Utakuwa umeshasikia usemi, "Rome wasn't built fin a day".Baada ya kukamilisha ukusanyaji data wilayani Igunga baada ya Nzega na Sikonge mkoani Tabora juu ya hali ya elimu nchini na huduma za afya, nimejiuliza maswali mengi sana.
Hivi Rais wangu anasema atatembea na masikini, hivi masikini wapi??
Katika shule moja, unakuta walimu wanne wanafunzi mianane, shule zingine walimu watatu wanafunzi mia sita, hao watoto wanasomaje???
Tar 01/09/16 nilitembelea shule ya Msingi Mtungulu. Shule hii iko kilomita 22 kutoka Igunga mjini. Nilikuta walimu watano (05) huku wanne wakiwa kazini mwingine akiwa na matatizo.
Idadi ya wanafunzi shuleni hapo ni zaidi ya 600. Masomo ya yanayondishwa ni kama vile Historia, Uraia, Kiswahili, Kiingereza, Haiba na michezo, Hisabati, Jiografia, Tehama nk.
Madarasa ni kuanzia la kwanza mpaka la saba. Kwa masomo hayo hapo juu walimu watafundishaje???
Maana yake ni kwamba ni kwamba, vipindi vingi havifundishwi. Watoto wengi wanakwenda kuzurura shuleni.
Nilipofanya utafiti juu ya hali ya uwezo wa watoto, bado tatizo la kutokujua kusoma na kuandika ni kubwa sana. Sasa, kama tunashindwa kupeleka walimu kusaidia watoto hao wa masikini, hao masikini tutawasaidiaje????
Kuna msaada kwa masikini zaidi ya elimu na Afya???
Tuweke kando siasa za watumishi hewa, tusaidie Taifa hili. [HASHTAG]#Ajiri[/HASHTAG] walimu
mkuu naona umeona ni bora uimbe pambio, usijali Mungu yupo kazini utamwonatu ndugu vuta subra.Baba Mungu kwa nini wasimama mbali nyakati za shida za watanzania kama hizi
Maendeleo hayaji kama mlipuko wa bomu..it is a step wise thing..kwani ww uliiahid familia yako nn kwamba ukipata kaz utawafanyia..mpaka leo umefanya vingap?
Mungu akamwambia Musa "kwa nini kunililia mimi? waambie wana wa Israel wasonge mbele"Baba Mungu kwa nini wasimama mbali nyakati za shida za watanzania kama hizi
tumsaidie kuajiri walimu au? maana sijui la kumsaidia coz he seems to know everythingEmbu jitengeni na siasa tumsaidie huyu mkuu kuinua taifa letu sio lake peke yake.
Kwani wewe kwa miezi kumi ulitaka awe ameisha fanya nini???, nipe tu mfano.
Hivi kuhamia dodoma ni tsh ngapi??? Na ni miaka mingapi???Mkuu ni kweli tunatakiwa kumsaidia Rais..na tunamsaidia kwa kulipa kodi za PAYE, kodi kwenye mafuta na bidhaa zingine, na hata tulipowekea VAT kinyemela kwenye miamala ya fedha hatujaandamana. Ebu jiulize Kiongozi mwenye kujielewa angeanza kushugulikia matatizo ya elimu na walimu pamoja na afya, au angekurupuka na safari ya Dodoma ambayo imeteka akili/mawazo/resources za wizara zote kwa sasa. Tatizo ni kukosa vipaumbele na hata alipoweka kipaumbele cha serikali yake kuwa ni Tanzania ya viwanda.....akaibuka na safari ya Dom from nowhere.
Hivi kuhamia dodoma ni tsh ngapi??? Na ni miaka mingapi???
Kufufua viwanda/kuanzisha viwanda ni shilingi ngapi na ni miaka mingapi???
Na kuboresha elimu ni shilingi ngapi??? Na ni miaka mingapi???
Nilichogundua kumbe tulijiandaa kupinga na kubisha.
Mwisho mtataka uchumi uwe sawa na marekani kwa muda alioingia.
Kwani mkuu wewe unajua kwanini watu wameamua wahamie dodoma.Kama una safari ya kwenda Mwanza ukapanda basi kuanza safari yako, kufika Mlandizi ukashuka ukapanda basi la kwenda Tunduma.....ni either hujui uendako au akili hazijakaa vizuri, haijalishi unatumia miaka mingapi kwenda Tunduma. Simpo logic
Kwani mkuu wewe unajua kwanini watu wameamua wahamie dodoma.
Iwe najua au sijui sio hoja hapa, hoja ni lack of vipaumbele. Kwani kwenda Dom ilikuwa kipaumbele kabla ya elimu/afya na Tz ya viwanda? Au kwenda Dodoma kuna accelerate kuanzishwa kwa viwanda? au kuna rahisisha maboresho ya elimu?
Mkuu ni kweli tunatakiwa kumsaidia Rais..na tunamsaidia kwa kulipa kodi za PAYE, kodi kwenye mafuta na bidhaa zingine, na hata tulipowekea VAT kinyemela kwenye miamala ya fedha hatujaandamana. Ebu jiulize Kiongozi mwenye kujielewa angeanza kushugulikia matatizo ya elimu na walimu pamoja na afya, au angekurupuka na safari ya Dodoma ambayo imeteka akili/mawazo/resources za wizara zote kwa sasa. Tatizo ni kukosa vipaumbele na hata alipoweka kipaumbele cha serikali yake kuwa ni Tanzania ya viwanda.....akaibuka na safari ya Dom from nowhere.
Hivi kuhamia dodoma ni tsh ngapi??? Na ni miaka mingapi???
Kufufua viwanda/kuanzisha viwanda ni shilingi ngapi na ni miaka mingapi???
Na kuboresha elimu ni shilingi ngapi??? Na ni miaka mingapi???
Nilichogundua kumbe tulijiandaa kupinga na kubisha.
Mwisho mtataka uchumi uwe sawa na marekani kwa muda alioingia.
Mkuu mimi kwakweli napata hasira sana watu wanavyopinga kila kitu.Tuacheni ubishi. Tujenge Taifa Letu kwa pamoja.