My Son drink water

JF-Expert Member
Nov 30, 2016
4,932
13,283
Rais wangu na mama yangu Samia, kwanza nakupongeza sana kwa hatua uliyochukua ya kuanza kuboresha mahusiano ya kidiplomasia na Kenya kwa sababu yalianza kufa kimya kimya, yaani Tulikuwa na uhusiano wa kinafiki, ktk hili sina muda wa kulieleza kwa kina kwa sababu lipo wazi kabisa.

Rais wangu, Tasnia ya mahusiano ya Taifa na Taifa inahitaji akili nyingi sana, kwa sababu ktk slogan ya kijasusi kila Taifa la jirani yako ni adui yako, kwa maana ya kwamba linaweza hata kutumika kukupiga na adui wa mbali.

Hii ina maana ya kwamba, tunakuwa majirani na ndugu tusioaminiana kwa kila kitu.

Ktk vinywa vyetu sisi ni marafiki wa kufa na kuzikana, ila ktk uhalisia sisi ni adui.

Rais wangu, Kenyatta ni Rais mwenye akili mno na mwingi wa hekima, kwa nje utamwona kawaida, lakini Kenyatta ni bonge la Intelligent.

Rais wangu, hakuna anayeweza kukueleza ukweli, kwa sababu Chama chenu kina slogan ya kusifia kila kitu, hiyo imefanya hadi idara ya usalama wa Taifa TISS kuwa dhaifu kupindukia.

Rais wangu, hivi unajua kuwa, Kenya kwa miongo mingi mno iliyopita imekuwa ikiitamani sana ardhi ya Tanzania? Unaposema kuwa unawakaribisha Wakenya wawekeze kwenye madini, maana yake ni kwamba unawapa mwanya wa kumiliki ardhi ya Tanzania ili watimize ndoto zao, ktk hili hapana, waite Wa Australia,Wamarekani, Waingereza, Wacanada, lakini siyo Kenya ktk sekta ya madini.

Wakenya na Wachina hawana Tofauti, mimi nimeolea kenya,mke wangu ni mkikuyu, Tulikutana Australia, na wala hajui kuwa jina langu fake ni My Son drink water nawajua vizuri sana hawa watu, hawana Tofauti na Watusi, ukweli unauma ila hauna budi kusemwa.

Rais wangu, ziara yako Kenya ilikuwa ni ya manufaa ya Kenya na si Tanzania, Kenyatta alikuwa ameshafanya calculation nzuri sana, kitaalamu inaitwa,"Pretend that you need them more, while your intention is to suck their Blood".

Sikatai kwamba Wakenya wasiwekeze Tanzania, ila hawa watu ni wajanja kama nyoka.

Message sent and Delivered
 
Nimeandika Uzi humu ndani watu wakatoka mapovu.

Yaani Matatizo waliyotaka wenyewe waje kusaidiwa huku, nilishangaa Rais aliposema Tanzania ina Ardhi anawakaribisha Wakenya, Akanichosha aliposema Tanzania ina madini wakenya waje, utadhani watu hatuijui Kenya.

Hivi Wakenya wangapi watakuja Tanzania kuwekeza Madini Tanzania tusiwaite wachimbaji wadogowadogo,
 
Nimeandika Uzi humu ndani watu wakatoka mapovu.

Yaani Matatizo waliyotaka wenyewe waje kusaidiwa huku, nilishangaa Rais aliposema Tanzania ina Ardhi anawakaribisha Wakenya, Akanichosha aliposema Tanzania ina madini wakenya waje, utadhani watu hatuijui Kenya.

Hivi Wakenya wangapi watakuja Tanzania kuwekeza Madini Tanzania tusiwaite wachimbaji wadogowadogo,
Mkuu, kenya ni Hatari sana, yaani hatutakubali eti waje washike vitalu vya madini, yaani hawa tukiwaruhusu Watanzania watabaki maskini wa kutupwa
 
Kubali kuliwa ili ule kama vile Kaaba anavyonunuliwa kwa elf 20 yeye kesho akapata mlo.

Wewe lala ndani Mimi nitoke tuone nani atarudi na chochote jion

Business is all about risk.
Mzee Marekani ni Richest Country Duniani lakini hawatakagi ujinga na ushirika wa upande mmoja.

Uingereza ni Taifa kubwa kuliko sisi na Mataifa yote Africa ila ulijitoa EU, muwege mnafikiria miaka 10 hadi 20
 
Nimeandika Uzi humu ndani watu wakatoka mapovu.

