Rais Samia tuondole DC Mtanda Arusha

Rais Samia tuondole DC Mtanda Arusha

Hivi karibuni kulifanyika mkutano kati ya wadau mbalimbali ili kutatua hili tatizo. Walikuwepo wenye kumbi za starehe,wakazi wa sehemu hizo wanaolalamika,kamati ya mazingira ikiongozwa na madiwani na Mkuu wa Wilaya Mheshimiwa Mtanda.
Walikubaliana kwamba wenye kumbi wachukue hatua za kupunguza kelele katika sehemu hizo ili wakazi waweze kulala bila kubughudhiwa na kelele za muziki baada ya saa sita usiku.
Mojawapo ya maazimio ni kuweka sound proof system na pia kuomba leseni ya Night Club ambayo ina vigezo vyake.
Kila moja akitimiza wajibu wake hili sio tatizo kubwa.Tatizo ni pale wenye kumbi wanapokataa kwa makusudi au kutojali kufuata makubaliano.
Mkuu wa Wilaya ni mchapa kazi hivyo majungu hayawezi kusaidia kwenye hili.
Kuwa wa mjini born town haina maana ya kutofuata sheria na kanuni tulizojiwekea.
 
Enforcement unamfanyia anayekulipa mshahara!
Amemkuwa mhalifu?
Kwamba akiuke wajibu wake na ababelekezwe? Pumbavu kabisa!
Kwamba yeye yupo pale kulipa mishahara ya wafanyakazi wa Serikali just for Leisure bila yeye kuwa na wajibu?
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Arusha ni Mkoa wa pili kwa kuingiza mapato baada ya Dar.

Mapato maana yake shughuli za kiuchumi ikiwemo utalii,madini,biashara za mazao mbali mbali ya kilimo hasa mboga mboga na matunda.

Nature ya mji wa Arusha ni starehe Hotel,Pub .......

DC mtanda kaanzisha sokomoko la aina yake anatembea na kikosi cha polisi Bar zote kuanzia saa 6 usiku akitaka music uzimwe watu wanywe kimya kimya utadhani wapo msibani.

Matendo ya DC Mtanda yanachangia kushusha mapato ya wafanyabiashara na Serekali.

Matendo ya DC Mtanda ya kuingiza polisi wenye bunduki katika sehemu starehe ni kuwaogopesha wateja na kuharibu biashara na kuzoretesha biashara pasipo sababu za maana.

DC Mtanda hastahili kuendelea na kazi za Mkuu wa Wilaya Arusha kama itakupendeza angepelekwa huko Turiani au Namtumbo kungemfaa zaidi.

Ngongo kwasasa The Pillar
Ahsante Mama kwa kutuondolea huyu DC Mshamba Mshamba,Wilaya uliyompeleka ni sahihi kabisa narudia tena ahsante sana.
 
Ahsante Mama kwa kutuondolea huyu DC Mshamba Mshamba,Wilaya uliyompeleka ni sahihi kabisa narudia tena ahsante sana.
Urambo Halmashauri wajiandae, DED lazima apelekeshwe ili DC apate mgao.
 
Hawa MaDC na MaRC washamba wapelekwe Ileje huko..Jiji kama Arusha inabidi liwe la kisasa kwelikweli..Watu wale burudani tena kwa kulindwa ikiwezekana..Patrol za kutosha 24/7.

Pia Usafi hili jiji bado haujawa wa kiwango cha kuridhisha.
 
Juzi nilikuwa natoka Dar muda wa saa 6 usiku nikapitia pale Hugo full shangwe music 🎶 mkubwa watu wanakula raha ungefikiri hakuna kesho.

Saa 8 naingia Arusha ukiwa umetamalaki kila sehemu nauliza kulikoni nasmbiwa DC Mtaka.

Hii nchi kuna sheria na taratibu za kila Mkoa au kila Wilaya kutegemea utashi wa kiongozi.
Hugo ni wapi
 
Na nyinyi acheni kuwapigia watu kelele kwa starehe zenu bhana. Wengine muda huo wanatakiwa kupumzisha akili.

DC yuko sahihi. Kama mnataka kuendelea kunywa kuanzia hiyo saa 6 usiku, zimeni mziki ili watu walale.

Na kama haiwezekani, basi wekeni sound proof.
Sawasawa na wavuta sigara
 
Lakini hii sheria si imepitishwa na mtanda ataki kua mnafki na anasimqmia sheria..
 
Haha naona mnazidi kumsagia kunguni mwananchi 🐼
 
Na hapa Mwanza kayatimba tena, alianza kumsaidia mmakonde mwenzake aliyekuwa RC wa Simiyu kumsafisha katika kesi ya ufiraji na jana katumia madaraka yake vibaya kuwasweka ndani viongozi wa timu ya Simba kutokana na mapenzi yake kwa timu yake ya Yanga na GSM. Huyu hafai hata kuwa afisa mtendaji sijui kwa nini Kizimkazi anamkumbatia.
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Back
Top Bottom