Rais Samia tukumbuke watumishi wa NIDA

Rais Samia tukumbuke watumishi wa NIDA

Poleni sana mkuu, Mungu atakisikia kilio chenu, mtajibiwa tu.

Tuendelee kumwamini Mungu.


JESUS IS LORD!
 
Mtetezi.com,
Nilikua nakuonea huruma ila baada ya hii comment nimejua kwanini ulikua kati ya walio timuliwa.

Sasa sikiliza..

Katika utumishi wa umma kuna kuchunguzwa na taarifa zinatumwa sehem husika kila mwezi.

Sasa baada ya uchunguzi wakaona wewe ni moja ya watoa huduma wenye majibu machafu na mtukana watu (kama ulivyo fanya hapa...)!

Nimeangalia comment za wadau na hii comment yako nimejiridhisha kwamba wewe ni mtu mwenye kauli chafu!

Na hii ndio sababu kwann ulikuwepo katika kundi la walio punguzwa!!

Na huwezi rudishwa maana tayari rais ana PDF yenu nyie watu wenye kauli mbovu kwa wananchi.
 
Kweli na unategemea mheshimiwa Rais wa jamuhuri apitie hapa kwenye comment kama hii?

Ukweli ni kwamba watumishi wengi huwa mmeweka dharau kwa wananchi na hata kuwasikiliza ni kama mnalazimishwa.


Mimi nasukuru nilipata kitambulisho mwaka 2014 hapa nawaza miaka miwili iliyobaki nitakuwa sina kitambulisho kwa mujibu wa utaratibu wenu utaifa eti ni miaka kumi una expire, sasa itabidi niende somalia nikachukue kitambulisho cha kudumu.




Sent using Jamii Forums mobile app
kwahiyo kuna watu vitambulisho vyao vita expire kabla hawajavipata?
 
Mtetezi.com,
Nilikua nakuonea huruma ila baada ya hii comment nimejua kwanini ulikua kati ya walio timuliwa.

Sasa sikiliza..

Katika utumishi wa umma kuna kuchunguzwa na taarifa zinatumwa sehem husika kila mwezi.

Sasa baada ya uchunguzi wakaona wewe ni moja ya watoa huduma wenye majibu machafu na mtukana watu (kama ulivyo fanya hapa...)!

Nimeangalia comment za wadau na hii comment yako nimejiridhisha kwamba wewe ni mtu mwenye kauli chafu!

Na hii ndio sababu kwann ulikuwepo katika kundi la walio punguzwa!!

Na huwezi rudishwa maana tayari rais ana PDF yenu nyie watu wenye kauli mbovu kwa wananchi.
Sawa boss

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Poleni , ndiyo mjifunze kuwa karimu wateja ona sasa, halafu mlijazana kindugulazation wengine hata kusoma hawajui tunafanya kuwachambulia hii form yangu, sisiem mlijazana jamani pambaneni tu!
 
Salamu za wazi kwako mama Samia, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!
Kazi iendelee!

Ninakuomba mama utukumbuke watumishi 598 tuliopunguzwa kazi mara tu baada ya Rais Magufuli kuingia na kumtumbua mkurugenzi wetu Dickson Mwaimu na kuteuliwa Bw Modestus Kapilimba kisha kutupunguza wafanyakazi 598 wa NIDA nchi nzima kwa kisingizio cha mrundikano wa wafanyakazi na kuacha uhaba mkubwa wa watumishi wa NIDA na ndio mana utoaji wa vitambulisho vya taifa umekuwa tatizo kubwa sana.

Mama watumishi wengi waliopunguzwa walishajitolea kwa zaidi ya miaka mitano wakiahidiwa na wakitegemea ajira za kudumu lakini haikuwa hivyo baada ya utawala wa awamu ya tano.

Kwa sasa wengi wetu tunaishi maisha magumu sana kwani ajira ni ngumu sana kupata na wengi wetu tuna familia zinatutegemea na pia watanzania wanateseka hawapati vitambulisho kwani NIDA inakabiliwa na uhaba mkubwa wa watumishi.

Tunaomba utufute machozi na jasho letu Mheshimiwa Rais.

Ninatanguliza shukurani zangu kwako mama.

By
Anonymous from Dar es Salaam
NIDA hakuna kazi mnafanya Bora watimuliwe wote
 
Kitambulisho changu kimekosewa jina yaani typing error ya aliyekuwa anafanya data entry nadhani, ila wakaniambia nilipie 20,000. Nikalipa nikafata taratibu zote. Toka 2019 mpaka leo sijaona sehem yoyote imebadilishwa. NIDA ni jipu
 
Nilijisajili 2014 ili kupata kitambulisho, kwa ile jeuri na dharau mliyonionyesha siku ile sitawasahau.
Mlifikiri sijui sijasoma, hivi huwa mnawaza kila anayekuja kwenu kujiandikisha hajasoma?
Kumbe mlifukuzwa eeh? Safi Sana na mfukuzwe tena huko mlipo
Ila siku nyingine punguzeni dharau na jeuri
Nilijua nimebaki peke yangu. Mimi tokea 2013 mkuu hadi leo holla. Hadi nimeacha kufuatilia nasubiri mwaka watakaonitumia msg ya kwenda kuchukua kitambulisho kama bado nitakuwa hai.
 
Back
Top Bottom