I am Groot
JF-Expert Member
- Jul 20, 2018
- 3,730
- 10,033
“Kuna Mwanangu (Goodluck Gozbert) aliimba ‘hauwezi kushindana na Mwanadamu mwenye kinywa’, mwenye kinywa atasema tu anayotaka kusema lakini ukweli utabaki palepale, chanjo hizi za Covid-19 zinasaidia kupunguza maumivu na hatari ya vifo kwa Watu".
“Chanjo hatusemi ni kinga kabisakabisa lakini hata Covid-19 ikikupata inakupata polepole, risk za kufa kwa wingi zinapungua, niwaombe Wanamichezo Kama mnataka kuendelea na michezo vizuri chanjeni, Mimi Mama yenu, Mkuu wenu, sitapeleka Jamii yangu kwenye hatari”.
“Chanjo ni muhimu, niwape mfano kuna Watu tumechanja nao lakini kwa bahati mbaya virusi vya Corona vikawanyemelea, wamekwenda tu vizuri na shughuli zao unampigia simu anasema niko vizuri baada ya siku tatu, nne ameenda kupima hakuna hicho kitu”.
“Chanjo hatusemi ni kinga kabisakabisa lakini hata Covid-19 ikikupata inakupata polepole, risk za kufa kwa wingi zinapungua, niwaombe Wanamichezo Kama mnataka kuendelea na michezo vizuri chanjeni, Mimi Mama yenu, Mkuu wenu, sitapeleka Jamii yangu kwenye hatari”.
“Chanjo ni muhimu, niwape mfano kuna Watu tumechanja nao lakini kwa bahati mbaya virusi vya Corona vikawanyemelea, wamekwenda tu vizuri na shughuli zao unampigia simu anasema niko vizuri baada ya siku tatu, nne ameenda kupima hakuna hicho kitu”.