Rais Samia Suluhu Hassan usikubali kuyumbishwa

Mzalendo2015

JF-Expert Member
Aug 14, 2012
6,697
9,048
Mama yetu wa Taifa, mpendwa wetu nani kama Mama?

Umeanza vzr sana ktk siku zako 100 kwa kusimamia Haki, Sheria, Amani, Upendo na Mshikamano. Katika siku 100 tumehuhudia kesi za kubambikiwa zikifutwa, watu waliodhulumiwa wakirudishiwa haki zao, wapinzani wakijumuishwa kwene Serikali yako etc.

Kasoro imeanza kujitokeza juzi wakti CHADEMA na uongozi wake walipotangaza kufanya Kongamano la ndani kuhusu Katiba mpya!
Kitendo cha kuwakamata Viongozi Waandamizi wa CHADEMA huku Mwenyekiti Mhe. Freeman Aikael Mbowe akikamatwa na kurudishwa Dar @ KUJIBU KESI/TUHUMA ZA UGAIDI KUTAKA KUUA VIONGOZI WA KITAIFA ni DOA KUBWA KWA UTAWALA WAKO MAMA YANGU.

Nina shawishika kabisa haya siyo mawazo yako! Tatizo ninalo liona hapa ni MAHAFIDHINA WA CCM ambao wameanza KUKUPOTOSHA ili upoteze mwelekeo ili urudi kulekule kwa mtangulizi wako Hayati Magufuli. Mama siasa zinahitaji uvumilivu, upendo na mshikamano. Usije ukakubali Mahafidhina wa CCM waanze kukuyumbisha. Wengi wana hofu ya kupoteza maharaja!

Usikubali Mahafidhina waanze kukuyumbisha wakilitumia JESHI LA POLISI kukuchonganisha na Watanzania hasa Wapinzani. Haiwezekani Mhe. Mbowe akamatwe na RPC MWANZA kwa madai ya mkutano wa ndani @ usio na kibali!! Halafu Ghafla polisi wakabadilisha maelezo kuwa MHE. MBOWE AMERUDISHWA DAR ANAKODAIWA ALIPANGA MAUAJI YA VIONGOZI WA SERIKALI!! Huu uongo na utengenezaji wa matukio ili kuwanyamazisha Wapinzani utali gharimu Taifa.

Kwa sasa kuna hasira za Watz kuanza KUBAMBIKIWA UTITIRI WA KODI KWENYE MIAMALA YA SIMU NA MAFUTA YA MAGARI! Ulishatoa maelekezo kwa Mawaziri husika kuangalia kodi hizi. Lakini ujue kuna tabia ya Mawaziri Mahafidhina ndani ya CCM kubadilisha mtazamo/mwelekeo wa Watz ili waache kufuatilia mambo ya msingi yanayowagusa.

Hii ni aibu kubwa kwa Serikali inayotaka kuongoza nchi kwa MATUKIO YA KUBUMBA.

Wasaalamu.
 
Rais na vyombo vyake vya ndani hawakosei.wewe umekosea
Acha uzezeta kaka!
Unataka kusema Rais na vyombo vyake ni Malaika???
Unajua kuna masasahisho ya uozo aliofanya Hayati Magufuli na vyombo vyake anayafanya Rais Mama Samia kwa sasa. Je, kama hawakosei kwanini yanafanyika??
 
Yaani miezi michache tu madaraka yamesha mlevya mtu! Sijui mpaka 2025, itakuwaje!! Urais wenyewe ni wa zari tu la mentali!! Lakini siyo kujitutumua huko!!

ningekuwa ndiyo mimi, ningekuwa very humble! Ndani ya hii miaka minne, ningehakikisha Katiba Mpya ya Wananchi inapatikana kwa haki! Ningetanguliza maslahi ya Nchi kwanza, huku ya kwangu na chama yakifuatia!

Na hiyo 2025, nisingegombea!
Hakika ningestaafu kwa heshima.
 
Acha uzezeta kaka!
Unataka kusema Rais na vyombo vyake ni Malaika???
Unajua kuna masasahisho ya uozo aliofanya Hayati Magufuli na vyombo vyake anayafanya Rais Mama Samia kwa sasa. Je, kama hawakosei kwanini yanafanyika??
Umenitukana bure,ukisoma vizuri ujumbe wangu nitake radhi.(alisema Mimi Rais sikosei)
 
Mama yetu wa Taifa, mpendwa wetu nani kama Mama?

Umeanza vzr sana ktk siku zako 100 kwa kusimamia Haki, Sheria, Amani, Upendo na Mshikamano. Katika siku 100 tumehuhudia kesi za kubambikiwa zikifutwa, watu waliodhulumiwa wakirudishiwa haki zao, wapinzani wakijumuishwa kwene Serikali yako etc.