Yaani Matatizo waliyotaka wenyewe waje kusaidiwa huku, nilishangaa Rais aliposema Tanzania ina Ardhi anawakaribisha Wakenya, Akanichosha aliposema Tanzania ina madini wakenya waje, utadhani watu hatuijui Kenya.

Hivi Wakenya wangapi watakuja Tanzania kuwekeza Madini Tanzania tusiwaite wachimbaji wadogowadogo,
Iko hivi kwa taarifa yako Wasukuma ndio wanaogoza kuwekeza kwenye migodi ya Kenya au unafikiri Kenya hakuna migodi?

Kuanzia Migori hapo kwenda mpaka kisumu kuna migodi kibao na wakazi wa huko ni wasukuma na wajaluo.

Sasa wewe sijui unataka wawekezaji kutoka wapi ndio waje wawekeze na mchanga wabebe

Hii nchi watu tunashindwa kujua kitu tunachokitaka..

Kwenye swala la uwekezaji na kukuza uchumi niko na mama.

Ila tutagombana kwenye democracy na ufisadi na katiba mpya.
 
Mkuu, kenya ni Hatari sana, yaani hatutakubali eti waje washike vitalu vya madini, yaani hawa tukiwaruhusu Watanzania watabaki maskini wa kutupwa
Nina mashaka na Uwezo wa kuamua wa Rais wangu, au kuna kundi linalonunulika linamshauri, yaani kikubwa ambacho Kenya itaifanyia Tanzania ni kuruhusu Mahindi, alafu sisi tutaruhusu Masuala ya Anga, Utalii.

Wao Wanazuia Shirika letu la ndege kufanya Kazi,ila lao wanataka tulihusu, Eti Mtalii afike Kenya ndio aje Tanzania, Kwa nini asianze Tanzania

Mama alipaswa amuache Kabudi kwenye wizara ya mambo ya nje aisee,
 
Iko hivi kwa taarifa yako Wasukuma ndio wanaogoza kuwekeza kwenye migodi ya Kenya au unafikiri Kenya hakuna migodi?

Kuanzia Migori hapo kwenda mpaka kisumu kuna migodi kibao na wakazi wa huko ni wasukuma na wajaluo.

Sasa wewe sijui unataka wawekezaji kutoka wapi ndio waje wawekeze na mchanga wabebe

Hii nchi watu tunashindwa kujua kitu tunachokitaka..

Kwenye swala la uwekezaji na kukuza uchumi niko na mama.

Ila tutagombana kwenye democracy na ufisadi na katiba mpya.
Hao ni wachimbaji wadogo wadogo...
 
Mzee Marekani ni Richest Country Duniani lakini hawatakagi ujinga na ushirika wa upande mmoja.

Uingereza ni Taifa kubwa kuliko sisi na Mataifa yote Africa ila ulijitoa EU, muwege mnafikiria miaka 10 hadi 20
Marekani yenyewe unayoisema ndio inaongoza kuwa na wafanyakazi wa kigeni kuliko nchi zote duniani

Ndio nchi inayoongoza kununua bidhaa toka China kuliko nchi zote za America.

We jamaa vipi wewe uwekezaji gani unautaka?
 
Nina mashaka na Uwezo wa kuamua wa Rais wangu, au kuna kundi linalonunulika linamshauri, yaani kikubwa ambacho Kenya itaifanyia Tanzania ni kuruhusu Mahindi, alafu sisi tutaruhusu Masuala ya Anga, Utalii.

Wao Wanazuia Shirika letu la ndege kufanya Kazi,ila lao wanataka tulihusu, Eti Mtalii afike Kenya ndio aje Tanzania, Kwa nini asianze Tanzania

Mama alipaswa amuache Kabudi kwenye wizara ya mambo ya nje aisee,
Tatizo ni TISS
 
Inaonekana hawajui wakenya vizuri. Mfumo wao licha ya kuwa wa kikabila, ni wa kibinafsi mno. Wachunguzeni ambao unawajua wanaoishi Tanzania. Wengi ambao nimekuwa na mawasiliano na mahusiano nao, mara nyingi huwa wanaongelea ujinga na upumbavu uitwao ukabila hata kama wana elimu ya juu kiasi gani.

Wanaishi na kuwaza kikabila. Ni wabinafsi na walafi. Kama tunahitaji watu wa kushirikiana nao nadhani waganda, wazambia na hata wacongo, wamalawi, wanafaa kuliko hawa waliobaki kwenye jumuia yetu ya afrika mashariki.
 
Back
Top Bottom