Rais Samia: Ukiingia kwenye mitandao ya kijamii kuna uzandiki mwingi sana

Nigrastratatract nerve

JF-Expert Member
Sep 4, 2019
1,395
3,901
"Ukiingia kwenye mitandao ya kijamii kuna uzandiki mwingi sana, kila mtu anazusha lake, naomba sana viongozi wa dini mlikemee hili na mengine yote yanayoenda kinyume na maadili na miiko yetu.

uzandiki: hali ya unafiki, udaku, umbeya, uongo.

Wanafiki mama anawaonya acheni unafiki
Wambeya mama amewaonya waache umbea
Waongo akina Mbowe na kundi lake mama kawaonya acheni umbea
 
Lakini Mbowe unamwonea.Kwanza Hakutajwa na Her excellency Madam President ,Pili yeye Kiongozi wa chama cha siasa(Upinzani), (CHADEMA), (Opposition party) lazima aendane tofauti na sera za Mh Rais ambaye anatoka CCM.

Ni kawaida duniani kote. Hiyo ndio maana ya Demokrasia.Lakini kunapokuja suala la utaifa kama vile Vita n.k Mwenyezi Mungu Atuepushe wote wanasimama pamoja na kuzika tofauti zao.
 
kaz kwel kwel
FB_IMG_1618614563254.jpg
 
Hata mimi nashangaa mradi ambao hata kichaa asingeruhusu ujengwe. Je ina maana Magufuli alikuwa amezungukwa na vichaa wengi kipindi hiki wanaojitokeza sasa hivi au wanataka kumfanya mwendazake kichaa? Hapa kuna tatizo tena kubwa tu. Ila tujue wote tutakufa mkumbuke jamani.
 
Sasa wewe umemuona wapi/lini mbowe kwenye mitandao ya kijamii

Chuki yako dhidi ya mbowe ni kubwa mno
 
Mamii taratibu khe
Usitukane wakunga na uzazi ungalipo
Usitukane mamba kabla hujavuka mto
Mtandaoni kunasaidia kunaumiza kunajenga na kubomoa zaidi kuna mengi ya kujifunza ya kukuepusha na mengi na kujirekebisha
Sio kila ukosoaji ni mbaya....
Pole pole ndio mwendo
.....tazama mbele na nyuma........
 
Hata wewe ni mzandiki kwanini hoja yako uilete kwenye mitandao ya kijamii, ungepeleka sehemu unayofikiri ni sahihi
 
Hapa Mama amekosea huku kwenye mitandao ndio bunge la wananchi tena ingefaa atuongezee bajeti ya bando.
 
Wale waliokuwa wanajipa moyo ooh mama anachukua ushauri wa mitandaoni wamefungwa midomo vibaya, kumbe anachokiona huku 98% ni umbea tu.
 
Back
Top Bottom