gibishi
Senior Member
- Aug 12, 2016
- 182
- 268
Baada ya kukamilisha ukusanyaji data wilayani Igunga baada ya Nzega na Sikonge mkoani Tabora juu ya hali ya elimu nchini na huduma za afya, nimejiuliza maswali mengi sana.
Hivi Rais wangu anasema atatembea na masikini, hivi masikini wapi??
Katika shule moja, unakuta walimu wanne wanafunzi mianane, shule zingine walimu watatu wanafunzi mia sita, hao watoto wanasomaje???
Tar 01/09/16 nilitembelea shule ya Msingi Mtungulu. Shule hii iko kilomita 22 kutoka Igunga mjini. Nilikuta walimu watano (05) huku wanne wakiwa kazini mwingine akiwa na matatizo.
Idadi ya wanafunzi shuleni hapo ni zaidi ya 600. Masomo ya yanayondishwa ni kama vile Historia, Uraia, Kiswahili, Kiingereza, Haiba na michezo, Hisabati, Jiografia, Tehama nk.
Madarasa ni kuanzia la kwanza mpaka la saba. Kwa masomo hayo hapo juu walimu watafundishaje???
Maana yake ni kwamba ni kwamba, vipindi vingi havifundishwi. Watoto wengi wanakwenda kuzurura shuleni.
Nilipofanya utafiti juu ya hali ya uwezo wa watoto, bado tatizo la kutokujua kusoma na kuandika ni kubwa sana. Sasa, kama tunashindwa kupeleka walimu kusaidia watoto hao wa masikini, hao masikini tutawasaidiaje????
Kuna msaada kwa masikini zaidi ya elimu na Afya???
Tuweke kando siasa za watumishi hewa, tusaidie Taifa hili. [HASHTAG]#Ajiri[/HASHTAG] walimu
Hivi Rais wangu anasema atatembea na masikini, hivi masikini wapi??
Katika shule moja, unakuta walimu wanne wanafunzi mianane, shule zingine walimu watatu wanafunzi mia sita, hao watoto wanasomaje???
Tar 01/09/16 nilitembelea shule ya Msingi Mtungulu. Shule hii iko kilomita 22 kutoka Igunga mjini. Nilikuta walimu watano (05) huku wanne wakiwa kazini mwingine akiwa na matatizo.
Idadi ya wanafunzi shuleni hapo ni zaidi ya 600. Masomo ya yanayondishwa ni kama vile Historia, Uraia, Kiswahili, Kiingereza, Haiba na michezo, Hisabati, Jiografia, Tehama nk.
Madarasa ni kuanzia la kwanza mpaka la saba. Kwa masomo hayo hapo juu walimu watafundishaje???
Maana yake ni kwamba ni kwamba, vipindi vingi havifundishwi. Watoto wengi wanakwenda kuzurura shuleni.
Nilipofanya utafiti juu ya hali ya uwezo wa watoto, bado tatizo la kutokujua kusoma na kuandika ni kubwa sana. Sasa, kama tunashindwa kupeleka walimu kusaidia watoto hao wa masikini, hao masikini tutawasaidiaje????
Kuna msaada kwa masikini zaidi ya elimu na Afya???
Tuweke kando siasa za watumishi hewa, tusaidie Taifa hili. [HASHTAG]#Ajiri[/HASHTAG] walimu