Kasoro imeanza kujitokeza juzi wakti CHADEMA na uongozi wake walipotangaza kufanya Kongamano la ndani kuhusu Katiba mpya!
Kitendo cha kuwakamata Viongozi Waandamizi wa CHADEMA huku Mwenyekiti Mhe. Freeman Aikael Mbowe akikamatwa na kurudishwa Dar @ KUJIBU KESI/TUHUMA ZA UGAIDI KUTAKA KUUA VIONGOZI WA KITAIFA ni DOA KUBWA KWA UTAWALA WAKO MAMA YANGU.

Nina shawishika kabisa haya siyo mawazo yako! Tatizo ninalo liona hapa ni MAHAFIDHINA WA CCM ambao wameanza KUKUPOTOSHA ili upoteze mwelekeo ili urudi kulekule kwa mtangulizi wako Hayati Magufuli. Mama siasa zinahitaji uvumilivu, upendo na mshikamano. Usije ukakubali Mahafidhina wa CCM waanze kukuyumbisha. Wengi wana hofu ya kupoteza maharaja!

Usikubali Mahafidhina waanze kukuyumbisha wakilitumia JESHI LA POLISI kukuchonganisha na Watanzania hasa Wapinzani. Haiwezekani Mhe. Mbowe akamatwe na RPC MWANZA kwa madai ya mkutano wa ndani @ usio na kibali!! Halafu Ghafla polisi wakabadilisha maelezo kuwa MHE. MBOWE AMERUDISHWA DAR ANAKODAIWA ALIPANGA MAUAJI YA VIONGOZI WA SERIKALI!! Huu uongo na utengenezaji wa matukio ili kuwanyamazisha Wapinzani utali gharimu Taifa.

Kwa sasa kuna hasira za Watz kuanza KUBAMBIKIWA UTITIRI WA KODI KWENYE MIAMALA YA SIMU NA MAFUTA YA MAGARI! Ulishatoa maelekezo kwa Mawaziri husika kuangalia kodi hizi. Lakini ujue kuna tabia ya Mawaziri Mahafidhina ndani ya CCM kubadilisha mtazamo/mwelekeo wa Watz ili waache kufuatilia mambo ya msingi yanayowagusa.

Hii ni aibu kubwa kwa Serikali inayotaka kuongoza nchi kwa MATUKIO YA KUBUMBA.

Wasaalamu.
Mama anayumba mwenyewe wala hajayumbishwa bado.
 
Yaani miezi michache tu madaraka yamesha mlevya mtu! Sijui mpaka 2025, itakuwaje!! Urais wenyewe ni wa zari tu la mentali!! Lakini siyo kujitutumua huko!!

ningekuwa ndiyo mimi, ningekuwa very humble! Ndani ya hii miaka minne, ningehakikisha Katiba Mpya ya Wananchi inapatikana kwa haki! Ningetanguliza maslahi ya Nchi kwanza, huku ya kwangu na chama yakifuatia!

Na hiyo 2025, nisingegombea!
Hakika ningestaafu kwa heshima.
Why kikundi cha wanaCDM wachache ndiyo wanakomaa na hiyo katiba bila uungaji mkono kutoka makundi mengine ya jamii?
 
.... CHADEMA wana siasa za confrontation. Wanang'ang'aniza wanachokihisi kinakinzana na CCM.

Alafu hawaelewi....Rais kasema "anataka kujenga uchumi'' wamuache kwanza. Au mpaka aseme hazina hakuna fedha? ( Jiwe kafilisi)

Hata Mama Samia akiweka mchakato wa katiba, bado watazua kingine.

Na kingine matusi ya wakina Mdude..walishapewa fair warning, 'tukosoane kistaarabu' wakaacha wapumbavu watukane kwenye majukwaa..Mbowe analipa gharama.
 
Why kikundi cha wanaCDM wachache ndiyo wanakomaa na hiyo katiba bila uungaji mkono kutoka makundi mengine ya jamii?
Suala la Katiba Mpya siyo la wanachadema wachache kama unavyo taka kupotosha! Ni la Watanzania walio wengi, isipokuwa nyinyi wachache mnao nufaika na hii Katiba ya 1977!

Wanachokifanya Chadema sasa, ni kuwasemea tu Wananchi walioshiriki kwenye mchakato wa kutoa mapendekezo yao, kiasi cha kusababisha kuandaliwa kwa Rasimu ya Katiba! Na ambayo mchakato wake uliishia kuvurugika kwenye Bunge la Katiba.
 
Raisi anaendesha nchi vizuri sana na pia alipanga kushirikiana vizuri na wapinzan ili kujenga nchi katika misingi iliyo bora ya amani, upendo na mshikamano. Lkn sasa wapinzan wenyewe ndio hawakutaka kushirikiana na raisi kwa lolote. Kwanza walianza kumtumia yule mnywa gongo kumvunjia mama heshima kwa kuja na kauli zisizopendeza kwa mtawala kuwa atamnyoa kwa wembe aliomnyoa mtangulizi wake, pili walipoona hiyo haitoshi wakaanza kuandaa makongomano ya kudai katiba bila vibali vya polisi na kujaribu kuonesha kwamba wao wanaweza kufanya chochote hata bila ya vibali vya serikali. Sasa kwa style hii ya upinzani unaopinga kila kitu kinachofanywa na serikali ikiwemo maandalizi ya kukutana nao wa kulaumiwa ni nani? Wao ilitakiwa wamuhitaji mama kwa maridhiano kuliko mama kuwahitaji wao ili kama wana ajenda zao za katiba na kadhalika wangeongea katika mkutano wao.. Ni serikali au raisi gani anaeweza kuvumilia upuuzi unaofanywa na wapinzani wa Tz.
 
