
Huu uchumi Wa Kati mwenzenu hata siuelewi kabisa, Mwenye kuuelewa naomba tafadhali anieleweshe
 
Back
Top Bottom