Chief Kabikula
JF-Expert Member
- Jan 1, 2019
- 7,567
- 9,026
Wandugu kwa kuwa rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania ameonyesha uungwana kwa kukubali kukutana na vyama vya upinzani kwa maslahi mapana ya nchi, tayari ameshakutana na wazee wa Dar es Salaam. Kwa uungwana huo aliouonyesha kujali makundi mbalimbali na kupata mawazo, kero, ushauri ninatabiri atafika mbali na kufanikiwa iwapo atakubali ushauri kutoka kwa Mtanzania yeyote yule na kutoka popote pale, ndani ya nchi au nje.
Kwakuwa ameahidi kuteua Mtanzania yeyote yule mwenye weledi bila kujali chama atakacho, mimi namshauri akutane na sisi wakosoaji wakubwa wa CCM na serikali tuliopo mtandaoni, kuanzia sisi tuliopo JF, Twitter, Instagram, Facebook ili apate michango, maoni, ushauri, mapendekezo na kero mbalimbali zilizopo nchini ili azifanyie kazi na kazi yake itakuwa nyepesi sana maana kwenye mitandao humu kuna watu wa aina tofauti tofauti wenye elimu na ujuzi tofauti.
Ushauri kwa kuwa zama za vitisho, utekaji zinaelekea kupotea au kuisha wawakilishi wote waliopo mitandaoni tuende ikulu tumevaa mask zilizoandikwa ID zetu kama utambulisho. Angalizo wanaoogopa kwenda hawalazimishwi wakae kushoto hii ni nchi yetu sote.
Jahazi litaongozwa na mimi Chief Kabikula, baadhi ya ajenda ni Katiba mpya, tume huru ya uchaguzi, uchumi, ajira, demokrasia, utawala bora, uwekezaji, mahusiano ya kimataifa, Kuachiwa wafungwa wa kisiasa na watu wote waliopo jela au rumande kwa makosa yaliyotokana na uchaguzi mkuu na uchaguzi wa serikali za mitaa na mada nyingine mtakazopendekeza wakuu.
Kwakuwa ameahidi kuteua Mtanzania yeyote yule mwenye weledi bila kujali chama atakacho, mimi namshauri akutane na sisi wakosoaji wakubwa wa CCM na serikali tuliopo mtandaoni, kuanzia sisi tuliopo JF, Twitter, Instagram, Facebook ili apate michango, maoni, ushauri, mapendekezo na kero mbalimbali zilizopo nchini ili azifanyie kazi na kazi yake itakuwa nyepesi sana maana kwenye mitandao humu kuna watu wa aina tofauti tofauti wenye elimu na ujuzi tofauti.
Ushauri kwa kuwa zama za vitisho, utekaji zinaelekea kupotea au kuisha wawakilishi wote waliopo mitandaoni tuende ikulu tumevaa mask zilizoandikwa ID zetu kama utambulisho. Angalizo wanaoogopa kwenda hawalazimishwi wakae kushoto hii ni nchi yetu sote.
Jahazi litaongozwa na mimi Chief Kabikula, baadhi ya ajenda ni Katiba mpya, tume huru ya uchaguzi, uchumi, ajira, demokrasia, utawala bora, uwekezaji, mahusiano ya kimataifa, Kuachiwa wafungwa wa kisiasa na watu wote waliopo jela au rumande kwa makosa yaliyotokana na uchaguzi mkuu na uchaguzi wa serikali za mitaa na mada nyingine mtakazopendekeza wakuu.