Katika uongozi wake, Rais Samia Suluhu Hassan ameweka mkazo mkubwa kwenye kuimarisha sekta ya kilimo (sekta inayoajiri 60% ya watanzania), hatua inayojenga msingi wa maendeleo jumuishi ya taifa. Tathmini ya sera, mikakati na hatua zilizochukuliwa zinaonyesha mwelekeo mzuri wa kulibadilisha kilimo kuwa sekta yenye tija zaidi kiuchumi.
Uwekezaji na Uanzishaji wa Benki Mpya
Leo hii tunaenda kushuhudia uzinduzi wa Benki ya Ushirika ikiwa na mtaji wa Shilingi bilioni 55, hii ni hatua muhimu ya kuimarisha upatikanaji wa mitaji kwa wakulima. Muundo wa umiliki wa hisa-51% kwa wanaushirika na 49 kwa sekta binafsi, unaashiria dhamira ya kuimarisha ushiriki wa wakulima katika usimamizi wa rasilimali.
Mageuzi katika Bajeti ya Kilimo
Katika kipindi cha miaka 5 iliyopita bajeti ya Wizara ya Kilimo imeongezeka kutoka bilioni 229.8 mwaka 2020/21 mpaka Trilioni 1.2 mwaka 2024/25 (Kibajeti mageuzi ya namna hii hayajawahi kutokea Afrika). Mfano; Bajeti ya umwagiliaji ilikuwa Bilioni 12.8 kwa mwaka 2020/21 na sasa ni Bilioni 403.8 mwaka 2024/25.
Programu za Maendeleo kwa Vijana na Wanawake
Kupitia programu kama Building a Better Tomorrow (BBT), vijana wanapewa mafunzo, mitaji na uunganishwaji na masoko. Hii inalenga kuzalisha kizazi kipya cha wakulima wanaotumia mbinu bora za kisasa na kuchangia mapinduzi ya kilimo nchini.
Mikakati ya serikali, utekelezaji wa hatua hizi unatarajiwa kuongeza mchango wa sekta ya kilimo kwenye Pato la Taifa. Aidha, uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara unatarajiwa kuongezeka kwa wastani wa asilimia 5 hadi 7 kila mwaka, jambo litakalo ifanya Tanzania iwe kati ya vinara wazalishaji wa chakula Barani Afrika.
Kwa kuzingatia mikakati iliyowekwa na hatua zinazochukuliwa kwa vitendo, mageuzi yanayoletwa na Rais Samia katika sekta ya kilimo yanaweka msingi wa maendeleo endelevu na kuongeza matumaini kwa mamilioni ya Watanzania. Kwa mara nyingine, kilimo kinawekwa kwenye nafasi yake sahihi kama mhimili wa uchumi wa taifa.
#SamiaTena #MguuKwaMguu
Uwekezaji na Uanzishaji wa Benki Mpya
Leo hii tunaenda kushuhudia uzinduzi wa Benki ya Ushirika ikiwa na mtaji wa Shilingi bilioni 55, hii ni hatua muhimu ya kuimarisha upatikanaji wa mitaji kwa wakulima. Muundo wa umiliki wa hisa-51% kwa wanaushirika na 49 kwa sekta binafsi, unaashiria dhamira ya kuimarisha ushiriki wa wakulima katika usimamizi wa rasilimali.
Mageuzi katika Bajeti ya Kilimo
Katika kipindi cha miaka 5 iliyopita bajeti ya Wizara ya Kilimo imeongezeka kutoka bilioni 229.8 mwaka 2020/21 mpaka Trilioni 1.2 mwaka 2024/25 (Kibajeti mageuzi ya namna hii hayajawahi kutokea Afrika). Mfano; Bajeti ya umwagiliaji ilikuwa Bilioni 12.8 kwa mwaka 2020/21 na sasa ni Bilioni 403.8 mwaka 2024/25.
Programu za Maendeleo kwa Vijana na Wanawake
Kupitia programu kama Building a Better Tomorrow (BBT), vijana wanapewa mafunzo, mitaji na uunganishwaji na masoko. Hii inalenga kuzalisha kizazi kipya cha wakulima wanaotumia mbinu bora za kisasa na kuchangia mapinduzi ya kilimo nchini.
Mikakati ya serikali, utekelezaji wa hatua hizi unatarajiwa kuongeza mchango wa sekta ya kilimo kwenye Pato la Taifa. Aidha, uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara unatarajiwa kuongezeka kwa wastani wa asilimia 5 hadi 7 kila mwaka, jambo litakalo ifanya Tanzania iwe kati ya vinara wazalishaji wa chakula Barani Afrika.
Kwa kuzingatia mikakati iliyowekwa na hatua zinazochukuliwa kwa vitendo, mageuzi yanayoletwa na Rais Samia katika sekta ya kilimo yanaweka msingi wa maendeleo endelevu na kuongeza matumaini kwa mamilioni ya Watanzania. Kwa mara nyingine, kilimo kinawekwa kwenye nafasi yake sahihi kama mhimili wa uchumi wa taifa.
#SamiaTena #MguuKwaMguu