  • Thanks
Reactions: mmh
Yaani miezi michache tu madaraka yamesha mlevya mtu! Sijui mpaka 2025, itakuwaje!! Urais wenyewe ni wa zari tu la mentali!! Lakini siyo kujitutumua huko!!

ningekuwa ndiyo mimi, ningekuwa very humble! Ndani ya hii miaka minne, ningehakikisha Katiba Mpya ya Wananchi inapatikana kwa haki! Ningetanguliza maslahi ya Nchi kwanza, huku ya kwangu na chama yakifuatia!

Na hiyo 2025, nisingegombea!
Hakika ningestaafu kwa heshima.
Mama ajakataa hoja ya katiba mpya amesema tusubiri kidogo ila kuna watu wanataka kumuonyesha umwamba nae wamemkuta yupo ngangari
 
Why kikundi cha wanaCDM wachache ndiyo wanakomaa na hiyo katiba bila uungaji mkono kutoka makundi mengine ya jamii?
Lengo ni kupiga hela za walalahoi kupitia vikao vya katiba. Ikumbukwe kuwa Chadema sasa hivi kiko hoi kifedha baada ya kugalagazwa katika sanduku la kura. Kwahiyo wanatafuta njia nyepesi ya kuwasaidia kupiga pesa za kuwalipa watu wanaokipigania chama huku mitandaoni.
 
Raisi anaendesha nchi vizuri sana na pia alipanga kushirikiana vizuri na wapinzan ili kujenga nchi katika misingi iliyo bora ya amani, upendo na mshikamano. Lkn sasa wapinzan wenyewe ndio hawakutaka kushirikiana na raisi kwa lolote. Kwanza walianza kumtumia yule mnywa gongo kumvunjia mama heshima kwa kuja na kauli zisizopendeza kwa mtawala kuwa atamnyoa kwa wembe aliomnyoa mtangulizi wake, pili walipoona hiyo haitoshi wakaanza kuandaa makongomano ya kudai katiba bila vibali vya polisi na kujaribu kuonesha kwamba wao wanaweza kufanya chochote hata bila ya vibali vya serikali. Sasa kwa style hii ya upinzani unaopinga kila kitu kinachofanywa na serikali ikiwemo maandalizi ya kukutana nao wa kulaumiwa ni nani? Wao ilitakiwa wamuhitaji mama kwa maridhiano kuliko mama kuwahitaji wao ili kama wana ajenda zao za katiba na kadhalika wangeongea katika mkutano wao.. Ni serikali au raisi gani anaeweza kuvumilia upuuzi unaofanywa na wapinzani wa Tz.
Ndugu,
Anachotakiwa Rais ni kuongoza nchi kwa utawala bora kwa kufuata Katiba na sheria za nchi. Mengine hayo ni matakataka tuliyokuwa tunaamini tumeisha yaacha kwa mwendazake.
Wananchi wanahitaji Katiba bora ya kuwezesha uwepo wa mifumo imara itakayohakikisha kuheshimiwa kwa haki za binadamu na kuleta/kuchochea maendeleo ya kweli. Ni haki yao ya msingo. Hatuhitaji kusikiliza leo kaamkaje.
 
Ndugu,
Anachotakiwa Rais ni kuongoza nchi kwa utawala bora kwa kufuata Katiba na sheria za nchi. Mengine hayo ni matakataka tuliyokuwa tunaamini tumeisha yaacha kwa mwendazake.
Wananchi wanahitaji Katiba bora ya kuwezesha uwepo wa mifumo imara itakayohakikisha kuheshimiwa kwa haki za binadamu na kuleta/kuchochea maendeleo ya kweli. Ni haki yao ya msingo. Hatuhitaji kusikiliza leo kaamkaje.
Uongozi bora kwani aliomba kura kwa wananchi aongoze.
Utawala bora ni mifumo ya kijeshi,kifalme,kisultani na kichifu.Hawa hawaombi kura kwa wananchi
 
Suala la Katiba Mpya siyo la wanachadema wachache kama unavyo taka kupotosha! Ni la Watanzania walio wengi, isipokuwa nyinyi wachache mnao nufaika na hii Katiba ya 1977!

Wanachokifanya Chadema sasa, ni kuwasemea tu Wananchi walioshiriki kwenye mchakato wa kutoa mapendekezo yao, kiasi cha kusababisha kuandaliwa kwa Rasimu ya Katiba! Na ambayo mchakato wake uliishia kuvurugika kwenye Bunge la Katiba.
Hivi mchakato wa Bunge la Katiba ulivugikaje?
 
Back
Top Bottom