Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,519
- 41,032
Natambua kuwa Rais Samia anataka kuvutia uwekezaji wa ndani na nje lakini hajagusa maeneo ya msingi ambayo yanaangaliwa na wawekezaji.
1) Nchi ambayo sheria za kodi zinabadilishwa kila mwaka, kamwe haiwezi kuvutia uwekezaji mkubwa kutoka kwa wawekezaji makini
Kati ya vigezo vikubwa vinavyoangaliwa na wawekezaji ili wakawekeze wapi, namba moja ni stability of fiscal regime. Hakuna mwekezaji anayeweza kwenda kuwekeza mahali ambapo, unaamua kuwekeza, kodi ni nyingine, unaanza kutengeneza miundombinu yako, kodi imebadilishwa, unamalizia kujenga, kodi imebadilika, unaingiza mitambo kodi imebadilika. Nchi ya namna hiyo, wawekezaji utakaowapata ni wale wa kufanya uchuuzi. Wale wa kuagiza bidhaa China, Thailand, Uturuki na India. Hawa wanaangalia, kodi ikiwa mbaya, wanaacha kuagiza. Ndiyo maana mpaka leo hii, pamoja na kelele na vikao vingi vya kuvutia wawekezaji, mwekezaji wa mwisho mkubwa alikuwa Dangote, ambaye naye anajutia kwa nini aliamua kuja kuwekeza Tanzania.
2) Utawala wa Sheria. Hili ni eneo ambalo wawekezaji wanalitazama sana
Huwezi kwenda kuwekeza mahali ambapo hakuna utawala wa sheria. Rais anaweza kubadilisha chochote, Waziri anaweza kubadilisha chochote, DC, RC, RPC, OCD, anaweza kukusweka ndani wakati wowote bila kosa lolote, na bila kufuata sheria. Mwekezaji ambaye maisha yake yote hajawahi kukaa mahabusu, hajawahi kushtakiwa, anaheshimika kwao ja mahali pengine Duniani, anafika Tanzania, mjinga mmoja anatoa amri, weka huyo ndani, na anawekwa ndani. Mfano mzuri ni yule mkurugenzi wa kiwanda cha Tumbaku Morogoro aliyelazwa kwenye mahabusu za polisi kwa amri ya RCO, sababu tu TCO amepokea majungu toka kwa wafanyakazi. Kinachompa mtu uhakika wa anachokifanya ni sheria, na jinsi sheria hiyo inavyoheshimiwa na Serikali.
3) Kushindwa kuelewa competetiveness ya Dunia katika kuwapata wawekezaji
Dunia nzima, nchi tajiri na maskini, zote zinawatafuta wawekezaji. Kiongozi mkuu wa China kila wakati yupo Ulaya kutafuta wawekezaji wa kuwekeza China, Saudi Arabia timu yao ipo Marekani wakati wote kutafuta wawekezaji, UK inatafuta wawekezaji, Dubai wanatafuta wawekezaji. Nchi yetu Tanzania ina nini cha pekee ambacho tunaweza kusema ndiyo strength yetu dhidi ya nchi nyingine katika kuwapata wawekezaji?
Umeme wako bei juu na hauna uhakika, njia usafirishaji ni aghali na wakati fulani mbovu, malighafi nyingi hakuna, utawala wa sheria hauheshimiwi, kodi juu na zinazobadilika kila leo, ni nini cha pekee unachozidi wengine hata umfanye mwekezaji mkubwa asiende China, Brazil, Vietnam, Hong Kong Malaysia au UAE, badala yakeaje Tanzania?
Serikali ijifunze kutoka Uingereza waliowahi kukaa na sheria ya uwekezaji kwa zaidi ya miaka 50, bila kuibadilisha ili kuwapa confidence wawekezaji.
Serikali ijifunze toka Dubai, Ghana, Mauritius katika kuwa na kodi za chini na rafiki za kuvutia wawekezaji.
Serikali ijifunze toka Malaysia katika kuheshimu wawekezaji.
Serikali ijifunze toka Botswana na Namibia katika kuheshimu mikataba ya uwekezaji.
Serikali ijifunze toka Singapore katika kuhakikisha Serikali inaajili super intelligent people katika ofisi za Serikali, na hasa zinazoshughulika na uwekezaji, kodi na utawala badala ya kuteua makada wa chama, ambao wengi wao uelewa wao katika uchumi wa Dunia, biashara, uwekezaji na utawala bora, ni mdogo sana.
Mataifa hayo niliyoyataja yote yamefanikiwa sana katika kuvutia wawekezaji.
Rais kama unataka kuvutia uwekezaji, kuinua uchumi, kutengeneza ajira, kuongeza uwigo wa kodi na mapato ya Serikali, kwanza kwa haraka badilisha sheria mbalimbali zinazohusiana na uwekezaji, kodi, na utawala wa sheria ili kuhakikisha tunakuwa washindani imara katika kuvutia wawekezaji. Vinginevyo, utazunguka Dunia nzima, utafanya vikao na wawekezaji mbalimbali, watakusikiliza, watakupa heshima na matumaini, lakini mwishowe hutawapata. Wawekezaji siyo wajinga, wengine ni practical super intelligent people, hawaendi kuwekeza mahali kwa sababu Rais amesema au amewakaribisha bali wanaangalia utimilifu wa selection criteria.
