Rais wangu Magufuli, uko kwa ajili ya masikini wapi?

Rais wangu Magufuli, uko kwa ajili ya masikini wapi?

Embu jitengeni na siasa tumsaidie huyu mkuu kuinua taifa letu sio lake peke yake.

Kwani wewe kwa miezi kumi ulitaka awe ameisha fanya nini???, nipe tu mfano.
Aajiri walimu, tangu atangaze elimu bure, hata walimu waliokuwa wanajitolea katika shule hizo kwa msaada wa wazazi hawapo tena..

Apeleke walimu, apeleke madaktari huko vijijini.
 
Kuna shule iko Katoro Geita, ina wanafunzi 10,000.ukiwakuta nje mfano wakati wa mapumziko utadhani michezo ya umitashumta unafanyika hapo.
Ila sijui idadi ya walimu na mahitaji mengine.siku nikirudi tena huko nitaulizia
Hiyo shule ina matundu 8 ya vyoo vyumba vya madarasa kama 10 hivi watoto wanasoma chini ya mti kuna watu wamejitolea madawati lakini hata haijasaidia Mpaka walimu wanaofundisha hapo utawaonea huruma asee
 
Mtu anajenga Uwanja wa ndege Chato kama kipaombele chake unategemea nini
 
Hata yeye anajua kuwa anachosema sio anachofanya
Baada ya kukamilisha ukusanyaji data wilayani Igunga baada ya Nzega na Sikonge mkoani Tabora juu ya hali ya elimu nchini na huduma za afya, nimejiuliza maswali mengi sana.

Hivi Rais wangu anasema atatembea na masikini, hivi masikini wapi??

Katika shule moja, unakuta walimu wanne wanafunzi mianane, shule zingine walimu watatu wanafunzi mia sita, hao watoto wanasomaje???

Tar 01/09/16 nilitembelea shule ya Msingi Mtungulu. Shule hii iko kilomita 22 kutoka Igunga mjini. Nilikuta walimu watano (05) huku wanne wakiwa kazini mwingine akiwa na matatizo.

Idadi ya wanafunzi shuleni hapo ni zaidi ya 600. Masomo ya yanayondishwa ni kama vile Historia, Uraia, Kiswahili, Kiingereza, Haiba na michezo, Hisabati, Jiografia, Tehama nk.

Madarasa ni kuanzia la kwanza mpaka la saba. Kwa masomo hayo hapo juu walimu watafundishaje???

Maana yake ni kwamba ni kwamba, vipindi vingi havifundishwi. Watoto wengi wanakwenda kuzurura shuleni.

Nilipofanya utafiti juu ya hali ya uwezo wa watoto, bado tatizo la kutokujua kusoma na kuandika ni kubwa sana. Sasa, kama tunashindwa kupeleka walimu kusaidia watoto hao wa masikini, hao masikini tutawasaidiaje????

Kuna msaada kwa masikini zaidi ya elimu na Afya???

Tuweke kando siasa za watumishi hewa, tusaidie Taifa hili. [HASHTAG]#Ajiri[/HASHTAG] walimu
Hakuna kitu kibaya kuyatilia maanani maneno ya utani
 
Baada ya kukamilisha ukusanyaji data wilayani Igunga baada ya Nzega na Sikonge mkoani Tabora juu ya hali ya elimu nchini na huduma za afya, nimejiuliza maswali mengi sana.

Hivi Rais wangu anasema atatembea na masikini, hivi masikini wapi??

Katika shule moja, unakuta walimu wanne wanafunzi mianane, shule zingine walimu watatu wanafunzi mia sita, hao watoto wanasomaje???

Tar 01/09/16 nilitembelea shule ya Msingi Mtungulu. Shule hii iko kilomita 22 kutoka Igunga mjini. Nilikuta walimu watano (05) huku wanne wakiwa kazini mwingine akiwa na matatizo.

Idadi ya wanafunzi shuleni hapo ni zaidi ya 600. Masomo ya yanayondishwa ni kama vile Historia, Uraia, Kiswahili, Kiingereza, Haiba na michezo, Hisabati, Jiografia, Tehama nk.

Madarasa ni kuanzia la kwanza mpaka la saba. Kwa masomo hayo hapo juu walimu watafundishaje???

Maana yake ni kwamba ni kwamba, vipindi vingi havifundishwi. Watoto wengi wanakwenda kuzurura shuleni.

Nilipofanya utafiti juu ya hali ya uwezo wa watoto, bado tatizo la kutokujua kusoma na kuandika ni kubwa sana. Sasa, kama tunashindwa kupeleka walimu kusaidia watoto hao wa masikini, hao masikini tutawasaidiaje????

Kuna msaada kwa masikini zaidi ya elimu na Afya???

Tuweke kando siasa za watumishi hewa, tusaidie Taifa hili. [HASHTAG]#Ajiri[/HASHTAG] walimu
Utaitwa "Mchochezi Bure ndugu yangu". Fumba macho tu kwa haya yote unayoyaona.
 
Vipi kwene suala la madawati? kuna ambao bado wanakaa chini?
Kusoma vizuri ukiwa na waalimu wa kutosha huku umekaa chini na kukaa kwenye madawati mazur huku unaenda kuuza sura shule bila walimu lipi bora
 
Ngoja tusubir ajira zifunguliwe maana zimesitishwa kwa mda labda watapelekewa waalimu
 
Mkuu jiandae kwa kesi ya uchochezi. Tumeambiwa tusifie tu, hawataki tuseme ukweli. Ukitaka kufanya press conference lazima wakuhoji kwanza.
 
Embu jitengeni na siasa tumsaidie huyu mkuu kuinua taifa letu sio lake peke yake.

Kwani wewe kwa miezi kumi ulitaka awe ameisha fanya nini???, nipe tu mfano.

Mkuu ni kweli tunatakiwa kumsaidia Rais..na tunamsaidia kwa kulipa kodi za PAYE, kodi kwenye mafuta na bidhaa zingine, na hata tulipowekea VAT kinyemela kwenye miamala ya fedha hatujaandamana. Ebu jiulize Kiongozi mwenye kujielewa angeanza kushugulikia matatizo ya elimu na walimu pamoja na afya, au angekurupuka na safari ya Dodoma ambayo imeteka akili/mawazo/resources za wizara zote kwa sasa. Tatizo ni kukosa vipaumbele na hata alipoweka kipaumbele cha serikali yake kuwa ni Tanzania ya viwanda.....akaibuka na safari ya Dom from nowhere.
 
Elimu bure! Endeleeni "kufyayua watoto"!

Hii nchi ni shiida sana.
 
Dah hiyo Avatar tu nimeshasahau shida zangu zote
 
Back
Top Bottom