Mtetezi.com
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 3,134
- 3,571
Salamu za wazi kwako mama Samia, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania!
Kazi iendelee!
Ninakuomba mama utukumbuke watumishi 598 tuliopunguzwa kazi mara tu baada ya Rais Magufuli kuingia na kumtumbua mkurugenzi wetu Dickson Mwaimu na kuteuliwa Bw Modestus Kapilimba kisha kutupunguza wafanyakazi 598 wa NIDA nchi nzima kwa kisingizio cha mrundikano wa wafanyakazi na kuacha uhaba mkubwa wa watumishi wa NIDA na ndio mana utoaji wa vitambulisho vya taifa umekuwa tatizo kubwa sana.
Mama watumishi wengi waliopunguzwa walishajitolea kwa zaidi ya miaka mitano wakiahidiwa na wakitegemea ajira za kudumu lakini haikuwa hivyo baada ya utawala wa awamu ya tano.
Kwa sasa wengi wetu tunaishi maisha magumu sana kwani ajira ni ngumu sana kupata na wengi wetu tuna familia zinatutegemea na pia watanzania wanateseka hawapati vitambulisho kwani NIDA inakabiliwa na uhaba mkubwa wa watumishi.
Tunaomba utufute machozi na jasho letu Mheshimiwa Rais.
Ninatanguliza shukurani zangu kwako mama.
By
Anonymous from Dar es Salaam
Kazi iendelee!
Ninakuomba mama utukumbuke watumishi 598 tuliopunguzwa kazi mara tu baada ya Rais Magufuli kuingia na kumtumbua mkurugenzi wetu Dickson Mwaimu na kuteuliwa Bw Modestus Kapilimba kisha kutupunguza wafanyakazi 598 wa NIDA nchi nzima kwa kisingizio cha mrundikano wa wafanyakazi na kuacha uhaba mkubwa wa watumishi wa NIDA na ndio mana utoaji wa vitambulisho vya taifa umekuwa tatizo kubwa sana.
Mama watumishi wengi waliopunguzwa walishajitolea kwa zaidi ya miaka mitano wakiahidiwa na wakitegemea ajira za kudumu lakini haikuwa hivyo baada ya utawala wa awamu ya tano.
Kwa sasa wengi wetu tunaishi maisha magumu sana kwani ajira ni ngumu sana kupata na wengi wetu tuna familia zinatutegemea na pia watanzania wanateseka hawapati vitambulisho kwani NIDA inakabiliwa na uhaba mkubwa wa watumishi.
Tunaomba utufute machozi na jasho letu Mheshimiwa Rais.
Ninatanguliza shukurani zangu kwako mama.
By
Anonymous from Dar es Salaam