Rais wa China aahidi kuzipatia nchi za Afrika chanjo ya COVID-19

Yoyo Zhou

Member
Jun 16, 2020
72
111
688806987.jpg


Rais Xi Jinping wa China ametoa hotuba kwenye mkutano maalumu wa kilele kuhusu mshikamano na ushirikiano kati ya China na Afrika katika kupambana na COVID-19.

Ameahidi kuwa mara chanjo ya COVID-19 inayotengenezwa na China itakapokamilika na kuthibitishwa, nchi za Afrika zitakuwa kati ya nchi za mwanzo kufaidika.

Pia ameongeza kuwa Ili kupunguza athari za COVID-19, ni muhimu kuongeza ushirikiano wa Ukanda Mmoja na Njia Moja, na kuongeza kasi ya ufuatiliaji wa matokeo ya mkutano wa FOCAC wa Beijing.

Kipaumbele kikubwa kinatakiwa kutolewa kwa ushirikiano katika afya ya umma, kufungua tena uchumi, na maisha ya watu.
 

Attachments

  • 688806987.jpg
    688806987.jpg
    37.1 KB · Views: 1
Mkuu wa nchi alishasema vitu vya msaada kwa suala la Corona ni kuwa navyo makini Sana! Kuna agenda ya siri inataka kupitishwa kupitia Corona. Sisi nyungu inatosha! Hatuhitaji chanjo!!
 
Mkuu wa nchi alishasema vitu vya msaada kwa suala la Corona ni kuwa navyo makini Sana! Kuna agenda ya siri inataka kupitishwa kupitia Corona. Sisi nyungu inatosha! Hatuhitaji chanjo!!
Usiseme "hatutaki" sema "sitaki"! Huyo una rais wako (kama akirudi) ndiye atakua wa kwanza kupokea huo msaada.
 
Usiseme "hatutaki" sema "sitaki"! Huyo una rais wako (kama akirudi) ndiye atakua wa kwanza kupokea huo msaada.
Na mimi ni mmoja wapo sitaki misaada ya Mabeberu, Rais wangu yupo na lini aliondoka?
usikubali msaada ya nje kwani Corona imeivamia tena China wakati kwetu popo tunapambana nao
wapeleke Uganda, Kenya, Zambia sisi haituhusu
 
Back
Top Bottom