1) Nchi ambayo sheria za kodi zinabadilishwa kila mwaka, kamwe haiwezi kuvutia uwekezaji mkubwa kutoka kwa wawekezaji makini
Kati ya vigezo vikubwa vinavyoangaliwa na wawekezaji ili wakawekeze wapi, namba moja ni stability of fiscal regime. Hakuna mwekezaji anayeweza kwenda kuwekeza mahali ambapo, unaamua kuwekeza, kodi ni nyingine, unaanza kutengeneza miundombinu yako, kodi imebadilishwa, unamalizia kujenga, kodi imebadilika, unaingiza mitambo kodi imebadilika. Nchi ya namna hiyo, wawekezaji utakaowapata ni wale wa kufanya uchuuzi. Wale wa kuagiza bidhaa China, Thailand, Uturuki na India. Hawa wanaangalia, kodi ikiwa mbaya, wanaacha kuagiza. Ndiyo maana mpaka leo hii, pamoja na kelele na vikao vingi vya kuvutia wawekezaji, mwekezaji wa mwisho mkubwa alikuwa Dangote, ambaye naye anajutia kwa nini aliamua kuja kuwekeza Tanzania.
2) Utawala wa Sheria. Hili ni eneo ambalo wawekezaji wanalitazama sana
Huwezi kwenda kuwekeza mahali ambapo hakuna utawala wa sheria. Rais anaweza kubadilisha chochote, Waziri anaweza kubadilisha chochote, DC, RC, RPC, OCD, anaweza kukusweka ndani wakati wowote bila kosa lolote, na bila kufuata sheria. Mwekezaji ambaye maisha yake yote hajawahi kukaa mahabusu, hajawahi kushtakiwa, anaheshimika kwao ja mahali pengine Duniani, anafika Tanzania, mjinga mmoja anatoa amri, weka huyo ndani, na anawekwa ndani. Mfano mzuri ni yule mkurugenzi wa kiwanda cha Tumbaku Morogoro aliyelazwa kwenye mahabusu za polisi kwa amri ya RCO, sababu tu TCO amepokea majungu toka kwa wafanyakazi. Kinachompa mtu uhakika wa anachokifanya ni sheria, na jinsi sheria hiyo inavyoheshimiwa na Serikali.
3) Kushindwa kuelewa competetiveness ya Dunia katika kuwapata wawekezaji
Dunia nzima, nchi tajiri na maskini, zote zinawatafuta wawekezaji. Kiongozi mkuu wa China kila wakati yupo Ulaya kutafuta wawekezaji wa kuwekeza China, Saudi Arabia timu yao ipo Marekani wakati wote kutafuta wawekezaji, UK inatafuta wawekezaji, Dubai wanatafuta wawekezaji. Nchi yetu Tanzania ina nini cha pekee ambacho tunaweza kusema ndiyo strength yetu dhidi ya nchi nyingine katika kuwapata wawekezaji?
Umeme wako bei juu na hauna uhakika, njia usafirishaji ni aghali na wakati fulani mbovu, malighafi nyingi hakuna, utawala wa sheria hauheshimiwi, kodi juu na zinazobadilika kila leo, ni nini cha pekee unachozidi wengine hata umfanye mwekezaji mkubwa asiende China, Brazil, Vietnam, Hong Kong Malaysia au UAE, badala yakeaje Tanzania?
Serikali ijifunze kutoka Uingereza waliowahi kukaa na sheria ya uwekezaji kwa zaidi ya miaka 50, bila kuibadilisha ili kuwapa confidence wawekezaji.
Serikali ijifunze toka Dubai, Ghana, Mauritius katika kuwa na kodi za chini na rafiki za kuvutia wawekezaji.
Serikali ijifunze toka Malaysia katika kuheshimu wawekezaji.
Serikali ijifunze toka Botswana na Namibia katika kuheshimu mikataba ya uwekezaji.
Serikali ijifunze toka Singapore katika kuhakikisha Serikali inaajili super intelligent people katika ofisi za Serikali, na hasa zinazoshughulika na uwekezaji, kodi na utawala badala ya kuteua makada wa chama, ambao wengi wao uelewa wao katika uchumi wa Dunia, biashara, uwekezaji na utawala bora, ni mdogo sana.
Mataifa hayo niliyoyataja yote yamefanikiwa sana katika kuvutia wawekezaji.
Rais kama unataka kuvutia uwekezaji, kuinua uchumi, kutengeneza ajira, kuongeza uwigo wa kodi na mapato ya Serikali, kwanza kwa haraka badilisha sheria mbalimbali zinazohusiana na uwekezaji, kodi, na utawala wa sheria ili kuhakikisha tunakuwa washindani imara katika kuvutia wawekezaji. Vinginevyo, utazunguka Dunia nzima, utafanya vikao na wawekezaji mbalimbali, watakusikiliza, watakupa heshima na matumaini, lakini mwishowe hutawapata. Wawekezaji siyo wajinga, wengine ni practical super intelligent people, hawaendi kuwekeza mahali kwa sababu Rais amesema au amewakaribisha bali wanaangalia utimilifu wa selection criteria.