Rais Samia aweka jiwe la msingi ujenzi wa bandari ya Samaki Kilwa

MANKA MUSA

JF-Expert Member
Jul 9, 2014
922
1,093
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan leo September 19 ameweka Jiwe la Msingi kwenye ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa pamoja na kugawa wa Boti 34 kati ya 160 zilizonunuliwa na Serikali kwa Wavuvi na Wakulima wa Mwani.

Hayo yamejiri Wakati wa Ziara ya Kikazi Mkoani Lindi Wilaya ya Kilwa ambapo Rais Samia amesema Ujenzi wa Bandari hiyo utagharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 260 na itachukuwa muda wa miezi 36 kukamilika.

Kuhusu Boti 34 kati 160 alizogawa kwa Wavuvi, Rais Dkt,Samia amesema boti hizo zinatolewa kwa mkopo nafuu na kuwataka Wavuvi waliokabidhiwa kurejesha mkopo kwa wakati.

Hata hivyo Rais Samia amesema Serikali imekusudia kufufua mji wa Kilwa kiuchumi na kuurudisha kwenye hadhi yake kama zamani.

IMG-20230919-WA0003.jpg
IMG-20230919-WA0004.jpg
IMG-20230919-WA0002.jpg
 
Bandari ya uvuvi kwa uvuvi wa boti wapi na wapi? Wangejenga kwanza Dar es salaam hiyo bandari ya uvuvi.

Angesema serikali ina mpango wa kununua meli kubwa za uvuvi zile za kwenda kuvua papa na jodari deep sea tungeelewa habari ya bandari ya uvuvi.
 
Wajinga waliwahi kusikika wakisema tumegawa nchi yetu dubai, hauruhusiwi kujenga chochote, eti tumegawa authority zetu kwa dubai, eti hatuna tena chetu, eti uwekezaji wowote lazima dubai apitie na kuuridhia, "hadithi za wapumbavu na Upumbavu wao"
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt,Samia Suluhu Hassan leo September 19 ameweka Jiwe la Msingi kwenye ujenzi wa Bandari ya Uvuvi Kilwa pamoja na kugawa wa Boti 34 kati ya 160 zilizonunuliwa na Serikali kwa Wavuvi na Wakulima wa Mwani.

Hayo yamejiri Wakati wa Ziara ya Kikazi Mkoani Lindi Wilaya ya Kilwa ambapo Rais Samia amesema Ujenzi wa Bandari hiyo utagharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 260 na itachukuwa muda wa miezi 36 kukamilika.

Kuhusu Boti 34 kati 160 alizogawa kwa Wavuvi, Rais Dkt,Samia amesema boti hizo zinatolewa kwa mkopo nafuu na kuwataka Wavuvi waliokabidhiwa kurejesha mkopo kwa wakati.

Hata hivyo Rais Samia amesema Serikali imekusudia kufufua mji wa Kilwa kiuchumi na kuurudisha kwenye hadhi yake kama zamani.

View attachment 2755191View attachment 2755192View attachment 2755193
Kwani DP WORLD ameshaombwa ruhusa na kuridhia?
 
Bandari ya uvuvi kwa uvuvi wa boti wapi na wapi? Wangejenga kwanza Dar es salaam hiyo bandari ya uvuvi.

Angesema serikali ina mpango wa kununua meli kubwa za uvuvi zile za kwenda kuvua papa na jodari deep sea tungeelewa habari ya bandari ya uvuvi.
Muhimu ni hiyo bandari. Kukiwa na bandari, hapo ndipo hata kampuni binafsi za uvuvi zinaweza kuwepo. Hizo kampuni binafsi za uvuvi ndizo zinaweza kufikiria kununua meli za uvuvi. Hizo boti bila shaka ni kwa ajili ya wavuvi wadogo.
 
Muhimu ni hiyo bandari. Kukiwa na bandari, hapo ndipo hata kampuni binafsi za uvuvi zinaweza kuwepo. Hizo kampuni binafsi za uvuvi ndizo zinaweza kufikiria kununua meli za uvuvi. Hizo boti bila shaka ni kwa ajili ya wavuvi wadogo.
Kuna watu wamepigwa ganzi ya akili na wanaojihisi kuwa ni wajuaji, wao hakuna jema.......ni kuponda kila kitu bila hata kufikiria.
 
Back
Top Bottom