Rais Samia hii miradi imekukosea nini?

Etwege

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2018
Posts
7,822
Reaction score
19,485
Serikali ya awamu ya 6 inayoongozwa na Rais Samia ina aleji kubwa na miradi ya kimkakati iliyoanzishwa kwa lengo la kumaliza matatizo ya watanzania.

Rais Samia amegoma kuuzindua mradi wa bwawa la Nyerere uliojengwa kwa lengo la kukomesha tatizo la umeme ndani ya nchi.

Rais Samia amegoma kuzindua barabara ya njia nane kutoka kimara hadi Kibaha uliojengwa kwa ajili ya kukomesha tatizo la foleni jijini.

Rais Samia amegoma kuipa msukumo bandari kavu ya kwala ili ijae makontena yatakayozuia foleni malori kuingia jijini na kuongeza foleni lakini pia kuharibu barabara za mitaa vibaya sana. Kila kona ya jiji sasa hivi wanajenga ICD za kuhifadhi makontena!

Rais Samia amegoma kuupa uzito mradi wa reli ya SGR hali iliyopelekea kipande cha Mwanza mkandarasi kufukuza wafanyakazi na kusuasua sana.

Serikali ya Samia haijulikani ni nini na iko uchumi gani maana uchumi wa kati tulishatolewa!
Serikali ya Samia yatenga Tzs trillion 1 kwa ajili ya safari.

Inasikitisha sana
 
ni zaidi ya kusikitisha
 
Nchi imeuzwa hii
 
Jhnpp inazinduliwa tarehe 21/8/26. Una la ziada?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…